Polisi waumbuka kwa kifo cha Mwangosi ushahidi ni huu.

Unanikumbusha vituko vya majuu ambavyo huwa ndugu yetu Mchambuzi anatuwekea humu JF. Haya ya polisi wetu pia yanafanana kwa karibu sana.
 
Mkumbuke kuwa kesho huenda serikali ikafunga mijadala yote juu ya mauaji haya kwa kuwafikisha mahakamani fasta fasta watuhumiwa wowote watakao"teuliwa" na jeshi la Polisi pengine bila kupanga vizuri mashtaka ili jambo hili lionekane liko mahakamani hivyo halijadiliki tena.

Ni bora mwenye habari inayoweza kuufikia umma ili ukweli uwe wazi aitoe katika vyombo ya habari leo na kesho asubuhi tu kabla mjadala haujafungwa
 
Polisi si wa kutetewa, bali ni wa kushitakiwa..........tujifunzeni kwa aliyekuwa Police Boss wa South Africa, Jack Selebi
Yaliyomkuta si haba hivyo hatuna haja ya The Hague kama Rais atafanya maamuzi magumu ya kuwasimamisha kazi mara moja na kuwapandisha kwa pilato. Ila kwa udhaifu wa Rais wetu, a.k.a Mwenyekiti hawezi sema lolote atakaa kimya kama alivyozoea........
Hivi Mh. Rais JM Kikwete, katika safari zako zote ulizoenda kwa nini usitembelee Liberia kwa mama Sirleaf, Ellen-Johnson kujifunza somo la jinsi ya kufanya maamuzi magumu hata kwa mwanao Riz1? Kule kutotaja mali zako unafutwa na kukabidhiwa kwa TAKUKURU ya huko. Kwa nini mwanamke ajizolee sifa za hata kumfuta kazi mwanae kwa kushindwa kuwajibika halafu wewe ushindwe kumfuta kazi Nchimbi,(WAZIRI WAKO WA MAMBO YA NDANI) Mwema,(IGP) na Kamuhanda?(RPC-IRINGA)? "Kwanini Moyo wako Rais wangu uwe Mgumu kama wa Pharao"? Kwani kuwafuta kazi inachukua wiki ngapi? Huna watu wengine wanaoweza kuziba pengo lao?

Jamani nawasilisha hii kwa uchungu sana, mtoto wa mwenzako kageuzwa "rundo la nyama kwa kupigwa bomu", hapo kuna haja gani ya tume au kamati ya uchunguzi? Uchunguzi wa nini hapo?

Kikwete, moyo wangu ulikuamini sana ulipokuwa waziri wa mambo ya ndani, haswa siku ile ya upatanishi wa Warundi (1998) AICC Arusha, na jinsi ulivyotii maagizo ya mwalimu JK Nyerere pale "parking"Jinsi pia ulivyonitambulisha kwa Aliyekuwa rais wa Zambia (RIP Fredrick J.T.Chiluba)kwa kumwambia mimi ni kijana mzuri na mtendaji? Mh. Kumbuka vizuri ulipowapanga media ni jinsi gani wamuhoji Mzee N.R Mandela na leo mmoja kati ya hao waandishi kauawa na wewe umekaa kimya? Sikuamini kama siku moja ungebadilika. Yako wapi yale ma-uwajibikaji ya kupanga magari ya serikali uliyokuwa unayafanya? Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba yeyote kutoka secretarieti ya utumishi wa umma anijibu maswali yangu haya humuhumu JF kama hadharani au katika vyombo vya habari italeta mzozo.

Kweli sasa naamini ule usemi usemao "kua uyaone'
 
Watadanganya ulimwengu, Ila wajue tu Mungu hadanganyiki.........
 
Zamani ilikuwa chama kinashika hatamu,hivyo nakumbuka watu walikuwa wanaimba'naapa naahidi mbele ya chama,mapinduzi nitakulinda mpaka kufa'.sasa mapinduzi hayaepukiki'social revolution is a must'.cortide tunga wimbo huu'naapa naahidi mbele ya chadema mafisadi nitawapinga mpaka kufa'.
 
