Polisi yaruhusu mikutano CHADEMA tangu jana: NINI MAANA YAKE?

AmaniKatoshi

Senior Member
Mar 31, 2009
158
14
Polisi yaruhusu mikutano CHADEMA.


Na Tumaini Makene.

SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulilalamikia Jeshi la Polisi juu ya kutoa amri ya kuzuia mikutano yake ya hadhara na ile ya kuwapokea wabunge wa chama hicho maeneo mbalimbali nchini, jeshi hilo limeondoa rasmi zuio hilo.

Jeshi hilo limesema kuwa limeondoa rasmi zuio hilo kuanzia jana baada ya 'uchaguzi kumalizika rasmi juzi' kwa mujibu wa taratibu za ndani za usimamizi wa shughuli ya uchaguzi, ambazo walikuwa wamejiwekea, ambazo hazikuwa zikimlenga mtu wala chama chochote cha siasa.

Jana CHADEMA kilikaririwa na vyombo vya habari kikisema kuwa vitendo hivyo vya polisi vilikuwa vinashiria hatari kwa demokrasia nchini, kuvunja haki za kikatiba na za kisheria za wananchi, huku vikiwa ni dalili ya nchi kupelekwa katika 'dola ya kipolisi,' kama vile ilivyokuwa katika nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini wakati wa utawala wa makaburu na Kenya wakati wa utawala wa Rais wa Pili, Daniel Arap Moi.

Vyombo vya habari vilimnukuu Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu akisema kuwa chama hicho hakitakuwa tayari kunyamazia hatua hiyo, kwani ingeweza kuwa mwendelezo wa kuminya haki ya watu kujumuika na kujadili mustakabli wa nchi yao, kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Akizungumza na Majira jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo wa maandamano na mikusanyiko ya kuwapokea wabunge na mikutano mingine ya kawaida ya hadhara, ilikuwa sehemu ya utaratibu wa jeshi hilo wakati na baada ya uchaguzi.

Bw. Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo haukumlenga mtu yeyote wala chama chochote kile cha siasa, bali ulikuwa ukizingatia hali halisi ya nchi baada ya uchaguzi, ambapo "serikali ilikuwa haijaundwa wala mawaziri hawajateuliwa," hivyo wameondoa rasmi amri hiyo jana.

"Kusema ukweli nimeshaongea na vyombo vya habari vingi leo juu ya suala hilo na nimeshatoa ufafanuzi. Tulichokuwa tumezuia ni maandamano na kupongezana si mikutano...unajua baada ya bunge kumalizika kulitolewa maombi mbalimbali ya maandamano watu wakitaka kuwapokea wabunge wao.

"Lakini unajua maandamano ni kitu kingine na mikutano ni kitu kingine, kila kimoja kina utaratibu wake, mapema ilikuwa imetolewa amri ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi kusimamia mambo yote hayo ya maandamano na mikutano...lakini amri hiyo sasa imeondolewa rasmi leo (jana) baada ya uchaguzi kuisha rasmi jana (juzi)," alisema Bw. Mtweve na kuongeza;

"Kwa mujibu wa utaratibu tuliokuwa tumejiwekea ndani ya jeshi, uchaguzi umemalizika jana (jana)...ma-OCD walipewa maelekezo ya kutoruhusu masuala ya maandamano kwani yale hayaangalii tu kitendo chako cha mwisho, bali yanahusisha taasisi nyingi na masuala ya usalama wa mali za watu, suala hilo halikumlenga mtu wala chama cha siasa...

"Hata hivyo, tulijaribu kuhoji kama ni suala la kupongezana kwani ni lazima watu wapongezane kwa kukusanyika uwanjani, wangeweza kufanya hata hotelini au ukumbini mahali," alisema.

Bw. Mtweve aliongeza kusema kuwa haikuwa vizuri baada ya uchaguzi kuruhusu maandamano na mikutano ya hadhara kwani nchi ilikuwa imetoka katika uchaguzi, huku 'mambo yakiwa hayajakaa sawa', serikali ikiwa haijaundwa na mawaziri hawajateuliwa.

