MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Na Mwl Udadis, Mtwara
Makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na kampuni za Equinor & Shell yamekamilika kwaajili ya uwekezaji katika mradi wa gesi asilia, mradi wenye thamani ya Dola Bilioni 42 (Fedha hii ni zaidi ya Bajeti ya mataifa ya Rwanda & Burundi kwa miaka 5).Kampuni za Tanzania zaidi ya 1760 zimesajiliwa kwaajili ya kutoa huduma katika ujenzi wa mradi huo unaokwenda kubadili taswira ya nchi yetu kiuchumi.
Kihistoria uwingi wa rasilimali haujawahi kutiliwa shaka ndani ya Afrika lakini uwezo wa kugeuza rasilimali hizo kuwa neema imekuwa swali gumu. Kwa mara nyingine ripoti mbalimbali za kimataifa zinaonyesha Tanzania inakwenda kujitoa katika nadharia hii kupitia uongozi wa Rais Samia Suluhu unaofanya mageuzi makubwa ktk kuvutia uwekezaji nchini.
Si katika mradi huu pekee, tuliona kwa mara ya kwanza katika historia katika kipindi cha miezi 24 pekee (March 2022 - Feb 2023), Rais Samia alifanikisha usajili wa miradi ya uwekezaji yenye thamani zaidi ya Trilioni 7 (32% ikiwa ni kutoka kwa wazawa, 41% wawekezaji wa nje & 27% ikiwa ni ushirikiano (Joint venture)). Mapinduzi haya ni pumzi ya uhai katika uchumi wa nchi yoyote Duniani.
Rais Samia anafanya mambo magumu yaonekane rahisi ndio maana kila unapojaribu kupitia ripoti mbalimbali mfano katika kilimo, utakutana na mikakati mingi ya kuhakikisha wakulima wanapata ruzuku ya kutosha na masoko ya uhakika na kipekee program kama BBT zinazolenga kuwainua vijana kiuchumi, mambo haya kwa muda mrefu yalionekana kama nadharia tu.
Kila sekta inaguswa kipekee, iwe huduma za kijamii, maslahi ya watumishi wa umma, demokrasia na utawala bora, diplomasia ya uchumi na hata mikakati ya muda mrefu. Mfano mdogo hivi karibuni Club ya Seattle Sounders FC, Seattle Seahawks (NFL), na Portland Trailblazers (NBA) zote zitaanza kuutangaza utalii wa Tanzania ambapo faida ni nyingi mno kwa Tanzania.
Watanzania tuzidi kumuunga mkono Rais Samia kwa mambo mazuri anayoyafanya, uzalendo na uchapakazi wake si wa kiwango cha kawaida.
Makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na kampuni za Equinor & Shell yamekamilika kwaajili ya uwekezaji katika mradi wa gesi asilia, mradi wenye thamani ya Dola Bilioni 42 (Fedha hii ni zaidi ya Bajeti ya mataifa ya Rwanda & Burundi kwa miaka 5).Kampuni za Tanzania zaidi ya 1760 zimesajiliwa kwaajili ya kutoa huduma katika ujenzi wa mradi huo unaokwenda kubadili taswira ya nchi yetu kiuchumi.
Kihistoria uwingi wa rasilimali haujawahi kutiliwa shaka ndani ya Afrika lakini uwezo wa kugeuza rasilimali hizo kuwa neema imekuwa swali gumu. Kwa mara nyingine ripoti mbalimbali za kimataifa zinaonyesha Tanzania inakwenda kujitoa katika nadharia hii kupitia uongozi wa Rais Samia Suluhu unaofanya mageuzi makubwa ktk kuvutia uwekezaji nchini.
Si katika mradi huu pekee, tuliona kwa mara ya kwanza katika historia katika kipindi cha miezi 24 pekee (March 2022 - Feb 2023), Rais Samia alifanikisha usajili wa miradi ya uwekezaji yenye thamani zaidi ya Trilioni 7 (32% ikiwa ni kutoka kwa wazawa, 41% wawekezaji wa nje & 27% ikiwa ni ushirikiano (Joint venture)). Mapinduzi haya ni pumzi ya uhai katika uchumi wa nchi yoyote Duniani.
Rais Samia anafanya mambo magumu yaonekane rahisi ndio maana kila unapojaribu kupitia ripoti mbalimbali mfano katika kilimo, utakutana na mikakati mingi ya kuhakikisha wakulima wanapata ruzuku ya kutosha na masoko ya uhakika na kipekee program kama BBT zinazolenga kuwainua vijana kiuchumi, mambo haya kwa muda mrefu yalionekana kama nadharia tu.
Kila sekta inaguswa kipekee, iwe huduma za kijamii, maslahi ya watumishi wa umma, demokrasia na utawala bora, diplomasia ya uchumi na hata mikakati ya muda mrefu. Mfano mdogo hivi karibuni Club ya Seattle Sounders FC, Seattle Seahawks (NFL), na Portland Trailblazers (NBA) zote zitaanza kuutangaza utalii wa Tanzania ambapo faida ni nyingi mno kwa Tanzania.
Watanzania tuzidi kumuunga mkono Rais Samia kwa mambo mazuri anayoyafanya, uzalendo na uchapakazi wake si wa kiwango cha kawaida.