Zamani ilikuwa chama kinashika hatamu,hivyo nakumbuka watu walikuwa wanaimba'naapa naahidi mbele ya chama,mapinduzi nitakulinda mpaka kufa'.sasa mapinduzi hayaepukiki'social revolution is a must'.cortide tunga wimbo huu'naapa naahidi mbele ya chadema mafisadi nitawapinga mpaka kufa'.
 
Amri inatoka kwa hawa:
attachment.php

attachment.php
 
Nawalaaniwe wote walioshiriki kutekeleza unyama huu. Tukio hili linadhihirisha wazi pia kwamba; baadhi ya Polisi wanatumia sigara kubwa. Hivi hata kama ni kutekeleza amri za wakubwa ndiyo hata kwa ukatili wa aina hii? Binadamu aliyetekeleza haya dhidi ya binadamu mwenzake unaweza kuamini kama akili yake iko sawa sawa? Kingine ni kwamba, binafsi nina wasiwasi na askari polisi wengi kama kweli wana mafunzo sahihi ya kulinda usalama wa raia na mali zao. Kwa nini katika miaka ya karibuni Polisi wanahusika sana katika mauaji ya kikatili dhidi ya raia wasio na hatia? Je, ni baada ya kuona CDM inakuja juu ikipiga jalamba kuchukua nafasi 2015, hivyo wanaagizwa kuchafua hali ya hewa ili watu wakichukie chama hiki makini? Je, ni kutokana na kwamba Polisi wa sasa wanaajiliwa kutoka JKT hivyo wana mafunzo ya kijeshi zaidi (kumwahi adui kabla hajakuwahi), badala ya kuwa na mafunzo ya kipolisi (kulinda usalama wa raia na mali zao) ikiwa ni pamoja na ku-balance jinsi ya kutumia nguvu pale inapobidi?. Binafsi natamani kuona wahusika wote wanatiwa kitanzi.
 
napingana na wewe , ubinadamu hautegemei elimu yako. kwani kuna watanzania wangapi hawajasoma kabisa na hawana matendo maovu kama ya polisi hawa?. tatizo si la askari wanaopigana mbele, si elimu yao au ubora wa vyeti vyao ni tatizo la dola nzima, ni tatizo la kisheria, nitatizo la maadili ya kazi, ni tatizo la mfumo. ni tatizo lako, ni tatizo langu. amka sasa, niamke sasa, tukeshe tukitafuta iliyo haki kwetu na
kwa vizazi vijavyo

I like ur comments. viongozi wetu wamejifanya hawaoni. hii inonesha wako tayari kwa lolote. any way hatahivyo walishasema 'liwalo na liwe '
 
Maneno ya baba wa Taifa,

TUMEONEWA kiasi cha kutosha,
TUMENYONYWA kiasi cha kutosha,
TUMEPUUZWA kiasi cha kutosha,
Sasa tunataka MAPINDUZI,
Ili TUSIONEWE tena,
TUSINYONYWE tena,
Na TUSIPUUZWE tena!

Alipoyasema hayo alikuwa anaifikiria Tanzania ya wakati ule. Picha aliyokuwa nayo ni kuwa watanzania kamwe hawataonewa, kunyonywa wala kupuuzwa. Alikuwa na matumaini kuwa misingi aliyotuwekea watanzania tutaienzi na kuendeleza mazuri yote aliyoyaacha. Kumbe waliokuwa wanalia sana kaburini ndiyo wachawi wetu. Wamegeuka manyang'au. Sio tu wanatuonea, wanatunyonya na kutupuuza, sasa WANATUUA! Hatuna lingine lililobaki ila ni kuleta MAPINDUZI ya kweli! Tukiamua tunaweza, tuko milioni 45 na ushee, wao wako wangapi? Tukianzia na hao polisi walioyafanya haya, wako wangapi hata watutishe watanzania wote? Hata askari wote wa polisi (na ninaamini sio wote wanaokubaliana na udhalimu huu) wakitoka kupamabana na watanzania. Silaha zao zote wazikusanye hawatatuweza!

