Mabibi na mabwana ni asiye na macho tu ndiye anayeweza kudhani palikuwa na uchaguzi hapa kwetu na kuwa eti matakwa ya wapiga kura yameheshimiwa.
Ndani ya nchi watu wako kimya si kuwa wote wameridhika au waliridhika na mwenendo wa uchaguzi huu. Mbaya zaidi idadi ya watu wenye manung'uniko na uchaguzi huu si kidogo wala kubeza.
Kunalalamikiwa uhalali wa uchaguzi, wizi, matumizi ya nguvu, uuwaji, utekaji, unyanyasaji, kukandamizaji, nk.
Kwamba Uganda tayari pana marehemu 37, Majeruhi 60 kati yao 48 wakiwa na majeraha ya risasi (kwa sababu ya harakati za uchaguzi huu) na kwetu haikuwa hivyo, washukuriwe sana Lissu, Maalim, na upinzani kwa ujumla kwa kitupishilia mbali na madhila kama hayo.
Kwa hakika waliotuvusha salama ni Lissu, Maalim na upinzani kwa ujumla. Hawa kama yule mama mwenye mtoto mbele ya mfalme Sulemani hawakuwa tayari kumvutania mtoto.
Lissu, Maalim na upinzani japo kwa shingo upande waliamua kuwaacha majahili kufanya yao kwa kila mtu kuwabaini. Kwa hakika walikuwa na wanao uwezo wa kukinukisha vilivyo. Lakini jamani maisha ya watu hayana thamani kiasi hicho?
Polisi Uganda na watawala Uganda kama ilivyo kwetu, wako tayari kumvutania mtoto eti kuonyesha kuwa mtoto ni wao.
Kwa kiu ya madaraka yao iliyopitiliza wako tayari hata kuuwa watu. Pathetic!
Kwamba hayakutokea maafa zaidi, busara za viongozi wetu hawa na zishukuriwe sana. Linganisha na upande wa pili njaa yao ya madaraka ni kubwa kupitiliza hata kama ni kwa kuuwa watu, wako tayari! Jambo la aibu sana.
Kama ilivyo Uganda sisi pia tumekuwa wa kunyooshewa vidole na wote wapenda haki wakiwamo jumuiya za kimataifa kuwa mamlaka zetu ni mijizi, miuaji, isiyojali haki za binadamu, isiyoheshimu uhuru wa watu wake nk, nk.
Nakazia, washukuriwe sana Lissu na Maalim Seif kwani bila ya busara na ustahamilivu wao usio kipimo katika mazingira magumu, baadhi yetu tu hai hata leo.
Ndani ya nchi watu wako kimya si kuwa wote wameridhika au waliridhika na mwenendo wa uchaguzi huu. Mbaya zaidi idadi ya watu wenye manung'uniko na uchaguzi huu si kidogo wala kubeza.
Kunalalamikiwa uhalali wa uchaguzi, wizi, matumizi ya nguvu, uuwaji, utekaji, unyanyasaji, kukandamizaji, nk.
Kwamba Uganda tayari pana marehemu 37, Majeruhi 60 kati yao 48 wakiwa na majeraha ya risasi (kwa sababu ya harakati za uchaguzi huu) na kwetu haikuwa hivyo, washukuriwe sana Lissu, Maalim, na upinzani kwa ujumla kwa kitupishilia mbali na madhila kama hayo.
Kwa hakika waliotuvusha salama ni Lissu, Maalim na upinzani kwa ujumla. Hawa kama yule mama mwenye mtoto mbele ya mfalme Sulemani hawakuwa tayari kumvutania mtoto.
Lissu, Maalim na upinzani japo kwa shingo upande waliamua kuwaacha majahili kufanya yao kwa kila mtu kuwabaini. Kwa hakika walikuwa na wanao uwezo wa kukinukisha vilivyo. Lakini jamani maisha ya watu hayana thamani kiasi hicho?
Polisi Uganda na watawala Uganda kama ilivyo kwetu, wako tayari kumvutania mtoto eti kuonyesha kuwa mtoto ni wao.
Kwa kiu ya madaraka yao iliyopitiliza wako tayari hata kuuwa watu. Pathetic!
Kwamba hayakutokea maafa zaidi, busara za viongozi wetu hawa na zishukuriwe sana. Linganisha na upande wa pili njaa yao ya madaraka ni kubwa kupitiliza hata kama ni kwa kuuwa watu, wako tayari! Jambo la aibu sana.
Kama ilivyo Uganda sisi pia tumekuwa wa kunyooshewa vidole na wote wapenda haki wakiwamo jumuiya za kimataifa kuwa mamlaka zetu ni mijizi, miuaji, isiyojali haki za binadamu, isiyoheshimu uhuru wa watu wake nk, nk.
Nakazia, washukuriwe sana Lissu na Maalim Seif kwani bila ya busara na ustahamilivu wao usio kipimo katika mazingira magumu, baadhi yetu tu hai hata leo.