Polisi wanadaiwa kushikilia simu 18 za wanawake wa CHADEMA Pamoja na gari la mmoja wao kwa zaidi ya miezi miwili

Taarifa hii ya kusikitisha na kufedhehesha imefichuliwa na Msemaji wa Chama hicho wa Kanda ya Pwani Mh Gervas Lyenda.

Inadaiwa wamama hao walikamatwa Kwenye viunga vya Mahakama ya Kisutu siku ya Kesi ya Mwenyekiti wa Chadema tarehe 5/8/2021 na kulundikwa Police Central kwa siku 5 mfululizo , huku ndugu zao na wanasheria wao wakikatazwa kuwaona , mmoja wa wamama hao aliyekuwa na gari binafsi , gari yake hiyo nayo imewekwa selo hadi leo hii kwa kosa la kuendeshwa hadi Mahakamani.

Hata hivyo juhudi za wamama hao kudai simu zao zimegonga mwamba , kwa vile kuna TETESI KWAMBA SIMU ZAO HAZIPO , POLISI WAMEGAWANA (tunaendelea kutafuta ukweli)

Tatizo ni rais mwanamke asiyethami wanawake wenzake
 
Back
Top Bottom