Pumzika kwa Amani Daudi Mwangosi.
Damu yako haitapotea bure.
Dunia imeona na imesikia.
Mungu Wetu Aliye Hai Ameona!
 
Hilo ndilo Jeshi la Polisi, unategema nini wakati wengi wao ni form four leavers au wakiwa miongoni mwa waliofoji vyeti vyao hata hivyo vya kidato cha nne? Unategemea haki na utaalamu wa policing the mass kwa ileterate kama hao with guns and license to kill? Unategemea nini kutoka kwa Jeshi la Polisi lisilo na ethics za kazi na hata training zao zenyewe ni za kuteswa teswa? Lijuse Jeshi la Polisi Tanzania, lililojaa uonevu, lililokosa heshima na lililopoteza utaratibu yakinifu wa kulinda amani na heshima ya mwananchi. Tanzania ilikurupuka kujiweka katika mfumo wa vyama vingi huku vyombo muhimu kama muhimili wa mageuzi hayo yakiachwa bila ya reform sahihi, justice department na vikosi vya ulinzi.

Halafu Nape athubutu kuwalaumu upinzani kwa kutekeleza misingi ya kazi zao, ni adui wa misingi ya demokrasia na tusipoangalia ndio watakaokuja kuitia nchi katika mauaji ya wenyewe kwa wenyewe. Taasisi za kiraia zinazoshuhulika na masuala ya sheria ni byema kukusanya ushahidi wote kamili yakiwemo majina ya wakuu wanaotoa amri kama hizi ili waje kusimama mbele ya mahakama kujibu shutuma za mauaji.

Mdhalimu wa roho ya binaadamu daima ataishi kwa kutegemea maguvu ya kuwadhalilisha wengine wanasahau duniani hapa tunapita tu, iko siku tutarejea kwa hakimu wa haki. Lala pema mwanademokrasia wa kweli. Kifo chako kamwe hakitasahaulika.
 
kisiwa cha amani!!!!!!????????hawa Machinja chinja hata kama hawatachukuliana hatua(maana ni wao kwa wao) Mungu aliye hai atawachukulia hatua,tuliyaona ya akina mzee Dito leo wako wapi? wakaja akina zombe leo wako wapi? udhalimu huu haukuwahi kufanywa hata na askari wa mkoloni.
 
Hili ndilo jeshi letu linaloitwa jeshi la kutulinda sisi raia na mali zetu. Linatulinda vipi kama hali ndiyo hii ya kuondoa roho zetu?

Ni ukweli usiopingika kuwa wanatumwa kutekeleza madhira haya kwa maslahi ya wakubwa wao. Lakini kwa nini wasifanye kazi yao kwa mujibu wa utaalamu wao waliofundishwa vyuoni kwao?

Yana mwisho!
 
polisi wetu wengi wao ni failures masomoni nndo tatizo lao

.........Nani asiyejua kuwa baba Rz ni kilaza kama vingne? mitihani yake yote alidesa na hatimae kutona na Gentlemen..... cheza na GPA 2.0 weye? unatarajia awe na uweza wa kufanya maamuzi magumu? acha bana!
 



Asanteni Kamati Kuu CHADEMA walau kwa kuitikia sauti ya na majonzi ya umma wa Tanzania na kutoa dira kwa Taifa, kukemea na kuainisha mambo gani yafanyike ili kutokomesha UKATILI WA JESHI LA POLISI dhidi ya raia na mauaji yasiokwisha kila kona ya nchi.

