Polisi wanaua raia kila siku lakini wanajeshi wa jwtz walihukimiwa kunyongwa kwa kosa la mauaji

Salathiel m.

Senior Member
Mar 12, 2011
185
41
hivi hapa inakuaje? Au polisi hua wanatumwa? Hata wakisema polisi waliohusika watachukuliwa hatua lakin hua hatusikii iyo kesi inapoishia. Mbona wale wanajeshi waliotuhumiwa kumuua mtoto wa fundikila walihukumiwa fast tena ndani ya miaka 2 kila kitu kikawa kimeisha tena walitumia ushahidi wa kimazingira tu.
 
Siasa zimeteka haki zote za binadamu awapo duniani...Ila haki zetu zipo kwa mungu kwani ukiidai hapa utapunguziwa hata ile ya kuendelea kuufurahia utukufu wa mungu hapa duniani. Fikiria polisi alimuua Mwangosi kila siku zinatolewa sababu mpya Mara gari haina mafuta, mara mgonjwa ila mlalahoi utapelekwa hata na machela.
 
Ni vizuri na nakushauri siku nyingine kabla ya kupost thread yako, fanya preview. Usiwe na haraka ya kupost. Ebu hapo ulliopo ambapo naamini umetulia, soma na wewe hiyo post yako uone inavyosomeka............!
 
kwa hiyo wanajeshi wakiua waachwe?wanajeshi wanalinda mipaka,polisi wanawalinda magamba ndani ya nchi
 
kwa hiyo wanajeshi wakiua waachwe?wanajeshi wanalinda mipaka,polisi wanawalinda magamba ndani ya nchi

Ilikuwaje ndege za majeshi ya mataifa mengine zilifanikiwa kutua nchini bila wao kujua au wao wanalinda mipakani wakulima wasitolosho korosho na mahindi kweda kuuza nje...hii nchi imeoza siyo jeshi, polisi, usalama wa wahuni wa magogoni....
 
Back
Top Bottom