Majira lilipotaka kujua kama jeshi hilo lilikuwa na wasiwasi zaidi na maandamano na mapokezi ya wabunge kwa nini lilizuia hata mikutano ya hadhara kama vile huko Segerea, Dar es Salaam, Bw. Mtweve alisema kuwa hiyo ilikuwa ni kwa mujibu wa "operetion order" (amri ya utendaji).

Alisisitiza kuwa kuanzia jana utaratibu wa kuomba na kukubaliwa mikutano ya hadhara na maandamano unarudi kama kawaida chini ya makamanda wa polisi wa wilaya.

Wakati huo huo, CHADEMA kimepongeza hatua ya kuondoa amri hiyo na kusema kuwa ni jambo zuri lakini halizuii kusudio lake la kufikisha hoja yake bungeni juu ya uvunjifu wa Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga ya Bunge ya mwaka 1988, kikisema kuwa polisi hawana ruhusa ya kuzuia mikutano ya wabunge "pale serikali inapokuwa haipo."

Akipongeza hatua hiyo, Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu alisema "Kama wameiondoa basi ni jambo zuri sana...ni kitendo kizuri lakini hakituzuii kwenda kuhoji bungeni kwa nini wabunge wetu walizuia kufanya kazi...kufanya mikutano.

"Hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kuvunja au kukiuka sheria ya haki, mamlaka na kinga ya bunge ikiwa serikali haipo au mawaziri hawajateuliwa," alisema Bw. Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni

Chanzo ni Gazeti la Majira la tarehe 30/11/2010 GAZETI HURU LA KILA SIKU:

My take:

1. Kwa nini kizuizi kuondolewa siku moja baada ya Lisu na Chadema kutoa tamko?
2. Je linahitajika somo kwa polisi kuhusu vifungu vya katiba?
3. Hiyo mamlaka ya juu Mtweve anayotaja niipi?
4. Kama Mwema alizuia kwa kuongea na media, kwa nini jana anamtuma mkurugenzi wa fedha?

There are more questions than answers!
 
Baada ya Mawaziri kuapishwa na rasmi, na jeshi la polisi kuhakikisha kuwa kutakuwa na usalama wa kutosha kwa raia wote, wawe Chadema, CCM, Cuf au wa chama kingine chochote na wale wasio na chama.

Walizuiliwa kufanya maandamano.

Sasa wafanye mikutano, kumbuka, sio maandamano. Mikutano.

Na ikiwa hiyo mikutano itasabisha uvunjifu wa amani. Basi hao wavunja amani watashughulikiwa ipasavyo.
 
Baada ya Mawaziri kuapishwa na rasmi, na jeshi la polisi kuhakikisha kuwa kutakuwa na usalama wa kutosha kwa raia wote, wawe Chadema, CCM, Cuf au wa chama kingine chochote na wale wasio na chama.

Walizuiliwa kufanya maandamano.

Sasa wafanye mikutano, kumbuka, sio maandamano. Mikutano.

Na ikiwa hiyo mikutano itasabisha uvunjifu wa amani. Basi hao wavunja amani watashughulikiwa ipasavyo.

Kuapishwa kwa mawaziri kunahusiana vp na mikutano ya CHADEMA na wananchi?
Kumbuka swala ni mikutano na sio vurugu.
Pia haimanishi kwamba watu wakiandamana basi wanafanya fujo. Noo
 
Baada ya Mawaziri kuapishwa na rasmi, na jeshi la polisi kuhakikisha kuwa kutakuwa na usalama wa kutosha kwa raia wote, wawe Chadema, CCM, Cuf au wa chama kingine chochote na wale wasio na chama.

Walizuiliwa kufanya maandamano.

Sasa wafanye mikutano, kumbuka, sio maandamano. Mikutano.

Na ikiwa hiyo mikutano itasabisha uvunjifu wa amani. Basi hao wavunja amani watashughulikiwa ipasavyo.


