Bundewe
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 400
- 141
Katika kipindi cha hivi karibuni, nimefuatilia nyendo za jeshi letu la polisi na kugundua limebadili kabisa mwelekeo wake wa kupambana na uhalifu. Sasa limeanza kushughulikia raia wema.
wametajwa mafisadi waliochangisha fedha kwa ajili ya kupitisha bajeti....polisi kimya. Waziri Mwakyembe kalalamika kuwekewa sumu, polisi ndo kwanza wanatetea. Dr. Slaa na Mnyika wameeleza kwamba wanawindwa na wahalifu ili watoe roho zao ....polisi kimya. Wabunge Mhe. Kiwia na Machemli wamepata kipigo ......polisi wametulia tu. Dr. Ulimboka katekwa na kupigwa .....polisi wako usingizini.
Kwa sasa polisi wako bize kupambana na wanafunzi wanaoandamana, walimu waliogoma, kumwaga maji ya pilipili kwenye mikutano ya chadema, na kubambikizia raia wema kesi.
Tunaelekea wapi????
wametajwa mafisadi waliochangisha fedha kwa ajili ya kupitisha bajeti....polisi kimya. Waziri Mwakyembe kalalamika kuwekewa sumu, polisi ndo kwanza wanatetea. Dr. Slaa na Mnyika wameeleza kwamba wanawindwa na wahalifu ili watoe roho zao ....polisi kimya. Wabunge Mhe. Kiwia na Machemli wamepata kipigo ......polisi wametulia tu. Dr. Ulimboka katekwa na kupigwa .....polisi wako usingizini.
Kwa sasa polisi wako bize kupambana na wanafunzi wanaoandamana, walimu waliogoma, kumwaga maji ya pilipili kwenye mikutano ya chadema, na kubambikizia raia wema kesi.
Tunaelekea wapi????