BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza sana Lissu kwa kampeni zake za hali ya juu na zilizokuwa na mahudhurio makubwa sana kila kona ya Nchi yetu uliyopita. Lugha zako za upendo ulizotumia na kutugusa mamilioni ya Watanzania Wazee, vijana na hata watoto. Ulikutana na vikwazo vya aina mbali mbali lakini vyote kwa ujasiri wako mkubwa ulivuka salama.
Napenda pia kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mke wa Lissu kwa kuwa bega na bega na Mh. Lissu tangu mwanzo wa kampeni hadi mwisho wa kampeni. Hongera sana Mama na ahsante sana kwa ujasiri wako pia
Pongezi zangu pia ni kwa viongozi wote wa Chadema kwa uongozi wenu bora pamoja na matatizo mbali mbali mliyopitia tangu 2015 mengine ya kutisha sana lakini hakumkata tamaa hata kwa sekunde moja mliendelea kukipigania chama kwa uwezo wenu wote. Tunawashukuru sana 🙏🏽🙏🏽🙏🏽
Mwisho kabisa pongezi zangu ni kwa Watanzania wa kila kona ya Nchi yetu. Upendo mkubwa sana mliouonyesha kwa Chadema kusema kweli umenishangaza sana na kunipa matumaini makubwa sana kwa Nchi yetu. Pamoja na Chadema kuzuiwa kwa miaka mitano kufanya shughuli zozote za kichama lakini upendo mliouonyesha ni kama vile Chadema ilikuwa very active kwa miaka yote mitano. Mahudhurio makubwa kwenye mikutano ya kampeni Nchi nzima michango yenu mikubwa kusaidia gharama mbali mbali za wagombea wa nafasi mbali mbali Nchini ilikuwa ni ushahidi tosha kwamba Chadema iko mioyoni mwa Watanzania hivyo juhudi za kuiua Chadema kamwe hazitafanikiwa.
Sasa masaa machache yajayo tukamilishe jambo letu kwa kishindo.
Mungu ibariki Chadema, Mungu ibariki Tanzania 🙏🏽🙏🏽🙏🏽
💪🏾💪🏾💪🏾
Napenda pia kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mke wa Lissu kwa kuwa bega na bega na Mh. Lissu tangu mwanzo wa kampeni hadi mwisho wa kampeni. Hongera sana Mama na ahsante sana kwa ujasiri wako pia
Pongezi zangu pia ni kwa viongozi wote wa Chadema kwa uongozi wenu bora pamoja na matatizo mbali mbali mliyopitia tangu 2015 mengine ya kutisha sana lakini hakumkata tamaa hata kwa sekunde moja mliendelea kukipigania chama kwa uwezo wenu wote. Tunawashukuru sana 🙏🏽🙏🏽🙏🏽
Mwisho kabisa pongezi zangu ni kwa Watanzania wa kila kona ya Nchi yetu. Upendo mkubwa sana mliouonyesha kwa Chadema kusema kweli umenishangaza sana na kunipa matumaini makubwa sana kwa Nchi yetu. Pamoja na Chadema kuzuiwa kwa miaka mitano kufanya shughuli zozote za kichama lakini upendo mliouonyesha ni kama vile Chadema ilikuwa very active kwa miaka yote mitano. Mahudhurio makubwa kwenye mikutano ya kampeni Nchi nzima michango yenu mikubwa kusaidia gharama mbali mbali za wagombea wa nafasi mbali mbali Nchini ilikuwa ni ushahidi tosha kwamba Chadema iko mioyoni mwa Watanzania hivyo juhudi za kuiua Chadema kamwe hazitafanikiwa.
Sasa masaa machache yajayo tukamilishe jambo letu kwa kishindo.
Mungu ibariki Chadema, Mungu ibariki Tanzania 🙏🏽🙏🏽🙏🏽
💪🏾💪🏾💪🏾