Polisi Wasababisha Vifo vya Wanafunzi Sumbawanga

Keykey

JF-Expert Member
Dec 1, 2006
3,250
740
Mh. Pinda unayajua haya? Kuna hatua zimechukuliwa au hadi iundwe tume nyingine kuchunguza?

Inapofikia polisi tunaowatarajia kutulinda wanaua watoto wetu? Tunasuburi kuona waliohusika wakiwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Polisi walaumiwa vifo vya wanafunzi Kantalamba
2008-05-04
Na Sammy Kisika PST, Sumbawanga

Wakati maiti ya tatu ya mwanafunzi wa shule ya sekondari Kantalamba ikiopolewa ndani ya mto Lwiche, wananchi mkoani Rukwa wamelitupia lawama jeshi la polisi kwa kudai linahusika kwa kusababisha vifo vya wanafunzi hao.

Mwili wa mwanafunzi wa tatu umepatikana jana nyakati za asubuhi baada ya kuonekana ukiwa unaelea katika mto huo, ambapo ilitolewa taarifa polisi na waokoaji kufika sehemu ya tukio na kuuopoa mwili huo.

Mwanafunzi huyo aliyeopolewa katika mto huo ametambuliwa kuwa ni Joseph Sadala (18), mwanafunzi wa kidato cha pili na mkazi wa Chala wilayani Nkasi mkoani humo.

Hata hivyo mwili wa Joseph, umekutwa tayari ukiwa umeharibika baada ya kukaa kwa mua wa siku tano ndani ya mto huo, ambapo ulitambuliwa na wanafunzi wenzake.

Mazingira ya kupatikana kwa mwili huo ni kama yale ya mwanafunzi aliyeopolewa juzi ambapo Katekista wa Kanisa Katoliki kigango cha Kanatalamba Bw.Cosmas Nchinga aliuona na kuwaarifu walimu wa shule hiyo waliojihimu katika eneo hilo.

Kufuatia kuongezeka kupatikana kwa miili zaidi ya wanafunzi hao, wanaoripotiwa kufa maji, wananchi wa mkoa huo wamelitupia lawama za moja kwa moja kwa jeshi la polisi kwa kile kinachodiwa kuwa walitumia nguvu kubwa katika kudhibiti vurugu za wanafunzi hao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Bw.Sebastian Mbilinyi mkazi wa majengo mjini hapa alidai Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) hakikutakiwa kutumia nguvu kubwa kiasi kile kutokana na hali halisi ya tukio lenyewe lilivyokuwa.

Alisema kuwa vurugu za wanafunzi hao, zilitakiwa kudhibitiwa kwa kutumia busara kwanza, kwa kuwataka wanafunzi hao kuondoka kwenye nyumba ya Mkuu wa shule na kurejea bwenini, lakini badala yake hakuna tangazo lolote lililotolewa isipokuwa FFU walivamia eneo hilo na kuanza kupiga mabomu ya machozi.

``Unajua sisi Watanzania wengine, katika umri huu mkubwa hatujawahi kusikia mlio wa bunduki, sasa inakuwaje kwa hawa vijana ambao wengi wao wametoka mazingira ya vijijini wanaposikia miio ya bunduki mfululizo na ikiwa ni usiku lazima wakimbie hovyo na matokeo yake ndio kama haya ya kutumbukia mtoni`` alisema Mbilinyi.

SOURCE: Nipashe
 
ni masikitiko makubwa sana kwa haya yaliyotokea. Mwenyezi Mungu awarehemu vijana hawa Inshaalah Amin.
 
Serikali iache kutumia maguvu mengi kuliko inavyopaswa. kwanza siyo sifa!
mabavu, mabavu bila kuangalia athari ya mabavu hayo ni ishara za woga na wala siyo busara.
Tunataka vyombo vyetu vya usalama viwalinde wananchi na visitumiwe na wanasiasa woga, wasiojiamini kutatua matatizo ya wananchi. wanasiasa wanaotanguliza mabavu mbele halafu fikra baadae ni hatari sana popote pale duniani
 
Jamani hawa polisi vipi ? Mwema yuko wapi ? Anategemea kufanya nini ? JK unasemaje ? Mbona Tanzania ya JK ina mashida mengi hivi ?
 
Jamani hawa polisi vipi ? Mwema yuko wapi ? Anategemea kufanya nini ? JK unasemaje ? Mbona Tanzania ya JK ina mashida mengi hivi ?

