Political bubbles ‘Mapovu ya kisiasa’

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1573299901171.png
Kila kitu duniani kina kanuni na misingi yake. Kwa mfano, unapoweka kinywaji chenye gesi kwenye glasi, kanuni yake ni kuweka taratibu, vinginevyo glasi itajaa mapofu badala ya kinywaji na muda mfupi baadae mapovu yatatoweka yenyewe na glasi inabaki tupu.

Demokrasia ina kanuni na misingi yake. Kama tumeamua kuifuata, ni vyema tuifuate katika hatua, misingi na kanuni zake. Kama tukiamua kukwepa kanuni na misingi ya demokrasia tukakimbilia matokeo (ya demokrasia?); hatutapata matokeo ya kuridhisha na kinyume chake yatotokea mapovu ya kisiasa.

Tutakuwa na hatari ya kujikuta siku moja tuna viongozi wa kisiasa wasiokuwa na muunganiko wa kisiasa ‘Political legitimacy’ na wanaowaongoza. Matokeo yake sio tu kwamba ushirikiano kati ya waongozaji na waongozwaji hautakuwepo bali pia muongozaji atapoteza morali au kujikuta kwenye confusion kubwa. Katika hatua ya juu kabisa, waongozwaji na waongozaji wote watapoteza kisha jaribu kufikiria nini kitafuata?

Tunachoweza kushauri ni kwamba; kama tumeamua kufuata mfumo wa demokrasia, ni muhimu tuufuate pamoja na kanuni na misingi yake na kama tunaona demokrasia haifai tena kwa sababu zozote zile; ni muhimu wadau wakubaliane rasmi kuachana nayo na kutangaza mfumo mpya ambao utaonekana kama mbadala wa demokrasia.

Hata hivyo kabla ya kufikiria uamuzi wa pili hapo juu, ni muhimu kukumbuka kuwa hadi sasa bado hakuna mfumo mbadala wa kisiasa unaoaminika kuwa bora zaidi ya demokrasia duniani.
 
Kudai kuwa sisi ni wanademokrasia, tuliopo kwenye nchi ya kidemokrasia na demokrasia ndio mfumo bora na wakati huo huo hatuko tayari kufuata misingi ya hiyo demokrasia yenyewe; ni sawa na kudai sisi ni matajiri lakini fedha zetu ziko kwenye akaunti flani huko Moscow nchini Urusi.
 
Kudai kuwa sisi ni wanademokrasia, tuliopo kwenye nchi ya kidemokrasia na demokrasia ndio mfumo bora na wakati huo huo hatuko tayari kufuata misingi ya hiyo demokrasia yenyewe; ni sawa na kudai sisi ni matajiri lakini fedha zetu ziko kwenye akaunti flani huko Moscow nchini Urusi.
Hayo yote yanasababishwa na maccm.
 
Kwa hiyo unamfananisha sawa na Dr.Shika?
Kudai kuwa sisi ni wanademokrasia, tuliopo kwenye nchi ya kidemokrasia na demokrasia ndio mfumo bora na wakati huo huo hatuko tayari kufuata misingi ya hiyo demokrasia yenyewe; ni sawa na kudai sisi ni matajiri lakini fedha zetu ziko kwenye akaunti flani huko Moscow nchini Urusi.
 
Ikumbukwe, toka zamani nguvu kuu za viongozi wa kisiasa kote duniani, msingi wake mkuu ni uungwaji mkono na msingi mkuu wa uungwaji mkono ni kujenga ushawishi. Katika zama hizi, umuhimu wa kujenga ushawishi na kutafuta uungwaji mkono unazidi kuwa muhimu kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya ulimwengu kutokana na kukuwa kwa mifumo ya mawasiliano.

Ni jambo la hatari kwa viongozi wowote wa kisiasa katika zama hizi kufikiria kuwa wanaweza kufanya vizuri bila kuungwa mkono au kufikiria kuungwa mkono bila kujenga ushawishi au kufikiria kujenga ushawishi kwa lazima. Jambo tunalopaswa kukaa chini na kutafakari ni kwamba, ni kwa vipi tunaweza kuepuka kanuni hii muhimu bila kukumbwa na 'political bubbles'?
 
Ikumbukwe, toka zamani nguvu kuu za viongozi wa kisiasa kote duniani, msingi wake mkuu ni uungwaji mkono na msingi mkuu wa uungwaji mkono ni kujenga ushawishi. Katika zama hizi, umuhimu wa kujenga ushawishi na kutafuta uungwaji mkono unazidi kuwa muhimu kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya ulimwengu kutokana na kukuwa kwa mifumo ya mawasiliano.

Ni jambo la hatari kwa viongozi wowote wa kisiasa katika zama hizi kufikiria kuwa wanaweza kufanya vizuri bila kuungwa mkono au kufikiria kuungwa mkono bila kujenga ushawishi au kufikiria kujenga ushawishi kwa lazima. Jambo linalopaswa kukaa chini na kutafakari ni kwamba, ni kwa vipi tunaweza kuepuka kanuni hii muhimu bila kukumbwa na 'political bubbles'?
magufulu anatembea huku anagawa mabulungutu akidhani ndo anashawishi kuungwa mkono katika nchi yenye population ya 50mil+
 
Kama dokta Shika tu.
Kudai kuwa sisi ni wanademokrasia, tuliopo kwenye nchi ya kidemokrasia na demokrasia ndio mfumo bora na wakati huo huo hatuko tayari kufuata misingi ya hiyo demokrasia yenyewe; ni sawa na kudai sisi ni matajiri lakini fedha zetu ziko kwenye akaunti flani huko Moscow nchini Urusi.
 
Kudai kuwa sisi ni wanademokrasia, tuliopo kwenye nchi ya kidemokrasia na demokrasia ndio mfumo bora na wakati huo huo hatuko tayari kufuata misingi ya hiyo demokrasia yenyewe; ni sawa na kudai sisi ni matajiri lakini fedha zetu ziko kwenye akaunti flani huko Moscow nchini Urusi.
Ya Dr. Shika hayo.
 
Pia tukumbuke kwamba kila mbegu ipandwayo, katika stage flani itaota, kwa hiyo tahadhari ni muhimu sana. Ni katika kukumbushana tu
 
Back
Top Bottom