Sawa afande tumekusikia ... lakini na maandamano tutafanya pia.
 
hiyo tz zaidi tuijuavyo,nimewahi kuuliza swali hapa jf kuwa hawa polisi wapo kwa maslahi ya nani? sikupata majibu sasa polepole majibu yanakuja juu ya jeshi la polisi la tz,nadhani wapo kwa maslahi ya watu wachache ambao wakisema jambo basi polisi hutekeleza kwa vitendo.
ipo siku tutaliona jsho la kunguni

mapinduziii daimaaaa
 
Hicho kikao chao walikaa juzi usiku na kuondoa hiyo amri usiku huohuo hadi jana asubuhi watangaze kuondoa rasmi? hivi uchaguzi unaisha baada ya kuhesabiwa kura na mshindi kupatikana au ni hadi baraza litangazwe? na kama hivyo ndivyo? kwani baraza lilitangazwa jana au juzi? kuna uhusiano gani wa baraza na mikutano ya vyama? shiiiii.....
 
CCM wajinga sana...yaani ukiwa mwizi unakuwa muoga sana sijui kwa nini
 
Hizi sababu za polisi mbona hazikutolewa katika hati ya zuio (kama ulikuwepo)? Lakini Chadema kwa mara nyingine wamethibitisha umakini wao na uwezo wa kudai haki kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo. Wamevumilia na kudai haki yao bila kuleta fujo ingawa katika mchakato huo baadhi watu tayari walidai Chadema wanataka kuleta fujo

well done Chadema, lazima tutafika
 
CCM wajinga sana...yaani ukiwa mwizi unakuwa muoga sana sijui kwa nini

Hata wakizuia mikutano si wananchi wenye akili nzuri wameshajua kwamba rais wao hakushinda kihalali? Chadema kususa hotuba ilikuwa bao la dhahabu
 
Hao ndo Polisi bana! wanatishiwa asubuhi, jioni wanaondoa ban!! hahahaha!
 
Baada ya Mawaziri kuapishwa na rasmi, na jeshi la polisi kuhakikisha kuwa kutakuwa na usalama wa kutosha kwa raia wote, wawe Chadema, CCM, Cuf au wa chama kingine chochote na wale wasio na chama.

Walizuiliwa kufanya maandamano.

Sasa wafanye mikutano, kumbuka, sio maandamano. Mikutano.

Na ikiwa hiyo mikutano itasabisha uvunjifu wa amani. Basi hao wavunja amani watashughulikiwa ipasavyo.

Al zawahiri hajambo?....mmemaliza mafunzo
 
Polisi yaruhusu mikutano CHADEMA.


Na Tumaini Makene.

SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulilalamikia Jeshi la Polisi juu ya kutoa amri ya kuzuia mikutano yake ya hadhara na ile ya kuwapokea wabunge wa chama hicho maeneo mbalimbali nchini, jeshi hilo limeondoa rasmi zuio hilo.

Jeshi hilo limesema kuwa limeondoa rasmi zuio hilo kuanzia jana baada ya 'uchaguzi kumalizika rasmi juzi' kwa mujibu wa taratibu za ndani za usimamizi wa shughuli ya uchaguzi, ambazo walikuwa wamejiwekea, ambazo hazikuwa zikimlenga mtu wala chama chochote cha siasa.

Jana CHADEMA kilikaririwa na vyombo vya habari kikisema kuwa vitendo hivyo vya polisi vilikuwa vinashiria hatari kwa demokrasia nchini, kuvunja haki za kikatiba na za kisheria za wananchi, huku vikiwa ni dalili ya nchi kupelekwa katika 'dola ya kipolisi,' kama vile ilivyokuwa katika nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini wakati wa utawala wa makaburu na Kenya wakati wa utawala wa Rais wa Pili, Daniel Arap Moi.

