Polisi yasitisha utendaji wa Chama cha Kutetea Abiria isipokuwa kwa mkoa wa Dar

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,889
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini DCP Mohamed Mpinga amesitisha utendaji wa chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA) kuendelea na shuguli zake katika mikoa yote nchini isipokuwa kwa mkoa wa Dar es Salaam pekee
mpinga_0.jpg

DCP Mohamed Mpinga

Akitaja sababu za kusitisha utendaji wa chama hicho leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa ripoti ya namna walivyojipanga kuzuia ajali za Barabarani DCP Mpinga amesema, utendaji mbaya na kukiuka maadili na kujikita katika usimamizi wa sheria badala ya kutoa elimu unaofanywa na chama hicho ndiyo sababu ya kusitishwa kwa utendaji wao na kwamba kuanzia sasa shughuli zao zitafanywa na Mabalozi wa Usalama Barabarani.
chakua.JPG


Hassan Mchanjama - Mwenyekiti CHAKUA

Muda mfupi baada ya kutolewa kwa tamko hilo, tulifanikiwa kumpata Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa, Bwana Hassan Mchanjama ambaye alikanusha tuhuma hizo huku akisema kuwa, kuzuia utendaji wa chama cha abiria kwa kile alichokiita ni maslahi binafsi ni kuwanyima wananchi mahala pa kuwasilisha kero zao ambapo amebainisha kuwa chama hicho hakijawahi kukiuka taratibu zake za utendaji kama ilivyoelezwa.

Mbali na suala hilo DCP Mohamed Mpinga amewataka wamiliki wa magari kote nchini kuondoa na kuacha mara moja kutumia taa zenye mwanga mkali maarufu kwa jina la 'Sportlights' katika vyombo vyao vya moto kwani taa hizo ziimekuwa kero kwa madereva wengine na kuchangia ajali za barabarani nchini.

Chanzo: IPP Media
 
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini DCP Mohamed Mpinga amesitisha utendaji wa chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA) kuendelea na shuguli zake katika mikoa yote nchini isipokuwa kwa mkoa wa Dar es Salaam pekee.

Akitaja sababu za kusitisha utendaji wa chama hicho leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa ripoti ya namna walivyojipanga kuzuia ajali za Barabarani DCP Mpinga amesema, utendaji mbaya na kukiuka maadili na kujikita katika usimamizi wa sheria badala ya kutoa elimu unaofanywa na chama hicho ndiyo sababu ya kusitishwa kwa utendaji wao na kwamba kuanzia sasa shughuli zao zitafanywa na Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Muda mfupi baada ya kutolewa kwa tamko hilo, tulifanikiwa kumpata Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa, Bwana Hassan Mchanjama ambaye alikanusha tuhuma hizo huku akisema kuwa, kuzuia utendaji wa chama cha abiria kwa kile alichokiita ni maslahi binafsi ni kuwanyima wananchi mahala pa kuwasilisha kero zao ambapo amebainisha kuwa chama hicho hakijawahi kukiuka taratibu zake za utendaji kama ilivyoelezwa.

Mbali na suala hilo DCP Mohamed Mpinga amewataka wamiliki wa magari kote nchini kuondoa na kuacha mara moja kutumia taa zenye mwanga mkali maarufu kwa jina la 'Sportlights' katika vyombo vyao vya moto kwani taa hizo ziimekuwa kero kwa madereva wengine na kuchangia ajali za barabarani nchini.
 
Naona wanatafuta ulaji mwingine kwenye hizi taa ,Magari ya sasa hivi Taa zake ni kama sport lights tu waende Japan kwenye viwanda wawakataze kutengeneza hizo taa
 
Kwa hili la sport lights nawaunga mkono asilimia miamoja zimekua kero kubwa
 
Back
Top Bottom