Pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa kuwahi kwenye matukio

Mtego wa Noti

JF-Expert Member
Nov 27, 2010
2,591
1,599
Napenda kutoa pongezi za dhati kwa jeshi la polisi Mkoa maalumu wa Kinondoni chini ya RPC Kingai kwa kuwa na utendaji wa haraka wa kufika kwenye matukio mara wanapopokea taarifa za uhalifu hata ikiwa usiku wa manane.

Mimi ni shuhuda maana majambazi waliingia mtaani na mara baada ya Polisi kupewa taarifa walifika haraka sana eneo la tukio tena magari mawili kutokea maeneo tofauti lakini wakielekea kwenye kupambana. Hii ni tofauti na ilivyotegemewa hasa siku za nyuma. Majambazi walihisi wako hatarini wakaondoka vinginevyo pangetifuka maana makamanda walifika wengi wakiwa wamejipanga kimapigano.

Na kwa muda wote mara baada ya taarifa kufika Polisi RPC Kingai mwenyewe alikuwa anaratibu vikosi mbalimbali kutokea Wazo, Goba na Madale kuvielekeza vifike eneo la tukio huku akiwapigia simu wahanga ili waelekeze vikosi vifike eneo la tukio.

Hongereni sana makamanda na sisi wakazi wa Goba tumefurahi mno na kujivunia uwepo na utendaji wenu wa haraka sana kwa kufika kwenye matukio. Endeleeni na spirit hiyo.
 
Napenda kutoa pongezi za dhati kwa jeshi la polisi Mkoa maalumu wa Kinondoni chini ya RPC Kingai kwa kuwa na utendaji wa haraka wa kufika kwenye matukio mara wanapopokea taarifa za uhalifu hata ikiwa usiku wa manane...

Namshukuru Mungu nimelelewa kuamini kwamba kumtukana mtu ni dhambi, pia nimejifunza kuheshimu mawazo na maoni ya wengine.

Umenisikitisha kuandika kitu ambacho ni tofauti kabisa na uhalisia.

Mwezi uliopita tukio limeripotiwa kituo cha Madale askari aliyekua zamu akasema yuko peke yake, kwenda Wazo ndio kabisaa.

Lakini mbaya zaidi kwa mhanga aliyeibiwa vifaa ukinitajia mambo ya polisi ni kama kutonesha kidonda.

Unaweza kutoa mfano wa tukio liliotokea wakafika kwa wakati na kufanya kazi yao? Acha hii kuandika kwa ujumla jumla.
 
Namshukuru Mungu nimelelewa kuamini kwamba kumtukana mtu ni dhambi, pia nimejifunza kuheshimu mawazo na maoni ya wengine...
Pole sana mkuu. Mimi nimejaribu kutoa ushuhuda wa kilichotokea na nilichoona kwa macho yangu. Inawezekana bado jeshi lina changamoto za hapa na pale lakini kuna muda wanafanya vizuri kama tukio la jana
 
Pole sana mkuu. Mimi nimejaribu kutoa ushuhuda wa kilichotokea na nilichoona kwa macho yangu. Inawezekana bado jeshi lina changamoto za hapa na pale lakini kuna muda wanafanya vizuri kama tukio la jana

Jana tukio lilitokea eneo gani mkuu? Na lilihusisha kitu gani?

Hawa jamaa washawahi kutuletea wakamataji wa Ulimboka unakumbuka?

Isijekua ni harakati zao zilezile za maigizo.
 
Namshukuru Mungu nimelelewa kuamini kwamba kumtukana mtu ni dhambi, pia nimejifunza kuheshimu mawazo na maoni ya wengine.

Umenisikitisha kuandika kitu ambacho ni tofauti kabisa na uhalisia.

Mwezi uliopita tukio limeripotiwa kituo cha Madale askari aliyekua zamu akasema yuko peke yake, kwenda Wazo ndio kabisaa.

Lakini mbaya zaidi kwa mhanga aliyeibiwa vifaa ukinitajia mambo ya polisi ni kama kutonesha kidonda.

Unaweza kutoa mfano wa tukio liliotokea wakafika kwa wakati na kufanya kazi yao? Acha hii kuandika kwa ujumla jumla.
Hahahahaha daaa we jamaa umenichekesha sana ina maana ingekuwa kutukana sio dhambi leo mtoa mada angepokea sana matusi au sio
 
Hahahahaha daaa we jamaa umenichekesha sana ina maana ingekuwa kutukana sio dhambi leo mtoa mada angepokea sana matusi au sio

Mungu anisamehe tu, kwanza nahisi kama kimoyomoyo nimerusha kirejareja
 
Napenda kutoa pongezi za dhati kwa jeshi la polisi Mkoa maalumu wa Kinondoni chini ya RPC Kingai kwa kuwa na utendaji wa haraka wa kufika kwenye matukio mara wanapopokea taarifa za uhalifu hata ikiwa usiku wa manane.

Mimi ni shuhuda maana majambazi waliingia mtaani na mara baada ya Polisi kupewa taarifa walifika haraka sana eneo la tukio tena magari mawili kutokea maeneo tofauti lakini wakielekea kwenye kupambana. Hii ni tofauti na ilivyotegemewa hasa siku za nyuma. Majambazi walihisi wako hatarini wakaondoka vinginevyo pangetifuka maana makamanda walifika wengi wakiwa wamejipanga kimapigano.

Na kwa muda wote mara baada ya taarifa kufika Polisi RPC Kingai mwenyewe alikuwa anaratibu vikosi mbalimbali kutokea Wazo, Goba na Madale kuvielekeza vifike eneo la tukio huku akiwapigia simu wahanga ili waelekeze vikosi vifike eneo la tukio.

Hongereni sana makamanda na sisi wakazi wa Goba tumefurahi mno na kujivunia uwepo na utendaji wenu wa haraka sana kwa kufika kwenye matukio. Endeleeni na spirit hiyo.
Polis wanafanya KAZI nzuri sana

Ussrt
 
Back
Top Bottom