Pongezi na hongera sana Wanakagera, nyie ni watu wastaarabu mno

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,817
11,485
Ndugu zangu wanakagera nyie ni watu wastaarabu mno, pamoja kwamba mmepatwa na majanga ya tetemeko la ardhi na serikali ikashindwa kuwasaidia bado mmeonesha kiwango cha juu kabisa cha kustaraabika nyie sio wa nchi hii kwa ustaarabu mlionesha kwa Mheshimiwa rais.

Pamoja na Mheshimiwa rais kuwasimanga baadala ya kuwapa pole lakini mliendelea kuwa wapole na kumsikiliza hadi mwisho, maneno aliyokuwa anayatamka Mhe rais hayana staha na sio maneno ambayo wafiwa wanapaswa kuwaambiwa, ikumbukwe kwamba hakuna mhanga aliyetaka kujengewa nyumba kama alivyosema Mhe watu walitaka pesa za rambirambi zitumike kuwasaidia wahanga na serikali ijenge miundombinu kwa pesa zake.

Mhe rais anasema nyie ni watu majanga tu, tetemeko, ukimwi, ugonjwa wa mnyauko bila kujua kwamba majanga haya ni asili hayakwepeki hii ni dhihaka kubwa sana kwenu pamoja na dhihaka hizo zote mlienda kumvumilia hata kumshangilia kinafiki.

Nina uhakika Mhe rais angeatamka haya kwa jamii ya watu wengine angepopolewa na mawe na uwanja ungegeuka wa damu, peleka dhihaka kama hizo Tarime uone utakachoambulia, endeleeni na ustaarabu huo Mwenyezi Mungu atawalipia.
 
Mtukufu hajawatendea haki watu wa kagera mosi ametutapeli Watanzania kwa kutuomba tuchangie wahanga wa tetemeko lakini kumbe alimaanisha tuichangie serikali kwa hiyo amewatumia wahaya kama chambo ya kutapelia.
pili badala ya kuwapa pole yeye kaenda kusema nonsense kama katelelo n.k na ingekuwa tu ni vyema kama angesema uhusiano uliopo kati ya katelelo na tetemeko huenda kuna uhusiano
Na mwisho kadanganya watanzania kuwa Italy ilishughulikia suala la tetemeko sawa na magu alivyolishughulikia .
 
Tatizo lasiku izi kila mtu anajua ila anasahau unaweza sema mengi ya muhimu ila yatakayo sambazo niyale hasi tu ivi nani anatembelea akili zetu wakizazi ichiii? Nakuwa na simanzi kila mara ninaposoma maandiko mbalimbali. Siku si zetu bali kumbuka upandalo ndo uvunalooo
 
Hahahaha.... Hili haliwezi kuwatoa kisiasa wapinzani. Limeshapita.

Mbunge wao kasema anamuunga mkono Magu
Kasema wapi wewe mtu? Mnatengeneza propaganda kisha wenyewe mnaziamini kuwa ni ukweli! Hebu tumieni akili kidogo
 
28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom