Siyabonga101
JF-Expert Member
- Mar 8, 2016
- 2,424
- 2,297
Ila hili suala la kukosa mdhamini limenisikitisha sana. Hata Mwanasheria wake msomi bwana Petro E. Mselewa ameingia mitini!? Ama kweli mashokolo mageni.
Hahaha kumbe mwanasheria msomi Petro alikuwa anamuwakilisha Dr shika mkuuIla hili suala la kukosa mdhamini limenisikitisha sana. Hata Mwanasheria wake msomi bwana Petro E. Mselewa ameingia mitini!? Ama kweli mashokolo mageni.
Kamanda Mambosasa amesema ameagiza Dk Shika ajidhamini na awe anaripoti polisi
Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema limefikia uamuzi wa kumtaka Dk Louis Shika ‘bilionea wa nyumba za Lugumi’ ajidhamini yeye mwenyewe baada ya kukosa mtu yeyote aliyejitokeza kwenda kutaka kumwekea dhamana.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Novemba 14, Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema “uchunguzi wa tuhuma dhidi yake unaendelea lakini mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyefika kutaka kumwekea dhamana, yaani anaishi kama mtu wa nyikani.”
Mambosasa ameongeza, “nimeagiza watendaji wangu wamwachie kwa dhamana yaani ajidhamini yeye mwenyewe na awe anakuja kuripoti,” amesema Mambosasa
Kamanda huyo ametoa kauli hiyo mara baada ya Mwananchi kumtafuta kutaka kujua hatima ya Dk Shika ambaye ameshikiliwa tangu Novemba 9 akituhumiwa kuvuruga mnada wa nyumba za kifahari za mfanyabishara Said Lugumi
Dk Shika tangu siku hiyo amekuwa gumzo sehemu mbalimbali kutokana na kile alichokifanya siku ya mnada alipokuwa akipandisha bei dhidi ya washindani wake na moja ya kauli zake zinaendelea kutumika hadi sasa ni ‘Mia 900 itapendeza.’
Chanzo: Mwananchi
=====
UPDATES: Dr Shika ameachiwa baada ya kujidhamini mwenyewe
Tehe tehe! Ndio Mwanasheria wake mkuu huyo kamanda. Hahaha!Hahaha kumbe mwanasheria msomi Petro alikuwa anamuwakilisha Dr shika mkuu
Ova
njia za MUNGU hazitambuliki na wanadamu inawezekana hii ndio ikawa fursa yake ya kufanikiwa kimaisha.Unaweza ukacheka sana lakini kwa upande mwingine inasikitisha sana, inakuwaje mtu anaishi bila ndugu wala jamaa, atakuwa na maisha magumu sana huyu jamaa... So sad
900 itapendeza Mkuu.Wazo zuri, naweka 800