Hakika bado tunaomba sana mambo yasiishie tu hapo kwenye ma-tamko bali zaidi wananchi tunaasubiri kuona CHADEMA kinavyofwatilia utekelezaji wa kila agizo la Kamati Kuu taifa kwa faida yetu sisi walalahoi huku vijijini.

Elimu ya uraia kwa umma wa Tanzania sasa ndio iongezewe kasi maraduru ili kila kijiji kiweze kufikiwa ki-undani zaidi na zaidi.

KOVU LA UKATILI WA JESHI LA POLISI DHIDI YA RAIA NCHINI:
WATANZANIA TUNAJIBU GANI KWA 'MACHOZI YA LAANA NA KILIO CHA HAKI YA MWANAMAMA WINFRIDA JOHN' WA KIJIJI CHA NYOLOLO MKOANI IRINGA ???


Kamanda Winfrida John, kada wa CHADEMA kijiji cha Nyololo, bila shaka wewe ni mwana mama mtu mdogo tu hapo kijijini Nyololo ambaye pengine hata mbunge wa eneo hilo huenda asikufahamu kitu achilia mbali wakuu wa wilaya na mkoa huko Mufindi na Iringa kwa mpangilio huo, ila kwa wachache sana tena wenye jicho la mwewe angani huenda lako hili la kipekee mno likawa limewagusa nao pia.

Naam, kabla sijaandika mengi juu yako na kile kilichonigusa mno kwako kwanza niombe kwamba tafadhali Mama Winfrida futa machozi yako, yale ya akinamama wengine wengi zaidi hapo Nyololo na kwamba katu usiendelee kutuhuzunisha zaidi sisi WaTanzania wenzako kwa uchungu wote huo; machozi yako hadharani ya KULILIA HAKI na kutuhoji sote kama taifa tukupe jibu UHURU WAKO WA MAONI, NA KUJUMUIKA ulikopotelea;

Ni kweli kwamba siku hiyo 'SIMBA MLA WANYONGE WANAAOLILIA HAAKI' alipomnyakua makuchani Mtanzania wa 22 (Daudi Mwangosi) afiaye mikononi mwa dola kwa visingizio mbalimbali za kisiasa tangu mwaka huu, bila shaka watu wengi tu hapo Nyololo, Itete na hata vijiji vingine vya mbali sana nao walilia ila wewe hapo chozi laako linageuka kuwa chozi la dhahabu si kwa kuwa tu ulikua kwenye eneo la tukio baali zaidi ni kwamba ni mmoja kati ya wenyeji waliotembelewa naa CHAADEMA kwa shughuli ya ufunguzi wa ofisi mahali haapo.

Hakika ni kutokana na udhahabu huo wa chozi lako tena ukiwaa ni mwanamama tu mnaohitajika kuimarishwa zaidi kushiriki katika siasa na uongozi wa taifa, inanifanya nisiamini tu kwamba hivi karibuni huenda ukawa ni mtu wa kutafutwa sana japo sauti na vyombo vingi vya nyumbani hapa na vile vya kimataifa kama vile BBC, VoA, Deuche Welle ...

... bali zaidi najikutaa pia nikiwa sina wasi wasi kwamba Mama Hellen Kijo Bisimba naye amekusikia popote alipo, naamini kwamba msururu wako wa maswali ya msingi sana uliyoyauliza siku hii hata Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani umemuacha hana amani moyoni;

Ndio, kwa mtaji w kilio chako kikiwakilicha KILIO CHA HAKI kwetu sisi WaTanzania kwa ujumla wetu bila shaka ni wazi kwamba tayari umetuma ujumbe mzito kiasi cha kuwalazimisha hata magwiji wa habari nchiki akina Mzee Jenerali Ulimwengu, Fred Masako, Mzee Mwanakijiji, pamoja na Pasco wa JF.

Nasema kwa kilio cha mwanamama 'kiumbe dhaifu' katika jamii yetu hii inayoendekeza ufalme wa akina-baba tu kwamba vile vile utakua umewakuna akina Mama Nkya, Ayub Ryoba, Muhingo Rweyemamu pamoja na wengine kibao, waondoke kwenye viyoyozi maofisini na kuanza kupiga kiguu na njia wao wenyewe bila kumuagiza mwandishi yeyote wa chini, kwenda kukutafutia majibu sahihi na murua zaidi kiasi cha kuweza kukufuta machozi wewe na vizazi vijavyo;

Mama Winifrida, kwa kilio hiki hapo kijijini Nyololo ni wazi kwamba tayari umewakilisha sauti dhaifu za akina mama wote na watoto Tanzania ambao kweli
siku Daudi Mwangosi alipogeuka RUNDO LA NYAMA hapo kijijini kwenu(kwa hisani ya maagizo ya serikali ya CCM) - wenzetu mmeonekana kuteseka mno kukimbia ovyo na vichanga kuokoa maisha huku mkidhalilishwa na mgeni wenu CHADEMA ambaye ndiye kwanza mlikua mnamkaribisha rasmi hapo kijijini kwenu kwa kumpa eneo akafungulie ofisi yake (kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi) lakini ukarimu wenu wote ukahitimishwa na kilio cha historia yote Nyololo kugeuka ghafla kuwa uwanja wa mauji kama Syria.

Naam, nielewavyo mimi ni kwamba mama yetu Winfrida, hadi hapo ni kwamba tayari umewaamrisha wanaharakati kama Kijana mwenzetu Kibodya, Tundu Lissu, Deus Mallya, Prof Shivji, John Tendwa, pamoja na Mhe Augustino Mrema.

Wengine zaidi ambao wapende wasipende machozi yako ya haki bila shaka yako mabegani mwao ni pamoja na Prof Palamagamba Kabudi, Madam Spika wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Mama Makinda, Prof Safari, Prof Maina, Prof Baregu, Dr Kitila Mkumbo, Dr Azaveli.

Ndio, nasema hawa waheshimiwa wote wanao wajibu kwako usiokwepeka kutoa jawabu kamili tena lisilocha maswali, kila mmoja kwa wakati wake, wakwambie kwamba kwenye katiba mpya wao wanategemea kuona Jeshi la Polisi la aina gani ili Winfrida John wa miaka hiyo ijayo wao wasije wakajikuta wakilia kilio kile kile kilichokumuaga machozi hapo Nyololo.

WaTanznia wote bila kujali itikadi za kidini na kisiasa, je tunalo jibu gani kwa mama huyu Winfrida John wa kijiji cha Nyololo ikiwa ni kielelezo cha kilio cha akina mama wengine wengi zaidi wasiokua na majina katika jamii yetu hii wangali nao wanao wachozi yasiokauka kulilia haki kama vile kule Igunga, Arumeru Mashariki, mauji ya Pemba, Arusha, Tarime, Mbeya ...?


 
Last edited by a moderator:
Hakika kuna nafsi inaongea ndani yao na iko siku tutaamka na kusikia Police wameandamana dhidi ya amri ya kuua bila hatia wala njama mbaya.
 
Hata polisi nao ni watoto wa walalahoi tunaodhalilishwa kimaisha na vitendo vya MAFISADI wanaofilisi nchi.

Hakika kuna nafsi inaongea ndani yao na iko siku tutaamka na kusikia Police wameandamana dhidi ya amri ya kuua bila hatia wala njama mbaya.
 
ifike wakati wananchi wasikubali, wacheza karateka wapo chungu nzima mitaani CDM chukueni hao, wakija hawa maaskari wanaotumwa mnawapa vichapo vya kueleweka kabla hawajawafanyia wananchi ukatili kama huu.
 
silaha za jadi zipo nyingi sana chupa, mawe maji ya moto na nyingine nyingi wao si wanataka vurugu, hapo wataelewa kuwa watu wamechoshwa na mambo haya ya uonevu.
 
Back
Top Bottom