Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,778
Polisi watuhumiwa kuwa majambazi
Arusha: Mmoja atoroka na bunduki, alihusika katika ujambazi
Rukwa: Mmoja akamatwa kwa kukwapua pesa kwenye ATM
Mara: Mmoja akamatwa kwa kutorosha mhalifu mahabusu
Mwanza: Kisiwa Ukerewe wadaiwa kusaidia majambazi
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema.
[FONT=ArialMT, sans-serif]Jeshi la Polisi nchini limekumbwa na kashfa kubwa, kufuatia polisi wake kadhaa kutuhumiwa kuhusika katika mfululizo wa matukio ya uhalifu nchini.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kuhusishwa kwa polisi hao katika uhalifu kunalitia doa kubwa jeshi hilo hivyo kuonekana mbele ya umma kuwa limebadili lengo lake la kuwalinda raia na mali zao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la kwanza, askari wa polisi mkoani Arusha, Mvanga Balele (30), ametoroka na bunduki aina ya SMG, redio ya upepo mali ya jeshi hilo baada ya kudaiwa kuhusika katika tukio la unyanganyi wa kutumia silaha katika eneo la Njiro.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hali kadhalika jeshi hilo linamshikilia askari mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Frank pamoja na pikipiki ya askari aliyetoroka yenye namba T133BAB ambayo ndio ilitumika katika tukio hilo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Tukio hilo ambalo limethibitishwa na jeshi la polisi mkoani hapa lilitokea juzi katika eneo la Njiro baada ya watu watatu akiwemo askari huyo kuvamia katika duka la vifaa vya ujenzi la Kitonga, lakini kabla ya kutekeleza uhalifu huo walizingirwa na polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio hilo mtuhumiwa mwingine wa ujambazi, Hilary Kibauli (24), aliuawa na polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo baada ya majambazi hayo kuzidiwa nguvu na askari sita wa doria walianguka katika mtaro na mmoja alifanikiwa kutoroka na Kibauli alipohojiwa aliwataja wenzake wakiwemno hao wawili.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Basilio Matei, alisema kuwa askari huyo alitoroka pamoja na familia yake muda mfupi baada ya tukio hilo na kwamba hajuliakani alipo mpaka sasa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Askari huyo alitoroka na tulituma vijana kufanya upekuzi na walifanikiwa kukuta vifaa vya kujibadlisha sura nyumbani kwake na tunaendelea kumsaka kwani tukio hili limefedhehesha jeshi, ni aibu kubwa, alisema Matei.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha Kamanda Matei alisema kuwa Kibauli ambaye alifariki dunia juzi jioni ndiye aliwataja askari hao kujihusisha na mtandao wa ujambazi wa kutumia silaha mkoani hapa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Matei alifafanua kuwa askari huyo alitakuwa katika lindo eneo la Njiro siku ya tukio, lakini uchunguzi ulionyesha kuwa hakufika eneo la ulinzi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alifafanua kuwa siku ya tukio, jeshi hilo lilipata taarifa za siri kuwa kuna majambazi ambayo yalipanga kufanya uhalifu na walianza kuwafuatiliwa na kufanikiwa kuwazingira kabla ya kuteleleza uhalifu wao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Baada ya kuzingirwa na mapambano kuwa makali mmoja alipigwa risasi, lakini yule aliyekuwa na SMG alifanikiwa kutoroka na baadaye kuteka gari la wanafunzi na kuwashusha na kuliendesha na baadaye kulitelekeza katika eneo la Kimandolu, alisema Matei.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alidai kuwa katika mapambanao hayo askari walifanikiwa kumpiga Kibauli risasi kiunoni na kunguka chini ambapo alipiga kelele akiomba asiuawe kwani ana mambo mengi makubwa ya kujulisha polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Basilio alisema kuwa jambazi huyo alianza kuwataja askari wanaojihusisha na ujambazi, lakini baadaye alifariki baada ya kuvuja damu nyingi. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kufuatia tukio hilo, kamanda huyo aliwataka watu wanaowafahamu askari wanaojihusisha na ujambazi kutoa taarifa za siri ili kutokomeza vitendo hivyo katika jeshi. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aibu hii ikiuukumba mkoa wa Arusha, mkoani Mwanza nako polisi imepakwa matope baada ya wananchi kudai kwamba katika tukio la mauaji ya raia 14 wilayani Ukerewe yaliyofanywa na majambazi wiki iliyopita, miongoni mwao kulikuwa na askari polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Wananchi waliishiwa uvumilivu na kumtaka Mkurugezi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) wa Polisi, Robert Manumba, aondoke na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ukerewe kwa madai kwamba amekuwa ni sehemu ya kulinda uhalifu wa polisi dhidi ya raia.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la tatu, Polisi mkoani Rukwa inamshikilia askari mwenye namba F 5767 Michael Mangi wa kituo cha polisi Namanyere kilichopo katika wilaya ya Nkasi kwa tuhuma za kuiba zaidi ya Sh. milioni moja za mteja kupitia mashine za kuchukulia fedha 'ATM' ya benki ya NMB tawi la Namanyere.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage, alisema mtuhiwa huyo aliiba kiasi cha Sh. 1,063,000.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Mantage alimtaja mteja huyo aliyegundua kuibiwa fedha zake ni Kasesaunga Joseph (50), mkazi wa kitongoji cha Ipanda kilichopo katika Wilaya ya Nkasi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema mwananchi huyo aligundua kupungua kwa fedha zake Januari 16, mwaka huu, baada ya kufika katika benki hiyo kwa lengo la kuchukua fedha kununulia bati za kuendeleza ujenzi wa nyumba yake.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kwa mujibu wa kamanda huyo, baada ya tukio hilo mwananchi huyo alitoa taarifa kwa uongozi wa benki hiyo na maafisa wa benki walibaini kuwa feha hizo zilichukuliwa kwa vipindi tofauti na kuhamishiwa katika akaunti mbili tofauti.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mantage alisema baada ya ugunduzi huo, uongozi wa benki ulitoa taarifa katika kituo cha polisi Namanyere ambapo wamiliki wa akaunti hizo mbili zilizohamishiwa fedha walikamatwa na kwamba katika mahojiano kila mmoja alikiri kuhamishiwa fedha katika akaunti yake na askari huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema watu hao walilieleza polisi kuwa walikuwa wakidanganywa na askari huyo kuwa yeye ana akaunti NMB na kwamba aliwaomba akaunti zao ili ndugu zake wamtumie fedha kupitia akaunti zao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwataja watu waliohamishiwa fedha za wizi na askari huyo kuwa ni Martin Magesa (25) ambaye alihamishiwa kiasi cha Sh. 500,000 na Geoffrey Sinkala (26), aliyehamishiwa Sh. 350,000 na kwamba walizichukua fedha hizo na kumkabidhi askari huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Mantage alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa fedha nyingine alikuwa akichukua kama muda wa maogenzi na kuhamishia katika simu yake ya mkononi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hata hivyo uchunguzi huo umebaini kuwa askari huyo alipata namba za siri ya kadi ya ATM za mwananchi huyo siku chache zilizopita baada ya mwananhi huyo kufika katika benki hiyo na kumkuta askari huyo akiwa lindo na kumuomba amfundishe namna ya kutumia kadi ya ATM.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamamda Mantage alisema kuwa askari huyo amehojiwa na kukiri kutenda kosa hilo na anaendelea na mashitaka ya kijeshi na akipatikana na hatia ataadhibiwa kijeshi na kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la nne, Jeshi la Polisi mkoani Mara limemfikisha katika mahakama ya kijeshi askari wake, Koplo John kujibu tuhuma za kula njama na kumtorosha mmoja wa watuhumiwa watano wa ujambazi na mauaji ya watu watatu yaliyotokea wilayani Bunda wiki iliyopita.