Polisi Zanzibar: Sheikh Farid wa Uamsho hakutekwa; kufikishwa mahakamani

Yani kanzu Nyeupeee haina hata mkunjo, kuonyesha alikwidwa kuonyesha alileta upinzani,,,nehi!!

Du!! usanii mwingine unahitaji shule hata ya std 7 kidogo, sio chuo tu.
 
Serikali hiyo hiyo imekataa kama ilimteka dr,Ulimboka....Hawana mpya.

wakamteka muda wote na kumwachia mrembo vile?! hujaona ulimboka alivyofanywa in only 8hrs? huyo anatafuta umaarufu, unafikiri jeshi lingembembeleza siku zote 3 vile, aa wapi, anatafuta kujulikana.
 
me naona hapa ni kama unawapigia story viziwi, kila anaefuatilia mambo anajua kuwa shekhe alikuwa msanii, hajatekwa bali anataka kuwaaminisha watanzania kuwa serekali yao sio nzuri, mimi siungi mkono hilo swala. serekali ya chama cha mapinduzi ipo thabiti, haitetereki na haiyumbishwi na wahuni.
 
technic ya shehe ya kitoto sana......

Hivi anajua kutekwa?

Hebu akamuulize ulimboka

halafu hata hakumpanga dereva wake story zikafanana

Hana shule huyu elimu ya kukunja miguu pekee haiwezi mpeleka mbali .Kajaribu sasa yamemkuta haswa .Faridi anatakiwa kuunganishwa na kesi ya mauaji na si zaidi ya hapo .Kuna mali za watu zimeharibika nk watu wameathirika kwa ujinga wake detention with no mentioning is where he deserve to be .
 
ulimboka22.jpg
DK.+ULIMBOKA.jpg
0000000000000001adkuli.jpg

Weka na za shekhe uamsho before na after kutekwa tuone mwili na ndevu zake kama zina badiliko lolote japo kiduchu

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
wakamteka muda wote na kumwachia mrembo vile?! Hujaona ulimboka alivyofanywa in only 8hrs? Huyo anatafuta umaarufu, unafikiri jeshi lingembembeleza siku zote 3 vile, aa wapi, anatafuta kujulikana.

sauli je, serikali ilikubali kama ilimteka dr,ulimboka? Pamoja na majaraha yote aliyokuwanayo dr,ulimboka... Kwanini serikali mpaka leo haijakubali kama ilihusika ?
 
Weka na za shekhe uamsho before na after kutekwa tuone mwili na ndevu zake kama zina badiliko lolote japo kiduchu

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

kwanini serikali imekanusha kumteka dr, Ulimboka? SASA KWANINI TUWE WEPESI KUKUBALI KAULI YA SERIKALI?
 
kwanini serikali imekanusha kumteka dr, Ulimboka? SASA KWANINI TUWE WEPESI KUKUBALI KAULI YA SERIKALI?
mkuu dizaini kama sikuelewielewi, yaani unataka kuonesha kwamba akili yako haijui nini cha kuamini nini sio au kwamba huwezi kupima pumba na mchele?
 
Sheikh Farid sio mara ya kwanza kutekwa, na kila aliyetekwa si lazima ang'olewe kucha...inategemea na mazingira...Chuki yako dhidi ya Sheikh Farid ndio inayokufanya uamini hivyo.

KWELI wewe umekula unga wa ndele, nyeusi inakuwa nyeupe na nyeupe inaitwa nyeusi. Kila anayeongea kwa mtazamo tofauti na wewe unasema anaCHUKI. Kweli "Kivuli Kinaishi" ni tamthiliya iliyosadifu akili za watu wa huko.
 
mkuu dizaini kama sikuelewielewi, yaani unataka kuonesha kwamba akili yako haijui nini cha kuamini nini sio au kwamba huwezi kupima pumba na mchele?

ulitaka huyo shehe aeleze kila kitu ??? AMWAGE MTAMA MBELE YA VIFALANGA ??? hiyo kesi ataijibu vipi??? huyo shehe alishapigwa huko nyuma na ndio mara hii wakaona wajifanye wastaalabu.

Hivi ulimboka alifunguliwa mashitaka??? yamemaliza vipi ???
 
Sheikh Farid sio mara ya kwanza kutekwa, na kila aliyetekwa si lazima ang'olewe kucha...inategemea na mazingira...Chuki yako dhidi ya Sheikh Farid ndio inayokufanya uamini hivyo.
kwa kweli me mwenyewe n muislam lakin kwa hili naona haya siwez kuwa miongon mwa wanafiki watu wameharbiwa mali zao,amani imetoka sababu ya huyu Farid wakat Mtume wetu mtukufu wa daraja amedharirishwa na Dhalimu yule lakin hakuna Muislam TZ aliyefanya fujo hapo ndpo nnapogundua kuwa huu si Uislam ni siasa za CUf na CCm siwez kumuunga mkono Farid kwa hili hapana siwezi
 
kwa kweli me mwenyewe n muislam lakin kwa hili naona haya siwez kuwa miongon mwa wanafiki watu wameharbiwa mali zao,amani imetoka sababu ya huyu Farid wakat Mtume wetu mtukufu wa daraja amedharirishwa na Dhalimu yule lakin hakuna Muislam TZ aliyefanya fujo hapo ndpo nnapogundua kuwa huu si Uislam ni siasa za CUf na CCm siwez kumuunga mkono Farid kwa hili hapana siwezi

Sasa unaıyunga mkono serikali ambayo ilimteka dr,Uilmboka na hadi sasa bado haijakubali kama ilimteka dr,Ulimboka?
 
nyie ndio wale ambao wakisikia ajali hawaamin hadi waskie au waone kuna watu wamekufa,,,,,au kupoteza viungo,,,pole sana CHUMA,,,,akil yako kama chuma,halisogei hadi lisogezwe

"kuna ajali imetokea kijijini kwenu na bibi yako amevunjika kiuno" amini basi!!
 
Jinsi Damu ya CHADEMA inavyowaathiri katika miili yenu na mulivyo na CHUKI dhidi ya UISLAMU naamini haya ndio mawazo ya wengi hapa JF, munachukulia
kutekwa ni kupigwa ama kuteswa kama
alivyofanywa Dk Ulimboka na
munajisahaulisha kama kuna aina njingi ya utekaji. Ingefurahisha zaidi kama mungekua wawazi na kukubali kwamba utekaji wa makachero wa usalama
wa taifa huwa ni wakutumia akili na maarifa mengi na wala hawakurupuki.
Dr Ulimboka alitekwa
kwa lengo la kumuua na Sheikh Farid katekwa kwa lengo la kuwachanganya wananchi na kuwagawa katika mitizamo yao.
Hapa ni lazima utekaji wao lazima uwe tofauti. CHADEMA muna matatizo sana nyinyi!
Double standard, hawa hawa leo wanasikiliza maneno ya polisi na kuyaunga mkono bila kupinga.
Mbona hawakukubali kuwa Ulimboka hakutekwa na polisi, je kwanini hawaamini kuwa alitekwa na majambazi na si polisi.
Huyo shekh kasema alitekwa polisi kama wao hawakumteka basi waprove hivyo, kwani ni polisi tu wanaoteka? Jamani mbona mnajitia ukichaa!! Ni chuki tu za Uislam?
 
Kamishna wa polisi ZNZ amesema kiongozi wa uamsho sheikh Farid hakutekwa bali alijifanya ametekwa ili kuanzisha vurugu zilizosababisha kifo cha askari.

Pia amesema wamewakamata baadhi ya viongozi wa uamsho na watafikishwa mahakamani kesho Jumatatu.

>>>>>>>>><<<<<<<<<<

OKTOBA 21, 2012 | Zanzibar

Jeshi la Polisi Zanzibar, linawashikilia watu 65 wakiwemo viongozi sita wa kundi la Uamsho na Jumuiya ya Maimam Zanzibar kwa tuhuma za kuchochea ghasia na vurugu zilizosababisha vitendo vya uporaji wa mali na uharibifu wa miundombinu ya barabara.

Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Insptekta Mohammed Mhina, amesema kuwa pamoja na kukamatwa kwa viongozi hao wa Jumuia mbili za Kidini mjini Zanzibar, Polisi pia imewakamata watu wengine sita kwa tuhuma za mauaji ya Askari Polisi.

Insepekta Mhina, amewataja viongozi waliokamatwa kuwa ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maimau Zanzibar Sheikh Faridi Hadi Ahmed(41) mkazi wa Mbuyuni na Sheikh Mselem Ali Mselem(52) wa Kwamtipura ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uamsho Zanzibar.

Wengine ni Sheikhe Azan Khalid Hamadi(48) wa Mtendeni, Hassan Bakari Suleiman(39) wa Tomondo na Ustaadh Mussa Juma Issa(33), Suleiman Juma Suleimain(66) pamoja na Mussa Juma Issa(37) wote wa Makadara mjini Zanzibar.

Inspekta Mhina amesema viongozi waliokamatwa ni wale walikuwa wakihojiwa na Polisi tangu jana kwa lengo la kutafuta ukweli wa taarifa za kutekwa kwa Sheikh Farid Hadi Ahmed kulikopelekea ghasia na uharibifu mbalimbali kabla ya kujitokeza tena hadharani juzi.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake, Kamamishina wa Polisi Zanzibar CP Mussa Ali Mussa amesema kuwa Jeshi la Polisi Visiwani humo linaendelea na operesheni maalumu ya kuhakikisha kuwa kila aliyehusika katika ghasi hizo anakamatwa na kukabili mkono wa sheria.

Akizungumzia maendeleo ya Upelelezi wa Kesi ya Kuuawa kwa Askari Polisi CPL Said Abdarahaman Juma aliyeuawa usiku wa kuamkia Alhamis wiki iliyopita, Kamishna Mussa amesema Polisi wamefanikiwa kuwatia nguvuni watu sita kwa kuhusika na mauaji ya askari huyo.

Amesema hadi sasa Polisi inawashikilia watu sita kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya askari huyo ambapo watuhumiwa watatu walikamatwa mjini Zanzibar na wengine watatu wamekamatwa mkoani Tanga.

Kamishna Mussa amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Abdallah Mohammed Said(35) wa Mwanyanya, Joli Gasuli(20) wa Vuga, Bakari Juma Yusufu(22) wa Mwembe Makumbi na Amour Rished(40) wa Bububu ambao walikamatwa mjini zanzibar siku ya kwanza lilipotokea tukio hilo.

Amewataja watuhumiwa wengine ambao wamekamatiwa Mkoani tanga na ambao tayari wamesharejeshwa Zanzibar kuwa ni Ali salum Seif(21) na Abubakari Haji Mbarouk(32) pamoja na mdogo wake Mohammed Haji Mbarouk(21) wote wakazi wa Ndagaa mkoa wa Kusini Unguja.

Kamishna Mussa amesema Polisi bado inaendelea kuwahoji watuhumiwa hao na wale watakaobainika kuhusika na mauaji ya askari huyo watafikishwa mahakamani.

Amesema kwa ujumla tangu kukamatwa kwa viongozi hao hali ya usalama katika mji wa Zanzibar imerejea upya na wananchi wameombwa kutoshabikia vitendo vyovyote vile vitakavyoweza kupelekea uvunjifu wa amani.

Amewataka Wazazi na walezi kutowaruhusu watoto wao kshiriki katika mikusanyiko na kuwa chanzo cha fujo na kwamba kwa yeyote atakayekaidi agizo hilo atashughulikiwa ipasavyo na mkono wa dola.
Afande Mhina hata ulimboka mlisema aliteswa na jambazi sugu kutoka kenya ambalo lilienda kanisani kuungama
lakini kanisa baadae lilikanusha na juzi Ulimboka mwenyewe alisema polisi na usalama wa taifa wanahusika
kulikuwa na suala la zombe na mauaji ya wafanya biashara wa madini na kuuliwa kwake huko mabe pande kwa kupigwa risasi, polisi mulisema walikua majambazi na walipigwa risasi kutokana na kurushiana risasi huko karibu na chuo kikuu .lakini tume iliyo undwa na rais mwenyewe ikathibitisha hawa sio majambazi na walipigwa risasi huko mabwe pande
pia kuna kifo cha mwandishi wa channel 10 hayati mwangosi..polisi walikanusha kuhusika lakini ushahidi wa video na picha ulionesha wazi polisi walivo husika
pia kuna mauaji ya muuza magazeti pale morogoro
kuna kifo cha mwanachama wa chadema pale arusha , matokeo yote hayo polisi wa nchi hii wamekanusha kuhusika kwake
na hakuna katika historia kwa polisi kufanya mauaji na ikaomba radhi siku zote huwa wanaka nusha hivyo hili suala la Farid ni la kwao na maafisa usalama
na pia hili si suala la kufurahia kwa sababu Farid ni mzanzibari na muislam , kutokana na historia ya jeshi hili yalivyo basi yaliyomtokea farid yanaweza kumtokea Lema, mbowe ama slaa,
majuzi slaa alisema kuna mpango wa uslama wa taifa kutaka kumuua ambapo jeshi la polisi walikanusha na Nchimbi Alitaka Slaa afike polisi kuthibitisha madai yake ..slaa alikataa kushirikiana na polisi kwa sababu tu hawaminiki..
hivyo tuwache chuki..ya kibinafsi kwa sababu ya udini ...haisaidii kitu tusamamie haki...kama polisi wanaweza kumua ama kutaka kumdhuru slaa pia inawezekana kwa farid
mpaka hapo polisi na vyombo vya usalama watakopothibisha beyond reasable doubt kwamba hawahusuki , sio kwa njiia za intimidations basi wao ni first culprits.
 
Anyongwe kabisa huy gaidi maana wameleta madhara makubwa sana na kikundi chake cha ajabu.
 
mkuu..lakini waliowahi tekwa na serikali sote tunajua walivopatikana either hawana kucha na meno au maiti kabisa...lakini shehe karudi na kanzu nyeupeeeeeee hata damu na anatabasamu..hope ulimuona ulimboka alivorudi from mwabepande alikua hacheki anaugulia kiume...i dont buy ulichopost about huu utekaji wa shehe.
Usisahau njaa ya siku tatu mtu anakuwaje!yeye yuko fiti utafikiri katoka kupata msosi heavy,pia kumbuka katika maelezo yake kuwa kuna time walipiga risasi kumtisha itabidi wazanzibar wote waulizwe kama kuna mtu alisikia risasi,amimi nakuambia zanzibar haman nyumba isiyo kuwa na jirani
 
Back
Top Bottom