Vyombo vya habari vilimnukuu Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu akisema kuwa chama hicho hakitakuwa tayari kunyamazia hatua hiyo, kwani ingeweza kuwa mwendelezo wa kuminya haki ya watu kujumuika na kujadili mustakabli wa nchi yao, kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Akizungumza na Majira jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo wa maandamano na mikusanyiko ya kuwapokea wabunge na mikutano mingine ya kawaida ya hadhara, ilikuwa sehemu ya utaratibu wa jeshi hilo wakati na baada ya uchaguzi.

Bw. Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo haukumlenga mtu yeyote wala chama chochote kile cha siasa, bali ulikuwa ukizingatia hali halisi ya nchi baada ya uchaguzi, ambapo "serikali ilikuwa haijaundwa wala mawaziri hawajateuliwa," hivyo wameondoa rasmi amri hiyo jana.

"Kusema ukweli nimeshaongea na vyombo vya habari vingi leo juu ya suala hilo na nimeshatoa ufafanuzi. Tulichokuwa tumezuia ni maandamano na kupongezana si mikutano...unajua baada ya bunge kumalizika kulitolewa maombi mbalimbali ya maandamano watu wakitaka kuwapokea wabunge wao.

"Lakini unajua maandamano ni kitu kingine na mikutano ni kitu kingine, kila kimoja kina utaratibu wake, mapema ilikuwa imetolewa amri ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi kusimamia mambo yote hayo ya maandamano na mikutano...lakini amri hiyo sasa imeondolewa rasmi leo (jana) baada ya uchaguzi kuisha rasmi jana (juzi)," alisema Bw. Mtweve na kuongeza;

"Kwa mujibu wa utaratibu tuliokuwa tumejiwekea ndani ya jeshi, uchaguzi umemalizika jana (jana)...ma-OCD walipewa maelekezo ya kutoruhusu masuala ya maandamano kwani yale hayaangalii tu kitendo chako cha mwisho, bali yanahusisha taasisi nyingi na masuala ya usalama wa mali za watu, suala hilo halikumlenga mtu wala chama cha siasa...

"Hata hivyo, tulijaribu kuhoji kama ni suala la kupongezana kwani ni lazima watu wapongezane kwa kukusanyika uwanjani, wangeweza kufanya hata hotelini au ukumbini mahali," alisema.

Bw. Mtweve aliongeza kusema kuwa haikuwa vizuri baada ya uchaguzi kuruhusu maandamano na mikutano ya hadhara kwani nchi ilikuwa imetoka katika uchaguzi, huku 'mambo yakiwa hayajakaa sawa', serikali ikiwa haijaundwa na mawaziri hawajateuliwa.

Majira lilipotaka kujua kama jeshi hilo lilikuwa na wasiwasi zaidi na maandamano na mapokezi ya wabunge kwa nini lilizuia hata mikutano ya hadhara kama vile huko Segerea, Dar es Salaam, Bw. Mtweve alisema kuwa hiyo ilikuwa ni kwa mujibu wa "operetion order" (amri ya utendaji).

Alisisitiza kuwa kuanzia jana utaratibu wa kuomba na kukubaliwa mikutano ya hadhara na maandamano unarudi kama kawaida chini ya makamanda wa polisi wa wilaya.

Wakati huo huo, CHADEMA kimepongeza hatua ya kuondoa amri hiyo na kusema kuwa ni jambo zuri lakini halizuii kusudio lake la kufikisha hoja yake bungeni juu ya uvunjifu wa Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga ya Bunge ya mwaka 1988, kikisema kuwa polisi hawana ruhusa ya kuzuia mikutano ya wabunge "pale serikali inapokuwa haipo."

Akipongeza hatua hiyo, Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu alisema "Kama wameiondoa basi ni jambo zuri sana...ni kitendo kizuri lakini hakituzuii kwenda kuhoji bungeni kwa nini wabunge wetu walizuia kufanya kazi...kufanya mikutano.

"Hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kuvunja au kukiuka sheria ya haki, mamlaka na kinga ya bunge ikiwa serikali haipo au mawaziri hawajateuliwa," alisema Bw. Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni

Chanzo ni Gazeti la Majira la tarehe 30/11/2010 GAZETI HURU LA KILA SIKU:

My take:

1. Kwa nini kizuizi kuondolewa siku moja baada ya Lisu na Chadema kutoa tamko?
2. Je linahitajika somo kwa polisi kuhusu vifungu vya katiba?
3. Hiyo mamlaka ya juu Mtweve anayotaja niipi?
4. Kama Mwema alizuia kwa kuongea na media, kwa nini jana anamtuma mkurugenzi wa fedha?

There are more questions than answers!
Tatizo polisi hawajui sheria wala katiba ya nchi, na wanasema na kutenda kutokana na maamuzi ya wanasiasa na si kwa mjibu wa kanuni na sheria. Jeshi la polisi limekuwa genge la wahuni, watu wanakwenda siku hizi kwa sababu tu mtaani panachimbika na si kwa nia na moyo thabiti wa kutumikia wananchi.
 
IGP Mwema naye yupo kwenye genge la waasisi wa kuvunja amani nchini linaloongozwa na Mkwere na RH wa CUF
 
Hivi mbona nchi nyingine zinafanya maandamano??? Tanzania maandamano wanayaogopa sana - why????? Na polisi wa CCM - yaani wenyewe wana shida kama nini - ila hata mseme mnafanya maandamano kwa ajili ya kuwatetea - bado watakataa - ama kweli umaskini saa ingine unaweza kuingia hadi kwenye ubongo wa mtu!!!!!!!!!!

Wanatakakiwa POLISI nao waandamane siku moja.......................:teeth::teeth::teeth:
 
Wameogopa nguvu ya wananchi. Usicheze na peoples power. CHADEMA ni chama cha wasomi baada ya kuona CHADEMA imetoa vifungu vya sheria vinavyowakaba ndo wanajifanya wanatengua Amri. Plato alishasema kazi za polisi ni za Iron boys, watu wanaotumia nguvu nyingi kuliko akili ndo maana wanafanya mambo bila kutafakari
Hivi CUF hawakuliona suala hili na vifungu vya sheria hawakuviona? Kweli CUF sio chama cha upinzani nadhani 2015 tutakipoteza kabisa kwa huku bara kitabaki visiwani
 
:confused2:
Polisi yaruhusu mikutano CHADEMA.


Na Tumaini Makene.

SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulilalamikia Jeshi la Polisi juu ya kutoa amri ya kuzuia mikutano yake ya hadhara na ile ya kuwapokea wabunge wa chama hicho maeneo mbalimbali nchini, jeshi hilo limeondoa rasmi zuio hilo.

Jeshi hilo limesema kuwa limeondoa rasmi zuio hilo kuanzia jana baada ya 'uchaguzi kumalizika rasmi juzi' kwa mujibu wa taratibu za ndani za usimamizi wa shughuli ya uchaguzi, ambazo walikuwa wamejiwekea, ambazo hazikuwa zikimlenga mtu wala chama chochote cha siasa.

Jana CHADEMA kilikaririwa na vyombo vya habari kikisema kuwa vitendo hivyo vya polisi vilikuwa vinashiria hatari kwa demokrasia nchini, kuvunja haki za kikatiba na za kisheria za wananchi, huku vikiwa ni dalili ya nchi kupelekwa katika 'dola ya kipolisi,' kama vile ilivyokuwa katika nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini wakati wa utawala wa makaburu na Kenya wakati wa utawala wa Rais wa Pili, Daniel Arap Moi.

Vyombo vya habari vilimnukuu Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu akisema kuwa chama hicho hakitakuwa tayari kunyamazia hatua hiyo, kwani ingeweza kuwa mwendelezo wa kuminya haki ya watu kujumuika na kujadili mustakabli wa nchi yao, kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Akizungumza na Majira jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo wa maandamano na mikusanyiko ya kuwapokea wabunge na mikutano mingine ya kawaida ya hadhara, ilikuwa sehemu ya utaratibu wa jeshi hilo wakati na baada ya uchaguzi.

