Bikis
Member
- Feb 23, 2019
- 52
- 74
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi, Sergei Lavrov amemwambia waziri mwenzake wa Marekani Mike Pompeo, "wakati umewadia kwa Moscow na Washington kuweka kando miaka kadhaa ya uhasama na kubuni njia ya kushirikiana".
Mike Pompeo yuko ziarani katika mji unaopakana na bahari nyeusi wa Sochi kwa mazungumzo pamoja na waziri mwenzake wa Urusi na baadae amepangiwa pia kukutana na rais Vladimir Putin.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umeingia sumu kutokana na madai-yaliyokanushwa na Moscow-kwamba Urusi imejaribu kushawishi matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2016, na pia kutokana na tofauti zao za maoni katika mzozo wa Venezuela, Iran, Syria na Ukraine.
"Tunaona kuna shaka na chuki" amesema Lavrov mwanzoni mwa mazungumzo yake pamoja na Pompeo."Hali hii inakorofisha usalama wa nchi yetu na nchi yenu pia na kusababisha wasi wasi ulimwenguni.Tunahisi wakati umewadia wa kubuni uhusiano mpya wenye manaufaa wa zaidi kwa pande zote" amesisitiza waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi Lavrov na kuongeza tunanukuu"Tuko tayari ikiwa wenzetu wa Marekani wako tayari pia."
Ziara ya Mike Pompeo ni hatua ya mwanzo ya mazungumzo ya ngazi ya juu kati ya Moscow na Washington tangu mwendesha mashitaka mkuu wa Marekani Robert Muller alipowasilisha ripoti yake iliyotathmini nafasi iliyoshikiliwa na Urusi katika uchaguzi wa rais mwaka 2016 nchini Marekani.
Mike Pompeo yuko ziarani katika mji unaopakana na bahari nyeusi wa Sochi kwa mazungumzo pamoja na waziri mwenzake wa Urusi na baadae amepangiwa pia kukutana na rais Vladimir Putin.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umeingia sumu kutokana na madai-yaliyokanushwa na Moscow-kwamba Urusi imejaribu kushawishi matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2016, na pia kutokana na tofauti zao za maoni katika mzozo wa Venezuela, Iran, Syria na Ukraine.
"Tunaona kuna shaka na chuki" amesema Lavrov mwanzoni mwa mazungumzo yake pamoja na Pompeo."Hali hii inakorofisha usalama wa nchi yetu na nchi yenu pia na kusababisha wasi wasi ulimwenguni.Tunahisi wakati umewadia wa kubuni uhusiano mpya wenye manaufaa wa zaidi kwa pande zote" amesisitiza waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi Lavrov na kuongeza tunanukuu"Tuko tayari ikiwa wenzetu wa Marekani wako tayari pia."
Ziara ya Mike Pompeo ni hatua ya mwanzo ya mazungumzo ya ngazi ya juu kati ya Moscow na Washington tangu mwendesha mashitaka mkuu wa Marekani Robert Muller alipowasilisha ripoti yake iliyotathmini nafasi iliyoshikiliwa na Urusi katika uchaguzi wa rais mwaka 2016 nchini Marekani.