Pongezi za wanaJamiiForums kwa Rais Magufuli kwa kupambana na wahujumu wa madini yetu

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,652
466996da971d7a10493f7fdd25079fc8.jpg
Wakuu habari zenu. Poleni na Majukumu ya hapa na pale.

Ni matumaini yangu kuwa, asilimia kubwa ya members wa JF ni watu wazima kabisa na wanaojielewa. Kwa uelewa wangu, mtu mzima anayejielewa hawezi jumuika katika maandamano yayosemekana kuandaliwa kwa nia ya kumpongeza JPM kwa hatua aliyofikia mpaka sasa juu ya Wizi wa Mali za Umma hasa madini yetu yaliyokuwa yakisombwa na Acacia.

Hivyo basi, Ninapendekeza kwa wale wanajamii forum walioguswa na wangependa kutoa pongezi au shukurani zao za dhati kwa Rais JPM, tuchukue nafasi hii kufanya ivyo kupitia uzi huu.

Si vibaya kumpongeza mtu hata kama kafanya mabaya mengi lakini hata akifanya zuri moja tu ni vyema kumpongeza ili aendelee kufanya mazuri kama haya.

Mi binafsi ningeaza kwa kumpa hongera kwa hatua aliyofikia mpaka sasa. Mi ni mmoja wa wale tulidhani ni maigizo ya kutafta kiki kwa pikipiki. ila hivi leo tumeanza muelewa. Ningependa pia kumkumbusha kuwa hata sisi Wapinzani ni Watanzania. Sisi wote ni ndugu. Tunataka maendeleo ila undugu wetu pia tunapenda uendelee kama alivyoukuta....

ANGALIZO.
Napendekeza tutoe pongezi bila mihemko. Ninajua wapo baadhi yenu ambao mnaweza kuwa tofauti au mkipingana na hatua alizochukua Magufuli. Ila ningewaomba kama mpo opposite mpite kushoto maana uzi huu hauwahusu.
 
hivi ni kweli kwamba hajawahi kupiga makofi ya ndiooooo wakati fulani wapinzani walipoibua izo hoja yeye akiwa mbunge wa kawaida? toeni kwanza ilo jibu ndio apewe pongezi.alafu, mbona mafisi wote ni ccm? si mpongezane ninyi masisiemu wenyewe kwa wenyewe? wezi ninyi, kila kitu ninyi afu mnatushirikisha wizi wenu.
 
Hata mimi nampongeza kwa hatua alizochukua mpaka sasa kwenye sakata la raslimali. Ila nampa angalizo asigeuze hili jambo kuwa kick ya kisiasa kwa chama chake.
 
Pongezi kwako Mh.Rais wewe ndio chaguo letu watanzania
Na tunaamini Umeletwa na mungu kulisaidia Taifa letu
Mwenyezi mungu akupe nguvu,ulinzi na afya tele.
Akulinde na Mashetani wakila aina ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania.
Tunaona juhudi zako kwa kipindi kifupi
Hivisasa watanzania twajiona Wenye kubarikiwa na kutoka kifua Mbele
Yote ni juu yako Mh.Rais.
 
hivi ni kweli kwamba hajawahi kupiga makofi ya ndiooooo wakati fulani wapinzani walipoibua izo hoja yeye akiwa mbunge wa kawaida? toeni kwanza ilo jibu ndio apewe pongezi.alafu, mbona mafisi wote ni ccm? si mpongezane ninyi masisiemu wenyewe kwa wenyewe? wezi ninyi, kila kitu ninyi afu mnatushirikisha wizi wenu.
Mkuuu upo sawa ila huu uzi haukuhusu.
 
Wakuu habari zenu. Poleni na Majukumu ya hapa na pale.

Ni matumaini yangu kuwa, asilimia kubwa ya members wa JF ni watu wazima kabisa na wanaojielewa. Kwa uelewa wangu, mtu mzima anayejielewa hawezi jumuika katika maandamano yayosemekana kuandaliwa kwa nia ya kumpongeza JPM kwa hatua aliyofikia mpaka sasa juu ya Wizi wa Mali za Umma hasa madini yetu yaliyokuwa yakisombwa na Acacia.

Hivyo basi, Ninapendekeza kwa wale wanajamii forum walioguswa na wangependa kutoa pongezi au shukurani zao za dhati kwa Rais JPM, tuchukue nafasi hii kufanya ivyo kupitia uzi huu.

Si vibaya kumpongeza mtu hata kama kafanya mabaya mengi lakini hata akifanya zuri moja tu ni vyema kumpongeza ili aendelee kufanya mazuri kama haya.

Mi binafsi ningeaza kwa kumpa hongera kwa hatua aliyofikia mpaka sasa. Mi ni mmoja wa wale tulidhani ni maigizo ya kutafta kiki kwa pikipiki. ila hivi leo tumeanza muelewa. Ningependa pia kumkumbusha kuwa hata sisi Wapinzani ni Watanzania. Sisi wote ni ndugu. Tunataka maendeleo ila undugu wetu pia tunapenda uendelee kama alivyoukuta....

ANGALIZO.
Napendekeza tutoe pongezi bila mihemko. Ninajua wapo baadhi yenu ambao mnaweza kuwa tofauti au mkipingana na hatua alizochukua Magufuli. Ila ningewaomba kama mpo opposite mpite kushoto maana uzi huu hauwahusu.
Pongezi kwa rais wetu,
KWA NIABA YA WANAJAMII FORUMS WOTE TUNAMPONGEZA RAIS NA SERIKALI YAKE!
 
Sisi tuliojitoa ufahamu tunaweza najua nyie hamwezia kwani hamkuwa na muda huo zaidi ya kuangaika na maisha yenu ya leo na kesho. Watu wengine sio wa mchezomchezo kwani hawajazoea kuishi leo tu na kesho ipo
 
Lini tena bunge na wanaccm wataandamana kwa kuwakamata rugemarila na Habindersing seti?
Na watakataa kabisa kama hawa kupiga makofi kikwete aliposema pesa sio zetu!

NChi hii bila unafiki haiendi
 
Hii ndio barabara ya bulyankulu segese ntobo kahama hii barabara imepitisha makinikia kwa kiwango kikubwa hii bara bara inayotumiwa na migodi mikubwa miwili accacia na GGM geita inanitia uchungu sana ndugu zangu watanzania tumuunge mkono raisi wa jamhuri ya muungano joseph pombe magufuli
mqdefault.jpg
 
Hii ndio barabara ya bulyakulu segese ntobo kahama hii barabara imepitisha makinikia kwa kiwango kikubwa hii bara bara inayotumiwa na migodi mikubwa miwili accacia na GGM geita inanitia uchungu sana ndugu zangu watanzania tumuunge mkono raisi wa jamhuri ya muungano joseph pombe magufuliView attachment 527141
Alafu majamaa kusema hata yaipitishie lami hakuna.

They milk the cow without feeding it.
 
Tunakupongeza muheshimiwa rais wetu kwa kazi nzuri unayo fanya kuongoza nchi yetu! Mwenye Enzi Mungu azidi kukubariki na kukulinda milele yote na akuzidishie hekima na busara!
 
Back
Top Bottom