nkiniangelikal
Member
- Feb 28, 2020
- 12
- 4
Napenda kumpongeza Waziri Simbachawene kwa kuwazuia jeshi la polisi na utaratibu wao mbovu wa kuwaweka ndani wananchi hata yule asiyekuwa na kosa.
Kwa mfano haswa kwa madereva wa magari ndio wamekuwa wahanga wakubwa kwa kuwekwa ndani au mahabusu hasa pale unapopata ajali hata kama huyo dereva hiyo ajali hakuisababisha yeye utaambiwa mwekeni ndani ukiuliza kwanini watakuambia unawekwa ndani kwa usalama wako.
Ukishawekwa ndani hadi siku tatu mpaka utoe rushwa ndio wakuachie ukishatoka watakuambia wewe huna kosa nenda zako mwenye kosa ni marehemu naomba Mh Waziri uliangalie na hili.
Kwa mfano haswa kwa madereva wa magari ndio wamekuwa wahanga wakubwa kwa kuwekwa ndani au mahabusu hasa pale unapopata ajali hata kama huyo dereva hiyo ajali hakuisababisha yeye utaambiwa mwekeni ndani ukiuliza kwanini watakuambia unawekwa ndani kwa usalama wako.
Ukishawekwa ndani hadi siku tatu mpaka utoe rushwa ndio wakuachie ukishatoka watakuambia wewe huna kosa nenda zako mwenye kosa ni marehemu naomba Mh Waziri uliangalie na hili.