Pongezi kwa Wizara ya Elimu si wanafunzi pekee Bali hata walimu pia waliteseka

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,893
14,347
Wakuu habari za wakati huu,

Napenda kutumia fursa hii kumpongeza Waziri wa elimu Profesa J.Ndalichako pamoja na Wizara ya Elimu kwa ujumla kwa kutoa waraka unao husu ufundishaji na ujifunzaji.

Naomba nikiri kuwa huu waraka umefika kwa wakati muafaka kwani ukiiusoma utabaini kuwa wakuu wa mikoa na maafisa elimu walitumia mamlaka yao kudhulumu haki za wanafunzi na walimu kwa kigezo cha kuinua ufaulu huku wakiwalazimisha walimu na wanafunzi kubaki kusoma wakati wa likizo na pia masomo kwa darasa la mitihani ililazimishwa kuanza saa kumi na mbili na nusu eti lengo kuu ni kuinua ufaulu wa wanafunzi.


Hivyo kwa waraka huu wa elimu kwa mwaka 2020 wizara ya elimu imepiga marufuku upuuzi huo, maana wahanga wakubwa walikuwa ni wanafunzi na walimu wa chini na ilifikia hatua walimu walinyumwa likizo kwa kigezo cha kufundisha wakati wa likizo,Mimi mwenyewe ni mhanga wa hili, niliwahi kugombana na bwana Godfrey Zambi mkuu wa mkoa wa Lindi juu ya ukiritimba huu alipotembelea shuleni kwangu mwaka 2017 na kuzuia walimu kwenda likizo ili wafundishe

Ukisikia serikali ya wanyonge basi tambua kuwa ni ile ile serikali ya awamu ya tano,

Soma waraka hapa>>>>>>View attachment WARAKA WA ELIMU 2020.pdf

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walaka una mazuri na mabaya yake

Suala la wanafunzi wa madarasa ya mtihani kukaa kambi wizara ingeangalia uboreshaji wa hizo kambi siyo kuzifuta kabisa kwani kambi zimekuwa zikisaidia asilimia 90 watahiniwa hususani wale ambao wakifika nyumbani wanakosa mda wa kujisomea yani mtoto akifika nyumbani tu basi ndio mama wa familia au baba majukumu yote anachiwa anakosa mda wa kujisomea

Asilimia 90 ya shule za kataa zinazofanya vizuri kwenye mitihani yao ya utimilifu kambi imekuwa ikiwasaidia watoto hususani wale waishio mazingira magumu mazingira ambayo ni mbali na shule, mazingira ambayo upatikanaji wa chakula nyumbani ni tatizo, mazingira ambayo si rafiki kwa kujisomea mfano ukosefu wa mwanga (taa) kwaiyo walipokusanyika kambi iliwezesha hawa wahitimu kutatua changamoto zao

Waraka upitiwe upya una mazuri na mabaya
 
Walaka una mazuri na mabaya yake

Suala la wanafunzi wa madarasa ya mtihani kukaa kambi wizara ingeangalia uboreshaji wa hizo kambi siyo kuzifuta kabisa kwani kambi zimekuwa zikisaidia asilimia 90 watahiniwa hususani wale ambao wakifika nyumbani wanakosa mda wa kujisomea yani mtoto akifika nyumbani tu basi ndio mama wa familia au baba majukumu yote anachiwa anakosa mda wa kujisomea

Asilimia 90 ya shule za kataa zinazofanya vizuri kwenye mitihani yao ya utimilifu kambi imekuwa ikiwasaidia watoto hususani wale waishio mazingira magumu mazingira ambayo ni mbali na shule, mazingira ambayo upatikanaji wa chakula nyumbani ni tatizo, mazingira ambayo si rafiki kwa kujisomea mfano ukosefu wa mwanga (taa) kwaiyo walipokusanyika kambi iliwezesha hawa wahitimu kutatua changamoto zao

Waraka upitiwe upya una mazuri na mabaya
Waraka haufunguki...msaada!!!!
 
Subiri baada ya wiki tu utasikia wakuu wa mikoa wavunja maagizo ya huo waraka. Wanavunja sheria za Bunge,Mahakama na Katiba sembuse ka waraka ka waalimu? Huu ni utawala wa kuvunja taratibu na sheria. Subiri uone. Mark my words.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
BASHITE ataanza kuuvunja WARAKA huu Dar. Then Nyumbu zote zitafuata.
Wait to see the unbecoming COME!
 
Huu waraka bado upo hai au kuna waraka mwingine umeshaufuta? Naomba nijulishwe jamani kwa mwenye taarifa.
 
Jamani mwenye taarifa naomba anijulishe huu waraka bado unafanya kazi au vinginevyo kwani kuna baadhi ya shule bado zimezuia wanafunzi wasianze likizo . Kama huu waraka bado upo hai basi nafikiri ni wakati muafaka sasa wa wizara ya elimu kuiongezea mapato serikali kwa kuzipiga faini baadhi ya shule ambazo bado zimekaidi na zinazuia wanafunzi wasiende likizo inayoanza kesho.
 
Back
Top Bottom