AmaniKatoshi
Senior Member
- Mar 31, 2009
- 158
- 14
Polisi yaruhusu mikutano CHADEMA.
Na Tumaini Makene.
SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulilalamikia Jeshi la Polisi juu ya kutoa amri ya kuzuia mikutano yake ya hadhara na ile ya kuwapokea wabunge wa chama hicho maeneo mbalimbali nchini, jeshi hilo limeondoa rasmi zuio hilo.
Jeshi hilo limesema kuwa limeondoa rasmi zuio hilo kuanzia jana baada ya 'uchaguzi kumalizika rasmi juzi' kwa mujibu wa taratibu za ndani za usimamizi wa shughuli ya uchaguzi, ambazo walikuwa wamejiwekea, ambazo hazikuwa zikimlenga mtu wala chama chochote cha siasa.
Jana CHADEMA kilikaririwa na vyombo vya habari kikisema kuwa vitendo hivyo vya polisi vilikuwa vinashiria hatari kwa demokrasia nchini, kuvunja haki za kikatiba na za kisheria za wananchi, huku vikiwa ni dalili ya nchi kupelekwa katika 'dola ya kipolisi,' kama vile ilivyokuwa katika nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini wakati wa utawala wa makaburu na Kenya wakati wa utawala wa Rais wa Pili, Daniel Arap Moi.
Vyombo vya habari vilimnukuu Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu akisema kuwa chama hicho hakitakuwa tayari kunyamazia hatua hiyo, kwani ingeweza kuwa mwendelezo wa kuminya haki ya watu kujumuika na kujadili mustakabli wa nchi yao, kwa mujibu wa katiba ya nchi.
Akizungumza na Majira jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo wa maandamano na mikusanyiko ya kuwapokea wabunge na mikutano mingine ya kawaida ya hadhara, ilikuwa sehemu ya utaratibu wa jeshi hilo wakati na baada ya uchaguzi.
Bw. Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo haukumlenga mtu yeyote wala chama chochote kile cha siasa, bali ulikuwa ukizingatia hali halisi ya nchi baada ya uchaguzi, ambapo "serikali ilikuwa haijaundwa wala mawaziri hawajateuliwa," hivyo wameondoa rasmi amri hiyo jana.
"Kusema ukweli nimeshaongea na vyombo vya habari vingi leo juu ya suala hilo na nimeshatoa ufafanuzi. Tulichokuwa tumezuia ni maandamano na kupongezana si mikutano...unajua baada ya bunge kumalizika kulitolewa maombi mbalimbali ya maandamano watu wakitaka kuwapokea wabunge wao.
"Lakini unajua maandamano ni kitu kingine na mikutano ni kitu kingine, kila kimoja kina utaratibu wake, mapema ilikuwa imetolewa amri ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi kusimamia mambo yote hayo ya maandamano na mikutano...lakini amri hiyo sasa imeondolewa rasmi leo (jana) baada ya uchaguzi kuisha rasmi jana (juzi)," alisema Bw. Mtweve na kuongeza;
"Kwa mujibu wa utaratibu tuliokuwa tumejiwekea ndani ya jeshi, uchaguzi umemalizika jana (jana)...ma-OCD walipewa maelekezo ya kutoruhusu masuala ya maandamano kwani yale hayaangalii tu kitendo chako cha mwisho, bali yanahusisha taasisi nyingi na masuala ya usalama wa mali za watu, suala hilo halikumlenga mtu wala chama cha siasa...
"Hata hivyo, tulijaribu kuhoji kama ni suala la kupongezana kwani ni lazima watu wapongezane kwa kukusanyika uwanjani, wangeweza kufanya hata hotelini au ukumbini mahali," alisema.
Bw. Mtweve aliongeza kusema kuwa haikuwa vizuri baada ya uchaguzi kuruhusu maandamano na mikutano ya hadhara kwani nchi ilikuwa imetoka katika uchaguzi, huku 'mambo yakiwa hayajakaa sawa', serikali ikiwa haijaundwa na mawaziri hawajateuliwa.