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Robert Boaz , alisema Koplo John alifikishwa katika mahakama hiyo jana na kusomewa tuhuma za kumtorosha mtuhumiwa huyo, Mwanzi Nyamsenda (30), mkazi wa Bunda wakati akiwa katika mahabusu ya kituo hicho baada ya kukamatwa na wenzake wanne kwa tuhuma hizo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Boaz alisema ikithibitika kuwa amemtorosha mtuhumiwa huyo, atafukuzwa katika Jeshi la Polisi na kufikishwa katika mahakama ya kiraia.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Boaz alisema Koplo John ni miongoni mwa askari sita waliokuwa zamu siku ambayo mtuhumiwa huyo inadaiwa alitoroshwa kutoka mahabusu.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwataja askari wengine kuwa Koplo Michael, WP Luciana, PC Arico, PC Kozi na Sajenti Sospeter.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema Koplo John alifikisha katika mahakama hiyo baada ya kudaiwa kuthibitika kuwa ndiye aliyemtorosha mtuhumiwa huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Juzi Kamanda Boaz alisema kutoroka kwa mtuhumiwa huyo kunazua maswali mengi kwa sababu mlango wa mahabusu haukuvunjwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Tutatoa taarifa wakati wowote maana mlango haukuvunjwa, lazima tuone mazingira ya kutoroka kwa mtuhumiwa yalikuwaje, alisema Boaz.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Januari 16, mwaka huu majira ya saa 8:00 usiku, kundi la watu wanaoshukiwa kuwa majambazi wakiwa na bunduki yalivamia maduka matatu katika mji mdogo wa Kibara na kuwaua walinzi wawili na kujeruhi mwingine kwa kuwapiga na vitu kizito vichwani na mtu mwingine Kijiji cha Mugara.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, jana hakuweza kutoa ufafanuzi kuhusiana na matukio hayo ya polisi kuhusika katika matukio kadhaa ya ujambazi, baada ya kuieleza Nipashe kuwa alikuwa na mfululizo wa vikao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Imeandikwa na Wilbroad Tungaraza, Bunda, Juddy Ngonyani, Rukwa na Charles Ole Ngereza, Arusha.[/FONT]
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema.
[FONT=ArialMT, sans-serif]Jeshi la Polisi nchini limekumbwa na kashfa kubwa, kufuatia polisi wake kadhaa kutuhumiwa kuhusika katika mfululizo wa matukio ya uhalifu nchini.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kuhusishwa kwa polisi hao katika uhalifu kunalitia doa kubwa jeshi hilo hivyo kuonekana mbele ya umma kuwa limebadili lengo lake la kuwalinda raia na mali zao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la kwanza, askari wa polisi mkoani Arusha, Mvanga Balele (30), ametoroka na bunduki aina ya SMG, redio ya upepo mali ya jeshi hilo baada ya kudaiwa kuhusika katika tukio la unyanganyi wa kutumia silaha katika eneo la Njiro.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hali kadhalika jeshi hilo linamshikilia askari mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Frank pamoja na pikipiki ya askari aliyetoroka yenye namba T133BAB ambayo ndio ilitumika katika tukio hilo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Tukio hilo ambalo limethibitishwa na jeshi la polisi mkoani hapa lilitokea juzi katika eneo la Njiro baada ya watu watatu akiwemo askari huyo kuvamia katika duka la vifaa vya ujenzi la Kitonga, lakini kabla ya kutekeleza uhalifu huo walizingirwa na polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio hilo mtuhumiwa mwingine wa ujambazi, Hilary Kibauli (24), aliuawa na polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo baada ya majambazi hayo kuzidiwa nguvu na askari sita wa doria walianguka katika mtaro na mmoja alifanikiwa kutoroka na Kibauli alipohojiwa aliwataja wenzake wakiwemno hao wawili.