Pongezi za Lowasa kwa Rais Magufuli ni kichaka cha kujificha kutokana na kuhusika na kuuza Buzwagi

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,367
image.jpg

Wadau, amani iwe kwenu.

Nimeshangazwa sana na uamuzi wa Edward Lowasa kubadili gia angani ghafla na sasa anaonekana kuwa na mahaba na Rais Magufuli. Najua mahaba haya ni ya kinafiki na yanalenga kumsahaulisha Rais asipambane kisawasawa na wale wote waliohusika na uuzwaji wa Rasilimali zetu akiwemo Edward Lowasa.

Hoja ya kusema anamuunga mkono Rais eti kwa sababu anatekeleza Ilani ya UKAWA, huu ni unafiki uliopitiliza. Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM na hiki anachosimamia sasa alikifikiria hata kabla hajaamua kugombea Urais. Naamini kila Mtanzania anayo ile Video Clip ikionesha jinsi anavyokerwa na usafirishaji mchanga wa Dhahabu long years ago.

Nitoe wito kwa Rais Magufuli. Usirudi nyuma. Pambana na kila aliyehusika na baada ya hapo tutakuwa salama. Upo ushahidi wa wazi wa Lowasa kuhusika kwenye maskandali mengi hapa nchini. Suala la IPTL na uuzwaji wa mgodi wa Buzwagi. Ushahidi upo na hakuna mahala Lowasa ataponea. Hizi mbeleko za Lowasa kwa Rais Magufuli kwa sasa ni too late.
 
Unaweza kufafanua uhusika wake kwenye mgodi wa Buzwagi....
 
  • Thanks
Reactions: bht
View attachment 523666
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimeshangazwa sana na uamuzi wa Edward Lowasa kubadili gia angani ghafla na sasa anaonekana kuwa na mahaba na Rais Magufuli. Najua mahaba haya ni ya kinafiki na yanalenga kumsahaulisha Rais asipambane kisawasawa na wale wote waliohusika na uuzwaji wa Rasilimali zetu akiwemo Edward Lowasa.

Hoja ya kusema anamuunga mkono Rais eti kwa sababu anatekeleza Ilani ya UKAWA, huu ni unafiki uliopitiliza. Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM na hiki anachosimamia sasa alikifikiria hata kabla hajaamua kugombea Urais. Naamini kila Mtanzania anayo ile Video Clip ikionesha jinsi anavyokerwa na usafirishaji mchanga wa Dhahabu long years ago.

Nitoe wito kwa Rais Magufuli. Usirudi nyuma. Pambana na kila aliyehusika na baada ya hapo tutakuwa salama. Upo ushahidi wa wazi wa Lowasa kuhusika kwenye maskandali mengi hapa nchini. Suala la IPTL na uuzwaji wa mgodi wa Buzwagi. Ushahidi upo na hakuna mahala Lowasa ataponea. Hizi mbeleko za Lowasa kwa Rais Magufuli kwa sasa ni too late.
Fafanua siyo kuleta magazeti ya zamani tuu
 
  • Thanks
Reactions: bht
Serikali yote ya awamu ya 3 na 4 hawachomoki katika kuuza rasilimali za nchi hii. Sio Lowassa, Sumaye, Magufuri, Kikwete wala Mkapa na hata Mwinyi.

Hapa hakuna haja ya kumnyooshe mmoja kidole wakati serikali nzima ya Ccm ndio ilifanya hayo madudu ndio maana Zitto aliposema hilo wabunge wote wa Ccm wakapiga kuraya kumfukuza Bungeni.

Hakuna msafi ndani ya ccm, labda mseme hayo waliyafanya wao wenyewe kwa matakwa yao na serikali ilikua haijui ambalo ni jambo lisilowezekana.

Magufuri alipouza nyumba za serikali tuliambiwa ni maamuzi ya serikali inakuaje hawa wengine tuambiwe ni maamuzi yao wenyewe??
 
Lizaboni Acha kumchafua mzee wa Watu... Ningekuona muungwana ungekuja hapa, nakuanzaa kuombaa chenge,, na genge lake wafutiwe uwanachama wa chama Chako Alafu Ndo huanze kufuatilia babu wa Watu.....
 
Mkuu [HASHTAG]#Lizaboni[/HASHTAG] threads zako wewe nikuongela watu tu, siyo kuongelea maswala yenye tija kwa nchi?

Sipati picha kama ungekuwa hujasoma kabisa na ni baba mwnye nyumba uswazi, halafu mpangaji wako anakaanga nyama kila siku na ww unashindia maharage...!

Atakapo shitakiwa EL na Jk lazima aambatanishwe, sasa sijui unavitenganisha vipi hivyo vitu!

Hata ww sio kama unampenda JPM kulioko ungetamani Membe angekuwa pale, ila unaamini ni figisu za EL ndio zilisababisha JPM awe alipo!

Kwa nafasi yako, ongelea umoja wa kitaifa, upinzani sio uhaini au shari....bali ni kukifanya chama chetu tawala kutosinzia!

Huwezi kuibua miradi na fursa ambzao zipo zimejificha kwa wananchi wa kawaida...kama vile mikopo ya benki kwa wakulima kama trektas na pembejeo nk?
 
