Kijana huyu wa kizanzibar amestahili kuaminiwa tena na Ndugu Mwenyekiti wa CCM Taifa na UVCCM Taifa kushika wadhifa wa katibu mkuu UVCCM Taifa katika kipindi cha 2017-2022.
Awali alikuwa naibu katibu mkuu wa UVCCM Zanzibar ambapo alifanya kazi nzuri sana na kupandishwa kuwa kaimu katibu mkuu UVCCM Taifa ambapo alifanya kazi nzuri na yenye heshima kwa kufanya ziara nyingi za kukagua uhai wa jumuiya, kusimamia nidhamu ya utendaji, kuhakikisha hoja na propaganda za wapinzani zinajibiwa kwa wakati na uzito unaostahili.
Katika kipindi chake akikaimu nafasi hiyo Ndugu Shaka alitekeleza kwa vitendo majukumu ya kumuunga mkono, kumlinda, kumtetea na kumpigania Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli na Chama Cha Mapinduzi.
Ni ukweli uliowazi ni katika kipindi chake UVCCM ilionekana kwani aliwaibua pia vijana wengi na kuwapa nafasi ya kuitumikia jumuiya.
Namtakia kila la kheri katika kipindi hiki kwani vijana tunaimani naye pamoja na mwenyekiti wetu wa UVCCM Taifa na muunganiko wao tunategemea mambo makubwa.
Awali alikuwa naibu katibu mkuu wa UVCCM Zanzibar ambapo alifanya kazi nzuri sana na kupandishwa kuwa kaimu katibu mkuu UVCCM Taifa ambapo alifanya kazi nzuri na yenye heshima kwa kufanya ziara nyingi za kukagua uhai wa jumuiya, kusimamia nidhamu ya utendaji, kuhakikisha hoja na propaganda za wapinzani zinajibiwa kwa wakati na uzito unaostahili.
Katika kipindi chake akikaimu nafasi hiyo Ndugu Shaka alitekeleza kwa vitendo majukumu ya kumuunga mkono, kumlinda, kumtetea na kumpigania Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli na Chama Cha Mapinduzi.
Ni ukweli uliowazi ni katika kipindi chake UVCCM ilionekana kwani aliwaibua pia vijana wengi na kuwapa nafasi ya kuitumikia jumuiya.
Namtakia kila la kheri katika kipindi hiki kwani vijana tunaimani naye pamoja na mwenyekiti wetu wa UVCCM Taifa na muunganiko wao tunategemea mambo makubwa.