Bado sijaona Polisi wamehusika visi katika vifo vya wanafunzi hawa. Ninachohisi ni labda vurugu zilikuwa kubwa,na Polisi wakaamua kupiga risasi hewani na kutumia hayo mabomu ya machozi, ni katika panic wanafunzi kukimbia na mambo kama hayo ya kuanguka mtoni yakatokea, unless kama Polisi walihusika kuwasukuma huko mtoni, then they should be blamed kwa kusababisha vifo.
May be tupunguze kulalamika tu kila wakati, "Mwema yuko wapi"? "JK unasemaje"? I'm at a loss, how are they involve in this?
Let's say wewe ungekuwa ni hao Polisi katika mazingira hayo, ungefanya nini? Au wewe ni hao wanafunzi, ungefanya nini? Au wewe ni huo uongozi wa shule, ingefanya nini? Au wewe ni..., au, au , au , au.........
Let's think big.

Ni hayo tu.
 
Ni kubaliane na wewe Lizy kwa hayo uliyoysema maana tumekuwa tukilalamika sana lakini tumekuwa tukishudia hata nchi zilizoenselea zimekuwa zikitumia nguvu kila inapobidi tuache kulalamika sana
 
Haya ndiyo yaliyoandikwa kwenye magazeti kuhusiana na fujo hizi.

Kantalamba closed after students’ mayhem‏

PETI SIYAME in Sumbawanga
Daily News; Thursday,May 01, 2008 @00:02

KANTALAMBA Boys’ High School in Sumbawanga Municipality, Rukwa Region, has
been closed indefinitely following students’ riots that left one of them
dead on Monday night. The decision to close the school was reached by a
school board meeting held on Tuesday night to pave way for state organs to
carry out investigation on the incident .

Regional Education Officer (REO), Ms Elizabeth Mfinanga, said in a
statement yesterday that more than 700 students have been given until
today to vacate school premises. She said no one has been arrested
following the incident, adding that the Board continues with its meeting
today to further deliberate on the saga.

A Form One student, Onesmo Mdindikasi, from Mufindi District in Iringa
reportedly drowned in Lwiche River, about two kilometres from the school
when fleeing the police whose help was enlisted by the school to control
the riots.

It all started on Monday night when a number of students armed with
stones, sticks and other objects waylaid the house of the school’s
headmaster, Mr Pius Kasansa, whom they accused of humiliating their fellow
student, one Daudi, by caning him in public.

Daudi was punished on the pitch, allegedly after attacking a Kalangasa
Secondary School student after a soccer match between the two schools in
which Kantalamba High School lost six nil. The irate students also blamed
their Headmaster for being behind their soccer team’s humiliating loss to
their rivals the previous day.

They smashed windows and hurled stones and other objects at the buildings
around the school and the Headmaster’s house and that was when police were
called in to quell the trouble. However, the law enforcers met stiff
resistance from the irate students, and had to use tear gas and engage in
physical battles to control the situation.

In the ensuing fracas, a number of students scampered for safety away from
the scene, including the deceased whose body was retrieved from the river
on Tuesday and was expected to be transported to Mufindi for burial
yesterday.

Mr Kasansa told the 'Daily News' he alerted the police by using his
handset and they immediately rushed to the scene before the situation got
worse. The Regional Police Commander, Mr Isunto Mantage, defended the use
of tear gas, saying the defiant students had been violent and hurled
stones and other objects at the law enforcers. According to the RPC, no
one was arrested but investigations continue.
 
Mm naona waziri wa USARAMA WA RAIA anapaswa kuwajibika kwa hili swala hata MWEMA naye hana budi kuwajibika.
Tatizo la viongozi wetu kung'ang'ania madaraka angalia sasa vijakazi wao wameua nani anapaswa kuwajibika??si wao wakubwa?lazima wawajibike ni aibu kwa polisi jamani/.
 
Ni kubaliane na wewe Lizy kwa hayo uliyoysema maana tumekuwa tukilalamika sana lakini tumekuwa tukishudia hata nchi zilizoenselea zimekuwa zikitumia nguvu kila inapobidi tuache kulalamika sana

Nikidhania unamaanisha nchi zilizoendelea kwenye bold, nakuuliza swali kidogo utaje hizo nchi zilizoendelea ambazo zinatuma polisi wake kufukuza watoto wa shule hadi mtoni na kuwaacha wakafia huko eti kwa sababu wamefanya fujo.
 
Back
Top Bottom