Bw. Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo haukumlenga mtu yeyote wala chama chochote kile cha siasa, bali ulikuwa ukizingatia hali halisi ya nchi baada ya uchaguzi, ambapo "serikali ilikuwa haijaundwa wala mawaziri hawajateuliwa," hivyo wameondoa rasmi amri hiyo jana.

"Kusema ukweli nimeshaongea na vyombo vya habari vingi leo juu ya suala hilo na nimeshatoa ufafanuzi. Tulichokuwa tumezuia ni maandamano na kupongezana si mikutano...unajua baada ya bunge kumalizika kulitolewa maombi mbalimbali ya maandamano watu wakitaka kuwapokea wabunge wao.

"Lakini unajua maandamano ni kitu kingine na mikutano ni kitu kingine, kila kimoja kina utaratibu wake, mapema ilikuwa imetolewa amri ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi kusimamia mambo yote hayo ya maandamano na mikutano...lakini amri hiyo sasa imeondolewa rasmi leo (jana) baada ya uchaguzi kuisha rasmi jana (juzi)," alisema Bw. Mtweve na kuongeza;

"Kwa mujibu wa utaratibu tuliokuwa tumejiwekea ndani ya jeshi, uchaguzi umemalizika jana (jana)...ma-OCD walipewa maelekezo ya kutoruhusu masuala ya maandamano kwani yale hayaangalii tu kitendo chako cha mwisho, bali yanahusisha taasisi nyingi na masuala ya usalama wa mali za watu, suala hilo halikumlenga mtu wala chama cha siasa...

"Hata hivyo, tulijaribu kuhoji kama ni suala la kupongezana kwani ni lazima watu wapongezane kwa kukusanyika uwanjani, wangeweza kufanya hata hotelini au ukumbini mahali," alisema.

Bw. Mtweve aliongeza kusema kuwa haikuwa vizuri baada ya uchaguzi kuruhusu maandamano na mikutano ya hadhara kwani nchi ilikuwa imetoka katika uchaguzi, huku 'mambo yakiwa hayajakaa sawa', serikali ikiwa haijaundwa na mawaziri hawajateuliwa.

Majira lilipotaka kujua kama jeshi hilo lilikuwa na wasiwasi zaidi na maandamano na mapokezi ya wabunge kwa nini lilizuia hata mikutano ya hadhara kama vile huko Segerea, Dar es Salaam, Bw. Mtweve alisema kuwa hiyo ilikuwa ni kwa mujibu wa "operetion order" (amri ya utendaji).

Alisisitiza kuwa kuanzia jana utaratibu wa kuomba na kukubaliwa mikutano ya hadhara na maandamano unarudi kama kawaida chini ya makamanda wa polisi wa wilaya.

Wakati huo huo, CHADEMA kimepongeza hatua ya kuondoa amri hiyo na kusema kuwa ni jambo zuri lakini halizuii kusudio lake la kufikisha hoja yake bungeni juu ya uvunjifu wa Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga ya Bunge ya mwaka 1988, kikisema kuwa polisi hawana ruhusa ya kuzuia mikutano ya wabunge "pale serikali inapokuwa haipo."

Akipongeza hatua hiyo, Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu alisema "Kama wameiondoa basi ni jambo zuri sana...ni kitendo kizuri lakini hakituzuii kwenda kuhoji bungeni kwa nini wabunge wetu walizuia kufanya kazi...kufanya mikutano.

"Hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kuvunja au kukiuka sheria ya haki, mamlaka na kinga ya bunge ikiwa serikali haipo au mawaziri hawajateuliwa," alisema Bw. Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni

Chanzo ni Gazeti la Majira la tarehe 30/11/2010 GAZETI HURU LA KILA SIKU:

My take:

1. Kwa nini kizuizi kuondolewa siku moja baada ya Lisu na Chadema kutoa tamko?
2. Je linahitajika somo kwa polisi kuhusu vifungu vya katiba?
3. Hiyo mamlaka ya juu Mtweve anayotaja niipi?
4. Kama Mwema alizuia kwa kuongea na media, kwa nini jana anamtuma mkurugenzi wa fedha?

There are more questions than answers!

:nono:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom