Wana JF,
Wilfred Lwakatare ameitwa Makao Makuu ya Polisi sasa hivi kwa mahojiano na jeshi hilo kufuatia video clip iliyowekwa mitandaoni jana.
Kwa taarifa ni kuwa atawakilishwa na wakili Nyaronyo Kicheere na baadaye kama watafungua kesi watakuwa na Mabere Marando.
Je, hii sio double standard ndani ya taifa?
Mbona Mwigulu hajakamatwa baada ya kusema ana mkanda wa njama za kufanya mauaji?
Huko mahakamani kama watamfikisha ndipo watakapoumbuka. Hii sinema wanayotaka kuicheza wasifikiri kwamba watu wamelala.
Walijitutumua kutengeneza filamu ya kichina kwa Jerry Muro wakaishia kuumbuka, sasa naona wanataka tena kuumbuka.
its true - watu wengi hawajui IT inaweza kufanya mambo yapi; tunatumia just 3% ya matumizi ya IT katika nchi hii. so kutengeneza video clip na kuiwekea maneno ni technologia ya zamani ambayo vijana watundu katika nchi zilizoendelea hutumia , leo kwetu tanzania ni kitu kipya mno na watu wote tunahaha eti Lwakatare anaweza kufanya hivyo kwa manufaa ya nani na kwa nini?Sina shida na kuhijiwa Lwakatare. Siku hizi katika ulimwengu wa IT unaweza kutengeneza picha yoyote na kuiwekea maneno hadi ionekane kuwa ni halisi. Kinachonishangaza ni watu kama Rama Ighondu waliotajwa na Ulimboka kuwa hawajaitwa Polisi na kuna kichaa Mkenya anasota rumande. Michael Kamuhanda alitetoa amri ya "Shoot" wala hakuhojiwa, askari aliyetii amri hiyo halali ndiye anasota. Hii haikubliki.
Waswahili mna akili iliyochanganyika na Mchuzi.Mkuu kwa hiyo wewe ulikuwa unategemea kwamba Lwakatare asikamatwe kwa hiyo clip inayotisha namna hiyo? Wacha wamhoji ukweli ujulikane tu
nenda youtube andika neno bukoba boy au hapa jf fungua thred inayosema chadema hapa lwakatare alikuwa ana maanisha nini????
kwa kipindi cha miaka miwili mitatu sasa kumekuwa na matukio ya kinyama na ya uvunjaji haki za binadamu dhidi ya watanzania wachache wenye moyo wa uzalendo wa kuleta haki na usawa kwa jamii ya kitanzania iliyonyanyasika kwa kipindi kirefu.
Hivi majuzi Absalom kibanda mwenyekiti wa jukwaa la wahariri ameteswa na kufanyiwa unyama wa hali ya juu huku jamii ikibaki na maswali yasiyokuwa na majibu.
Aliteswa mpiganaji DR ULIMBOKA wakati yupo kwenye harakati za kuitetea sekta ya afya hapa nchini.
kijana ISSAH alimwagiwa tindikali huko igunga huku kukitokea mauaji ya kusikitisha ya mwandishi DAUDI MWANGOSI mkoani iringa na mwananchi asiye na hatia huko morogoro.
Watu wenye uchungu na nchi yao wamechoka wameona sasa basi..
Tukio la KIBANDA ni mwendelezo wa matukio yanayofuata.. Hivi karibuni mtasikia tukio lingine kubwa dhidi ya mwandishi mwandamizi wa mwananchi communications Ltd......sikiliza video.
Huyu anayeongea ni mchora dili mkuu kwa maelekezo ya mwenyekiti na katibu wake mkuu.
Hii ni part 4, part zingine zimekwisha tekelezwa Ila ZITAWEKWA HAPA WAKATI MAHSUSI UKIFIKA......