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Basilio Matei, alisema kuwa askari huyo alitoroka pamoja na familia yake muda mfupi baada ya tukio hilo na kwamba hajuliakani alipo mpaka sasa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Askari huyo alitoroka na tulituma vijana kufanya upekuzi na walifanikiwa kukuta vifaa vya kujibadlisha sura nyumbani kwake na tunaendelea kumsaka kwani tukio hili limefedhehesha jeshi, ni aibu kubwa, alisema Matei.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha Kamanda Matei alisema kuwa Kibauli ambaye alifariki dunia juzi jioni ndiye aliwataja askari hao kujihusisha na mtandao wa ujambazi wa kutumia silaha mkoani hapa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Matei alifafanua kuwa askari huyo alitakuwa katika lindo eneo la Njiro siku ya tukio, lakini uchunguzi ulionyesha kuwa hakufika eneo la ulinzi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alifafanua kuwa siku ya tukio, jeshi hilo lilipata taarifa za siri kuwa kuna majambazi ambayo yalipanga kufanya uhalifu na walianza kuwafuatiliwa na kufanikiwa kuwazingira kabla ya kuteleleza uhalifu wao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Baada ya kuzingirwa na mapambano kuwa makali mmoja alipigwa risasi, lakini yule aliyekuwa na SMG alifanikiwa kutoroka na baadaye kuteka gari la wanafunzi na kuwashusha na kuliendesha na baadaye kulitelekeza katika eneo la Kimandolu, alisema Matei.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alidai kuwa katika mapambanao hayo askari walifanikiwa kumpiga Kibauli risasi kiunoni na kunguka chini ambapo alipiga kelele akiomba asiuawe kwani ana mambo mengi makubwa ya kujulisha polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Basilio alisema kuwa jambazi huyo alianza kuwataja askari wanaojihusisha na ujambazi, lakini baadaye alifariki baada ya kuvuja damu nyingi. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kufuatia tukio hilo, kamanda huyo aliwataka watu wanaowafahamu askari wanaojihusisha na ujambazi kutoa taarifa za siri ili kutokomeza vitendo hivyo katika jeshi. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aibu hii ikiuukumba mkoa wa Arusha, mkoani Mwanza nako polisi imepakwa matope baada ya wananchi kudai kwamba katika tukio la mauaji ya raia 14 wilayani Ukerewe yaliyofanywa na majambazi wiki iliyopita, miongoni mwao kulikuwa na askari polisi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Wananchi waliishiwa uvumilivu na kumtaka Mkurugezi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) wa Polisi, Robert Manumba, aondoke na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ukerewe kwa madai kwamba amekuwa ni sehemu ya kulinda uhalifu wa polisi dhidi ya raia.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la tatu, Polisi mkoani Rukwa inamshikilia askari mwenye namba F 5767 Michael Mangi wa kituo cha polisi Namanyere kilichopo katika wilaya ya Nkasi kwa tuhuma za kuiba zaidi ya Sh. milioni moja za mteja kupitia mashine za kuchukulia fedha 'ATM' ya benki ya NMB tawi la Namanyere.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage, alisema mtuhiwa huyo aliiba kiasi cha Sh. 1,063,000.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Mantage alimtaja mteja huyo aliyegundua kuibiwa fedha zake ni Kasesaunga Joseph (50), mkazi wa kitongoji cha Ipanda kilichopo katika Wilaya ya Nkasi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema mwananchi huyo aligundua kupungua kwa fedha zake Januari 16, mwaka huu, baada ya kufika katika benki hiyo kwa lengo la kuchukua fedha kununulia bati za kuendeleza ujenzi wa nyumba yake.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kwa mujibu wa kamanda huyo, baada ya tukio hilo mwananchi huyo alitoa taarifa kwa uongozi wa benki hiyo na maafisa wa benki walibaini kuwa feha hizo zilichukuliwa kwa vipindi tofauti na kuhamishiwa katika akaunti mbili tofauti.