Majira lilipotaka kujua kama jeshi hilo lilikuwa na wasiwasi zaidi na maandamano na mapokezi ya wabunge kwa nini lilizuia hata mikutano ya hadhara kama vile huko Segerea, Dar es Salaam, Bw. Mtweve alisema kuwa hiyo ilikuwa ni kwa mujibu wa "operetion order" (amri ya utendaji).
Alisisitiza kuwa kuanzia jana utaratibu wa kuomba na kukubaliwa mikutano ya hadhara na maandamano unarudi kama kawaida chini ya makamanda wa polisi wa wilaya.
Wakati huo huo, CHADEMA kimepongeza hatua ya kuondoa amri hiyo na kusema kuwa ni jambo zuri lakini halizuii kusudio lake la kufikisha hoja yake bungeni juu ya uvunjifu wa Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga ya Bunge ya mwaka 1988, kikisema kuwa polisi hawana ruhusa ya kuzuia mikutano ya wabunge "pale serikali inapokuwa haipo."
Akipongeza hatua hiyo, Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu alisema "Kama wameiondoa basi ni jambo zuri sana...ni kitendo kizuri lakini hakituzuii kwenda kuhoji bungeni kwa nini wabunge wetu walizuia kufanya kazi...kufanya mikutano.
"Hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kuvunja au kukiuka sheria ya haki, mamlaka na kinga ya bunge ikiwa serikali haipo au mawaziri hawajateuliwa," alisema Bw. Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni
Chanzo ni Gazeti la Majira la tarehe 30/11/2010 GAZETI HURU LA KILA SIKU:
My take:
1. Kwa nini kizuizi kuondolewa siku moja baada ya Lisu na Chadema kutoa tamko?
2. Je linahitajika somo kwa polisi kuhusu vifungu vya katiba?
3. Hiyo mamlaka ya juu Mtweve anayotaja niipi?
4. Kama Mwema alizuia kwa kuongea na media, kwa nini jana anamtuma mkurugenzi wa fedha?
There are more questions than answers!
Na Tumaini Makene.
SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulilalamikia Jeshi la Polisi juu ya kutoa amri ya kuzuia mikutano yake ya hadhara na ile ya kuwapokea wabunge wa chama hicho maeneo mbalimbali nchini, jeshi hilo limeondoa rasmi zuio hilo.
Jeshi hilo limesema kuwa limeondoa rasmi zuio hilo kuanzia jana baada ya 'uchaguzi kumalizika rasmi juzi' kwa mujibu wa taratibu za ndani za usimamizi wa shughuli ya uchaguzi, ambazo walikuwa wamejiwekea, ambazo hazikuwa zikimlenga mtu wala chama chochote cha siasa.
Jana CHADEMA kilikaririwa na vyombo vya habari kikisema kuwa vitendo hivyo vya polisi vilikuwa vinashiria hatari kwa demokrasia nchini, kuvunja haki za kikatiba na za kisheria za wananchi, huku vikiwa ni dalili ya nchi kupelekwa katika 'dola ya kipolisi,' kama vile ilivyokuwa katika nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini wakati wa utawala wa makaburu na Kenya wakati wa utawala wa Rais wa Pili, Daniel Arap Moi.
Vyombo vya habari vilimnukuu Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu akisema kuwa chama hicho hakitakuwa tayari kunyamazia hatua hiyo, kwani ingeweza kuwa mwendelezo wa kuminya haki ya watu kujumuika na kujadili mustakabli wa nchi yao, kwa mujibu wa katiba ya nchi.
Akizungumza na Majira jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo wa maandamano na mikusanyiko ya kuwapokea wabunge na mikutano mingine ya kawaida ya hadhara, ilikuwa sehemu ya utaratibu wa jeshi hilo wakati na baada ya uchaguzi.
Bw. Mtweve alisema kuwa uzuiaji huo haukumlenga mtu yeyote wala chama chochote kile cha siasa, bali ulikuwa ukizingatia hali halisi ya nchi baada ya uchaguzi, ambapo "serikali ilikuwa haijaundwa wala mawaziri hawajateuliwa," hivyo wameondoa rasmi amri hiyo jana.
"Kusema ukweli nimeshaongea na vyombo vya habari vingi leo juu ya suala hilo na nimeshatoa ufafanuzi. Tulichokuwa tumezuia ni maandamano na kupongezana si mikutano...unajua baada ya bunge kumalizika kulitolewa maombi mbalimbali ya maandamano watu wakitaka kuwapokea wabunge wao.
"Lakini unajua maandamano ni kitu kingine na mikutano ni kitu kingine, kila kimoja kina utaratibu wake, mapema ilikuwa imetolewa amri ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi kusimamia mambo yote hayo ya maandamano na mikutano...lakini amri hiyo sasa imeondolewa rasmi leo (jana) baada ya uchaguzi kuisha rasmi jana (juzi)," alisema Bw. Mtweve na kuongeza;
"Kwa mujibu wa utaratibu tuliokuwa tumejiwekea ndani ya jeshi, uchaguzi umemalizika jana (jana)...ma-OCD walipewa maelekezo ya kutoruhusu masuala ya maandamano kwani yale hayaangalii tu kitendo chako cha mwisho, bali yanahusisha taasisi nyingi na masuala ya usalama wa mali za watu, suala hilo halikumlenga mtu wala chama cha siasa...
"Hata hivyo, tulijaribu kuhoji kama ni suala la kupongezana kwani ni lazima watu wapongezane kwa kukusanyika uwanjani, wangeweza kufanya hata hotelini au ukumbini mahali," alisema.
Bw. Mtweve aliongeza kusema kuwa haikuwa vizuri baada ya uchaguzi kuruhusu maandamano na mikutano ya hadhara kwani nchi ilikuwa imetoka katika uchaguzi, huku 'mambo yakiwa hayajakaa sawa', serikali ikiwa haijaundwa na mawaziri hawajateuliwa.
Majira lilipotaka kujua kama jeshi hilo lilikuwa na wasiwasi zaidi na maandamano na mapokezi ya wabunge kwa nini lilizuia hata mikutano ya hadhara kama vile huko Segerea, Dar es Salaam, Bw. Mtweve alisema kuwa hiyo ilikuwa ni kwa mujibu wa "operetion order" (amri ya utendaji).
Alisisitiza kuwa kuanzia jana utaratibu wa kuomba na kukubaliwa mikutano ya hadhara na maandamano unarudi kama kawaida chini ya makamanda wa polisi wa wilaya.
Wakati huo huo, CHADEMA kimepongeza hatua ya kuondoa amri hiyo na kusema kuwa ni jambo zuri lakini halizuii kusudio lake la kufikisha hoja yake bungeni juu ya uvunjifu wa Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga ya Bunge ya mwaka 1988, kikisema kuwa polisi hawana ruhusa ya kuzuia mikutano ya wabunge "pale serikali inapokuwa haipo."
Akipongeza hatua hiyo, Mkurugenzi wa Haki, Sheria na Katiba wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu alisema "Kama wameiondoa basi ni jambo zuri sana...ni kitendo kizuri lakini hakituzuii kwenda kuhoji bungeni kwa nini wabunge wetu walizuia kufanya kazi...kufanya mikutano.
"Hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kuvunja au kukiuka sheria ya haki, mamlaka na kinga ya bunge ikiwa serikali haipo au mawaziri hawajateuliwa," alisema Bw. Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni
Chanzo ni Gazeti la Majira la tarehe 30/11/2010 GAZETI HURU LA KILA SIKU:
My take:
1. Kwa nini kizuizi kuondolewa siku moja baada ya Lisu na Chadema kutoa tamko?
2. Je linahitajika somo kwa polisi kuhusu vifungu vya katiba?
3. Hiyo mamlaka ya juu Mtweve anayotaja niipi?
4. Kama Mwema alizuia kwa kuongea na media, kwa nini jana anamtuma mkurugenzi wa fedha?
There are more questions than answers!