Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,778
Polisi yazuia mtoto kuoa mwanamke
JESHI la Polisi nchini, limezuia kufungwa ndoa ya mwanafunzi wa kidato cha tatu Hasira Seif (17) wa Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia sakata hilo jana, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema mwanafunzi huyo alitaka kufunga ndoa juzi na Hillary Salum (29), ambaye ni mfanyabiashara wa jijini lakini askari wakafanikiwa kuizuia.
Tumefanikiwa kuzuia ndoa ya mwanafunzi wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko lakini sitatolea maelezo zaidi hadi Jumatatu, napitia kwanza vifungu vya sheria kwa sababu vinakinzana.
Nawasiliana na wanasheria wakati na mimi nikiisoma sheria ya ndoa kwa umakini ili kujua kama ndoa ile ilikuwa kinyume cha sheria na haki za watoto, alisema Kamanda Kova alipozungumza na Tanzania Daima na kuongeza kwamba ndoa ya mwanafunzi huyo ilikuwa ifanyike juzi.
Wakati huo huo, askari polisi usiku wa kuamkia jana walifanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa sita wa ujambazi wanaodaiwa kufanya uhalifu kwenye makao makuu ya Kampuni ya Simu ya Sasatel na vituo viwili vya mafuta.
Katika hilo, Kamanda Kova alisema watuhumiwa hao wamekutwa na mitungi miwili ya gesi, aina tofauti ya funguo bandia zipatazo 73, mitalimbo minne, washeli 12, kisu kimoja, koleo mbili, plasta kubwa moja na festa ya umeme.
Alisema majina ya watuhumiwa hao yamehifadhiwa kwa sababu za kiusalama, kwa kuwa polisi wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine.
Hawa watu sita walikamatwa kutokana na operesheni ya polisi ya kudhibiti uhalifu inayoendelea jijini, wanadaiwa kuiba kwenye Kampuni ya Sasatel makao makuu, kituo cha mafuta GAPCO cha Kunduchi Mtongani na GAPCO Oysterbay. Tutawashikilia na kuwahoji hadi tutakapowapata watuhumiwa wengine wa ujambazi huu, kwa sababu wanaendelea kutajana. Ni watu hatari sana hawa, hivi vitu walivyokutwa navyo ni mabomu, haya yanaweza kulipuka, alisisitiza Kamanda Kova, aliyedai kuwa watafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika. Aidha, jeshi hilo limefanikiwa kukamata bangi na gongo katika msako huo vikiwa vimefungwa kwa namna tofauti na kusema polisi wamo kazini muda wote, ili kuhakikisha hadi tunafika kwenye kipindi cha Uchaguzi Mkuu, matukio ya uhalifu yawe yamepungua.
JESHI la Polisi nchini, limezuia kufungwa ndoa ya mwanafunzi wa kidato cha tatu Hasira Seif (17) wa Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia sakata hilo jana, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema mwanafunzi huyo alitaka kufunga ndoa juzi na Hillary Salum (29), ambaye ni mfanyabiashara wa jijini lakini askari wakafanikiwa kuizuia.
Tumefanikiwa kuzuia ndoa ya mwanafunzi wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko lakini sitatolea maelezo zaidi hadi Jumatatu, napitia kwanza vifungu vya sheria kwa sababu vinakinzana.
Nawasiliana na wanasheria wakati na mimi nikiisoma sheria ya ndoa kwa umakini ili kujua kama ndoa ile ilikuwa kinyume cha sheria na haki za watoto, alisema Kamanda Kova alipozungumza na Tanzania Daima na kuongeza kwamba ndoa ya mwanafunzi huyo ilikuwa ifanyike juzi.
Wakati huo huo, askari polisi usiku wa kuamkia jana walifanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa sita wa ujambazi wanaodaiwa kufanya uhalifu kwenye makao makuu ya Kampuni ya Simu ya Sasatel na vituo viwili vya mafuta.
Katika hilo, Kamanda Kova alisema watuhumiwa hao wamekutwa na mitungi miwili ya gesi, aina tofauti ya funguo bandia zipatazo 73, mitalimbo minne, washeli 12, kisu kimoja, koleo mbili, plasta kubwa moja na festa ya umeme.
Alisema majina ya watuhumiwa hao yamehifadhiwa kwa sababu za kiusalama, kwa kuwa polisi wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine.
Hawa watu sita walikamatwa kutokana na operesheni ya polisi ya kudhibiti uhalifu inayoendelea jijini, wanadaiwa kuiba kwenye Kampuni ya Sasatel makao makuu, kituo cha mafuta GAPCO cha Kunduchi Mtongani na GAPCO Oysterbay. Tutawashikilia na kuwahoji hadi tutakapowapata watuhumiwa wengine wa ujambazi huu, kwa sababu wanaendelea kutajana. Ni watu hatari sana hawa, hivi vitu walivyokutwa navyo ni mabomu, haya yanaweza kulipuka, alisisitiza Kamanda Kova, aliyedai kuwa watafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika. Aidha, jeshi hilo limefanikiwa kukamata bangi na gongo katika msako huo vikiwa vimefungwa kwa namna tofauti na kusema polisi wamo kazini muda wote, ili kuhakikisha hadi tunafika kwenye kipindi cha Uchaguzi Mkuu, matukio ya uhalifu yawe yamepungua.