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mantage alisema baada ya ugunduzi huo, uongozi wa benki ulitoa taarifa katika kituo cha polisi Namanyere ambapo wamiliki wa akaunti hizo mbili zilizohamishiwa fedha walikamatwa na kwamba katika mahojiano kila mmoja alikiri kuhamishiwa fedha katika akaunti yake na askari huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema watu hao walilieleza polisi kuwa walikuwa wakidanganywa na askari huyo kuwa yeye ana akaunti NMB na kwamba aliwaomba akaunti zao ili ndugu zake wamtumie fedha kupitia akaunti zao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwataja watu waliohamishiwa fedha za wizi na askari huyo kuwa ni Martin Magesa (25) ambaye alihamishiwa kiasi cha Sh. 500,000 na Geoffrey Sinkala (26), aliyehamishiwa Sh. 350,000 na kwamba walizichukua fedha hizo na kumkabidhi askari huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda Mantage alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa fedha nyingine alikuwa akichukua kama muda wa maogenzi na kuhamishia katika simu yake ya mkononi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hata hivyo uchunguzi huo umebaini kuwa askari huyo alipata namba za siri ya kadi ya ATM za mwananchi huyo siku chache zilizopita baada ya mwananhi huyo kufika katika benki hiyo na kumkuta askari huyo akiwa lindo na kumuomba amfundishe namna ya kutumia kadi ya ATM.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamamda Mantage alisema kuwa askari huyo amehojiwa na kukiri kutenda kosa hilo na anaendelea na mashitaka ya kijeshi na akipatikana na hatia ataadhibiwa kijeshi na kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika tukio la nne, Jeshi la Polisi mkoani Mara limemfikisha katika mahakama ya kijeshi askari wake, Koplo John kujibu tuhuma za kula njama na kumtorosha mmoja wa watuhumiwa watano wa ujambazi na mauaji ya watu watatu yaliyotokea wilayani Bunda wiki iliyopita.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Robert Boaz , alisema Koplo John alifikishwa katika mahakama hiyo jana na kusomewa tuhuma za kumtorosha mtuhumiwa huyo, Mwanzi Nyamsenda (30), mkazi wa Bunda wakati akiwa katika mahabusu ya kituo hicho baada ya kukamatwa na wenzake wanne kwa tuhuma hizo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Boaz alisema ikithibitika kuwa amemtorosha mtuhumiwa huyo, atafukuzwa katika Jeshi la Polisi na kufikishwa katika mahakama ya kiraia.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Boaz alisema Koplo John ni miongoni mwa askari sita waliokuwa zamu siku ambayo mtuhumiwa huyo inadaiwa alitoroshwa kutoka mahabusu.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwataja askari wengine kuwa Koplo Michael, WP Luciana, PC Arico, PC Kozi na Sajenti Sospeter.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema Koplo John alifikisha katika mahakama hiyo baada ya kudaiwa kuthibitika kuwa ndiye aliyemtorosha mtuhumiwa huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Juzi Kamanda Boaz alisema kutoroka kwa mtuhumiwa huyo kunazua maswali mengi kwa sababu mlango wa mahabusu haukuvunjwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Tutatoa taarifa wakati wowote maana mlango haukuvunjwa, lazima tuone mazingira ya kutoroka kwa mtuhumiwa yalikuwaje, alisema Boaz.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Januari 16, mwaka huu majira ya saa 8:00 usiku, kundi la watu wanaoshukiwa kuwa majambazi wakiwa na bunduki yalivamia maduka matatu katika mji mdogo wa Kibara na kuwaua walinzi wawili na kujeruhi mwingine kwa kuwapiga na vitu kizito vichwani na mtu mwingine Kijiji cha Mugara.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, jana hakuweza kutoa ufafanuzi kuhusiana na matukio hayo ya polisi kuhusika katika matukio kadhaa ya ujambazi, baada ya kuieleza Nipashe kuwa alikuwa na mfululizo wa vikao.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Imeandikwa na Wilbroad Tungaraza, Bunda, Juddy Ngonyani, Rukwa na Charles Ole Ngereza, Arusha.[/FONT]