Polisi wavamia nyumba kwa aliyemuweka Ndugu yake rehani huko Pakistan

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,490
54,884
image-1-559x520.png

Aliyemuweka Ndugu yake rehani adaiwa kuwa na utajiri wa ‘Kutupwa’, Polisi wavamia nyumba yake, wamempata??
Adamu ambaye ni mkazi wa Magomeni Mtaa wa Chemchem na Idirsa, inasemekana aliwekwa rehani kwa ghamara ya Dola za Marekani 700, 000, sawa na zaidi ya Sh bilioni 1.5 za Tanzania.

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa ndugu wa karibu wa Mtanzania huyo zinasema kuwa, Adamu aliwekwa rehani na kaka yake huyo akitakiwa kulipa fedha za unga (mihadarati) aliochukua.

“Aliyesababisha yote hayo ni Adamu kwa sababu ndiye aliyekwenda naye Pakistani kwa kisingizio kwamba fedha zinapatikana kwa urahisi huko,” alisema ndugu huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Wakati hayo yakiendelea, jana usiku askari polisi walivamia nyumba ya Juma Neti kwa ajili ya kumkamata kwa tuhuma za kuuza dawa za kulevya.

Nyumba hiyo ambayo ipo Kunduchi, maeneo ya Ununio, Manispaa ya Kinondoni, ilivamiwa na askari hao baada ya gazeti hili kuanza kuripoti uwepo wa Mtanzania nchini Pakistani anayeshikiliwa na kundi hilo la maharamia.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime, alipopigiwa simu kuzungumzia tukio hilo hakupokea na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa maneno, hakuujibu.

Pamoja na Neti kutaka kukamatwa jana, taarifa zinasema polisi wamekuwa wakimtafuta kwa muda mrefu kutokana na tabia yake ya kujihusisha na biashara hiyo bila mafanikio.

Taarifa zaidi zinasema kwamba, Neti amekuwa na utajiri wa kutisha kwa kuwa miaka michache iliyopita, alikuwa na maisha ya kaiwada ingawa sasa anaonekana kuwa miongoni mwa Watanzania wenye ukwasi mkubwa.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, hivi karibuni Neti aliingia ubia na kampuni moja ya Kenya baada ya kuwekeza Dola za Marekani 400,000, sawa na zaidi ya Sh milioni 800 za Tanzania.
 
Back
Top Bottom