Polisi Wilayani Geita watuhumiwa kuhusika na mauaji ya kijana aliyekuwa mlizi wa kampuni ya Jerusalemu Security Ltd

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Jeshi la Polisi Wilayani Geita mkoani humo linatuhumiwa kuhusika na mauaji ya kijana aliyekuwa mlizi wa kampuni ya Jerusalemu Security Ltd. ambaye ni mkazi wa mtaa wa Mwatulole kata ya Buhalahala Mjini Geita anayedaiwa kufariki dunia katika mazingira ya kutatanisha.

Kifo cha kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Baraka Vitalis mwenye umri wa miaka 23 kimetokea wakati ndugu na kaka yake wakihaha kumtafuta katika kituo cha polisi, ambapo imeelezwa kabla ya uamuti marehemu alikamatwa Novemba 8 2018 majira ya saa 12 jioni katika eneo la nyumbani kwake na kupelekwa kituo cha Polisi Geita kwa tuhuma za wizi baada ya kutajwa na wenzake 10 wanaoshikiliwa na jeshi hilo ambapo majira ya saa tatu usiku alifikishwa katika hospitali ya rufaa akiwa amefariki.

Polisi Mkoani humo imekiri kutokea kwa kifo cha Baraka lakini imesema mpaka sasa inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha kifo.

 
Kazi ya polisi imebadilika baada ya kulinda raia sasa imekuwa kuua raia?.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Hawa ni wale wanaosadiki matamko ya mh. Kangi Lugola kuwa ni siasa tu.

Mh. Kangi tembelea hawa kama wale wa Kigoma. Yaonesha bado hujaeleweka mkuu.
 
Niliwakuta hao ndugu wa huyo jamaa kituo cha polisi, wanasema kuna polisi walikuwa wanagombea demu na huyo mshikaji, demu akawa anamkubali mshikaji zaidi kuliko huyo polisi SASA bifu likaanzia hapo, nasikia kuna siku mkono ulipigwa huyo Askari akachezea Sana wakaahidi kumfanyizia kitu mbaya mshkaji matokeo yake ndio hayo sasa!
 
Back
Top Bottom