  • Thanks
Reactions: bht
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimeshangazwa sana na uamuzi wa Edward Lowasa kubadili gia angani ghafla na sasa anaonekana kuwa na mahaba na Rais Magufuli. Najua mahaba haya ni ya kinafiki na yanalenga kumsahaulisha Rais asipambane kisawasawa na wale wote waliohusika na uuzwaji wa Rasilimali zetu akiwemo Edward Lowasa.

Hoja ya kusema anamuunga mkono Rais eti kwa sababu anatekeleza Ilani ya UKAWA, huu ni unafiki uliopitiliza. Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM na hiki anachosimamia sasa alikifikiria hata kabla hajaamua kugombea Urais. Naamini kila Mtanzania anayo ile Video Clip ikionesha jinsi anavyokerwa na usafirishaji mchanga wa Dhahabu long years ago.

Nitoe wito kwa Rais Magufuli. Usirudi nyuma. Pambana na kila aliyehusika na baada ya hapo tutakuwa salama. Upo ushahidi wa wazi wa Lowasa kuhusika kwenye maskandali mengi hapa nchini. Suala la IPTL na uuzwaji wa mgodi wa Buzwagi. Ushahidi upo na hakuna mahala Lowasa ataponea. Hizi mbeleko za Lowasa kwa Rais Magufuli kwa sasa ni too late.
Humuamini rais?

Rais ameagiza wafuatao wahojiwe.
FB_IMG_1497359565714.jpg
 
Tena Lowasa muungwana kweli kweli, kaomba na mabadiliko ya katiba ili kuchapuza nia ya rais kwenye kuwashughulikia waliohusika kufuja rasilimali zetu na kusaidia wawekezaji kutuibia! Hii ina maana kama na yeye alihusika hatachomoka!
 
View attachment 523666
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimeshangazwa sana na uamuzi wa Edward Lowasa kubadili gia angani ghafla na sasa anaonekana kuwa na mahaba na Rais Magufuli. Najua mahaba haya ni ya kinafiki na yanalenga kumsahaulisha Rais asipambane kisawasawa na wale wote waliohusika na uuzwaji wa Rasilimali zetu akiwemo Edward Lowasa.

Hoja ya kusema anamuunga mkono Rais eti kwa sababu anatekeleza Ilani ya UKAWA, huu ni unafiki uliopitiliza. Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM na hiki anachosimamia sasa alikifikiria hata kabla hajaamua kugombea Urais. Naamini kila Mtanzania anayo ile Video Clip ikionesha jinsi anavyokerwa na usafirishaji mchanga wa Dhahabu long years ago.

Nitoe wito kwa Rais Magufuli. Usirudi nyuma. Pambana na kila aliyehusika na baada ya hapo tutakuwa salama. Upo ushahidi wa wazi wa Lowasa kuhusika kwenye maskandali mengi hapa nchini. Suala la IPTL na uuzwaji wa mgodi wa Buzwagi. Ushahidi upo na hakuna mahala Lowasa ataponea. Hizi mbeleko za Lowasa kwa Rais Magufuli kwa sasa ni too late.
Lizaboni natamani nikuone japo kwa sekunde 0.000001,
Kama uliamua kumuua Ben Saanane basi utakionja kifo ambacho kitakuwa kibaya zaidi ya mliomfanyia binadamu mwenzenu.
Walikuwepo wajeuri lakini sasa hivi ni vivutio vya utalii
 
maisha hayajawahi kuwa fair,watu hawana hofu ya Mungu we binadamu utawaambia nini? "wamejiwekea hazina duniani, maana hata wakifa watazikwa na fire extinguisher"
 
Jambo 1 nikuulize ewe kada mtiifu wa CCM,hivi wewe ni mzalendo kwa taifa lako au siyo mzalendo? baada ya jibu lako kuna jambo nitasema.
 
Mwenyekiti Wa baraza LA mawaziri huwa ni nani vile!lakini tukubali tusikubali lakini ndio hali halisi hili swala LA madini nchini kwetu hakuna hatua yyt ya kinidhamu itakayochukuliwa na uongozi wetu kwani kunavizingiti vingi hapo kwanza pawepo na kubadikisha baadhi ya sheria za nchi ndo hapo maamuzi magumu ya ndani yafanyike na Kwa maamuzi ya nje yanaweza kufanyika lakini ifanyike Kwa umakini mkubwa isije kuwa balaa Kwa taifa letu,nashukuru rais wetu kwenye swala hili amekuwa umakini sana nadhani washauri Wa kisheria wamefanya kazi nzuri,lazima tukubali migodi yetu tumeiuza Wa mapepari na wametupora vya kutosha na rais had I kufikia hapa amethubutu,tuliwacheka wasukuma enzi za ukoroni almasi kuchezea bao lakini ss hivi tumesoma tunaelimu ya kutosha lakini mambo tuliyoyafanya ni aibu tupu!
 
Lizaboni: Mnatoa wito kuwa kila mtanzania amuunge mkono Rais. Lowassa kaitikia wito wenu, nalo tena limekuwa shida. Mnataka watanzania tufanyeje?
 
sasa serikali ya CCM inasubiri nini kumshtaki Lowasa na wengine wote waliouza rasilimali za nchi??

list ni ndefu:
Lowasa
Kikwete
Mkapa
Sumaye
Chenge
Karamagi
Ngeleja
nk

Kama CCM ina nia ya dhati tunataka tuone watu wote hao wanaburuzwa kwenye ile mahakama yenu ya mafisadi ambayo kwa sasa inatumika kuwekea magunia ya mkaa.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom