bablai2020
Senior Member
- Sep 5, 2020
- 149
- 373
Habari zenu wapendwa ,naamini bado mpo na hangover ya furaha ya did.Kuna Jambo ningependa kuliweka hapa nikiamini mamlaka husika wanaweza kulipitia na kuliangalia upya.
Last week nilikuwa na safari ya kuelekea nyanda za juu kusini . Bahati nzuri nilifankiwa kupata lifti kwa jamaa yangu mmoja alikuwa na safari ya uelekeo huo. Kufika pale kitonga kama kawaida unakutatana na mabango mbali mbali ya tahadhari ukitahadharishwa juu ya hatari ya mlima na kwa bahati mbaya mlima mzima huruhusiwi ku overtake. Basi tulipoanza kuupanda mbele kidogo tukakutana na malori manne yamesheheni mzigo tukayafwata kwa taratibu kwa dk kadhaa kufika mbele kidogo akaona upenyo (kwenye mlima kuna sehemu wamepanua barabara kwenda kushoto) jamaa akatanua kwenda kushoto kabisa akapata upenyo wa kupita..kwenda mbele kidogo tukakutana na malori mengine.tukayafwata na tulipofika kona iliyo vikzuri tukachomoka kama kawaida .kazi ikawa ni kuangalia usalama na kuchomoka ..kufika kat Kati ya mlima tukakutana na trafki akatupiga mkono tukae pembeni..tuliposhuka akatuita na kutuonyesha kwamba mmeanza kucheza rafu kuanzia kuleee.kumbe bwana waliposimama wanauwezo wa kuona barabara kuanzia mwanzo wa mlima ..
Tukamsikiliza kisha nikamuuliiza kwa hiyo huu mlima wote haturuhusiwi ku overtake ?
Akanijibu kwa hasira hujui Alama za barabarani ? Umesona uderava kweli?
Nikamjibu mbona hujajibu swali langu?
Nikamwomgezea swali lingine..kwa hiyo mimi mwenye gari dogo Natakiwa niwe nyuma ya malori haya hadi mwisho..hamuoni kwamba ni hatari na upotevu wa muda?
Nikaona anazidi kuwa mkali..yaani wewe badala ya kuomba msamaha unajifanya kuhoji na kujifanya mjuaji?
Nikamjibu sioni sababu ya kuomba msamaha kwa sababu kiuhalisia huu mlima hakuna gari dogo litakalofwata hiyo sheria yenu hata ninyi wenyewe hamuwezi kuifwata..huu niuonevu wa wazi yaani haina tofauti na vibaka wa usiku..mzee akawaka na kusema huyu lazima aandikiwe maana anajifanya mjuaji..nikamwambia jamaa yangu wacha waandike nitakulipia..hakuna kuwapa hela ni bora niichangie serikali yangu.
Mara ghafla wakalisimamisha gari lingine dogo kwa kosa lile ..alipofungua kilo kumbe wanafahamiana wakaanza kuchekena na kupigishana story kisha akamtakia safari njema.nikamuliza huyu jamaa alikuwa nyuma yangu na malori niliyoanza nayo mimi bado nayaona yaleee kwenye kona ya pili ya mlima..ina maana huyu Nae aliyapita ..mbona mmemwachia?
Wakajibu usitufundishe kazi wewee..sisi ndio wenye mlima..nikabaki nashangaa huku nikimwomba amalizie kutuandikia tuendelee na safari..wakati anandika yakapita malori matatu na fuso nyuma yake. Akamwambia dereva wa fuso acha kulal overtake weweee.jamaa akaovertake..nikamuuliiza na hii tunaiitaje ? Akajibu mm ndio mtu wa usalama nimemruhusu ....nikabaki nashangaa.
Kabla sijaondoka nikaliona gari walilopaki pembeni..nikacheka Sana wakaniuliza wacheka nini.
Nikawambia mwaka huu January nilisafiri toka makambako nikapita hapa..kufika ilula huwa hamruhusu ku overtake kabisa ingawa pako vizuri.ghafla nikapitwa kwa kazi na hii gari na mbele kulikuwa na malori kadhaa akayapita tena. Kuna jamaa akaamua kuwaiga hakufika hata mbali akadakwa akaandikiwa ..bahati nzuri mi napafahamu nikawa mpole..kufika kabla ya mlima nikalikuta hili gari lenu mmepaki ..ndio nikagundua kumbe ni trafki ndio maana hamkusimamishwa..wakati nashuka mlima mkaja tena mkanipita kwa kasi na malori kadhaa mbele nikaja nikawakuta hapa ..sasa hizi sheria nyie haziwahusu au?
Wakanijibu kwa hasira tumeshakuandia naomba uondoke..nikawauliza kama mnasena huu mlima ni hatari ina maana hiyo hatari iko kwetu tu? Ila kwa maaskari na jmaa zao Wana kinga.? Nikaona wamekuwa wakali na kurudi kwenye ofisi yao..
Naomba serikali wauangalie huu mlima vizuri..wasitugeuze raia kama chanzo cha mapato.Ni kwa nn mtunge sheria ambayo hta ninyi hamuwezi kuifwata?
Last week nilikuwa na safari ya kuelekea nyanda za juu kusini . Bahati nzuri nilifankiwa kupata lifti kwa jamaa yangu mmoja alikuwa na safari ya uelekeo huo. Kufika pale kitonga kama kawaida unakutatana na mabango mbali mbali ya tahadhari ukitahadharishwa juu ya hatari ya mlima na kwa bahati mbaya mlima mzima huruhusiwi ku overtake. Basi tulipoanza kuupanda mbele kidogo tukakutana na malori manne yamesheheni mzigo tukayafwata kwa taratibu kwa dk kadhaa kufika mbele kidogo akaona upenyo (kwenye mlima kuna sehemu wamepanua barabara kwenda kushoto) jamaa akatanua kwenda kushoto kabisa akapata upenyo wa kupita..kwenda mbele kidogo tukakutana na malori mengine.tukayafwata na tulipofika kona iliyo vikzuri tukachomoka kama kawaida .kazi ikawa ni kuangalia usalama na kuchomoka ..kufika kat Kati ya mlima tukakutana na trafki akatupiga mkono tukae pembeni..tuliposhuka akatuita na kutuonyesha kwamba mmeanza kucheza rafu kuanzia kuleee.kumbe bwana waliposimama wanauwezo wa kuona barabara kuanzia mwanzo wa mlima ..
Tukamsikiliza kisha nikamuuliiza kwa hiyo huu mlima wote haturuhusiwi ku overtake ?
Akanijibu kwa hasira hujui Alama za barabarani ? Umesona uderava kweli?
Nikamjibu mbona hujajibu swali langu?
Nikamwomgezea swali lingine..kwa hiyo mimi mwenye gari dogo Natakiwa niwe nyuma ya malori haya hadi mwisho..hamuoni kwamba ni hatari na upotevu wa muda?
Nikaona anazidi kuwa mkali..yaani wewe badala ya kuomba msamaha unajifanya kuhoji na kujifanya mjuaji?
Nikamjibu sioni sababu ya kuomba msamaha kwa sababu kiuhalisia huu mlima hakuna gari dogo litakalofwata hiyo sheria yenu hata ninyi wenyewe hamuwezi kuifwata..huu niuonevu wa wazi yaani haina tofauti na vibaka wa usiku..mzee akawaka na kusema huyu lazima aandikiwe maana anajifanya mjuaji..nikamwambia jamaa yangu wacha waandike nitakulipia..hakuna kuwapa hela ni bora niichangie serikali yangu.
Mara ghafla wakalisimamisha gari lingine dogo kwa kosa lile ..alipofungua kilo kumbe wanafahamiana wakaanza kuchekena na kupigishana story kisha akamtakia safari njema.nikamuliza huyu jamaa alikuwa nyuma yangu na malori niliyoanza nayo mimi bado nayaona yaleee kwenye kona ya pili ya mlima..ina maana huyu Nae aliyapita ..mbona mmemwachia?
Wakajibu usitufundishe kazi wewee..sisi ndio wenye mlima..nikabaki nashangaa huku nikimwomba amalizie kutuandikia tuendelee na safari..wakati anandika yakapita malori matatu na fuso nyuma yake. Akamwambia dereva wa fuso acha kulal overtake weweee.jamaa akaovertake..nikamuuliiza na hii tunaiitaje ? Akajibu mm ndio mtu wa usalama nimemruhusu ....nikabaki nashangaa.
Kabla sijaondoka nikaliona gari walilopaki pembeni..nikacheka Sana wakaniuliza wacheka nini.
Nikawambia mwaka huu January nilisafiri toka makambako nikapita hapa..kufika ilula huwa hamruhusu ku overtake kabisa ingawa pako vizuri.ghafla nikapitwa kwa kazi na hii gari na mbele kulikuwa na malori kadhaa akayapita tena. Kuna jamaa akaamua kuwaiga hakufika hata mbali akadakwa akaandikiwa ..bahati nzuri mi napafahamu nikawa mpole..kufika kabla ya mlima nikalikuta hili gari lenu mmepaki ..ndio nikagundua kumbe ni trafki ndio maana hamkusimamishwa..wakati nashuka mlima mkaja tena mkanipita kwa kasi na malori kadhaa mbele nikaja nikawakuta hapa ..sasa hizi sheria nyie haziwahusu au?
Wakanijibu kwa hasira tumeshakuandia naomba uondoke..nikawauliza kama mnasena huu mlima ni hatari ina maana hiyo hatari iko kwetu tu? Ila kwa maaskari na jmaa zao Wana kinga.? Nikaona wamekuwa wakali na kurudi kwenye ofisi yao..
Naomba serikali wauangalie huu mlima vizuri..wasitugeuze raia kama chanzo cha mapato.Ni kwa nn mtunge sheria ambayo hta ninyi hamuwezi kuifwata?