Polisi wamejichanganya, kati ya kauli hizi mbili tuchukue ipi?

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Siku zote tunaambiwa usalama ni jukumu la kila mwananchi na hivi karibuni tumeambiwa jeshi linafanya mabadiliko makubwa baada ya kujitathimini na kuona sura ya jeshi hilo kwa jamii imeharibika kiasi cha kukosa ushirikiano toka kwa jamii. Jana wakati wakiwajibu Bavicha wakasema HAWAITAJI MSAADA WA MTU YOYOTE katika kuhakikisha usalama wa nchi na kama watahitaji msaada kwa VYOMBO VINGINE vyenye mafunzo na ueledi wa kufanya kazi hiyo!

Sasa tuchukue lipi? Au ndo kusema wamechanganywa na mkakati wa Bavicha? Walizuia mikutano leo wanasema wanakuja na majibu mengi! Mara hatukuzuia mikutano ya kikanuni na kikatiba! Mara tupewe ushirikiano na usalama ni jukumu la kila raia, baadae hatutaki msaada wa mtu yoyote! TUCHUKUE LIPI?
 
Asa wakitaka Jeshi la Polis lifanye kazi kimatabaka ndani ya nchi mmoja hapo wanakosa .
Simply waache tu vuruguvurugu mda huu na kauli za utengano ...dola imeshachukuliwa na.upande mmoja ,sote sasa tuijenge nchi hadi hapo watakapota Fursa nyingine 2020 wauze sera kwa wananchi . . Ila nw tufanyeni kazi sasa .. Siasa ismekua kama Cancer kwnye Ubongo wa Watanzania .
 
Asa wakitaka Jeshi la Polis lifanye kazi kimatabaka ndani ya nchi mmoja hapo wanakosa .
Simply waache tu vuruguvurugu mda huu na kauli za utengano ...dola imeshachukuliwa na.upande mmoja ,sote sasa tuijenge nchi hadi hapo watakapota Fursa nyingine 2020 wauze sera kwa wananchi . . Ila nw tufanyeni kazi sasa .. Siasa ismekua kama Cancer kwnye Ubongo wa Watanzania .
Siasa ni maisha
 
Ulishawahi kuona kuku kachinjwa na kabla hajakata roho akaachiwa? Ndio hao jamaa sasa
 
Wengi hawajui hilo kwa sababu tu ya tafsiri zao nyembamba za neno siasa. Ukishakufa hapo ndio mwisho wa siasa, lakini ukiwa hai unakwepaje siasa wakati ndio maisha yenyewe?!
Siyo kwamba hawajui bali wanawafanya watu wajinga ili wasifuatilie siasa wafanye wanachotaka. Ndiyo maana utasikia wanakwambia siasa mchezo mchafu wakati hawaachii vyeo vya kisiasa
 
Siasa ndiyo inaendesha maisha ya kila siku.. sahihi kabisa kwakuwa viongozi wanaotuongoza wametokana na michakato ya kisiasa na wanafanya kazi zao kama viongozi wa kisiasa. Hivyo viongozi hawa jukumu lao kubwa ni kuhakikisha wanatimiza ahadi walizozitoa kwa wananchi wao tena kwa wakati. Ni vema vingozi wa kisiasa wabaki katika maeneo yao ya utawala na kuhamasisha maendeleo siyo kusalia na kuishi maeneo yanayoongozwa na viongozi wengine. Kimsingi chama cha siasa kikitaka kufanya mambo ya kikatiba/kanuni waashwe na siyo Bavicha kutaka kufanya kazi ya polisi. Wewe Bavicha kama raia unachotakiwa ni kutoa taarifa na si kujihusisha na shughuli za kipolisi moja kwa moja. Halafu wanaishi waliopo Dodoma ndiyo wanaijua Dodoma kiundani hivyo taarifa kuhusu eneo lao watakuwa wanazo na wataweza kulisaidia jeshi la polisi. Ila nyie mtakao kwenda Dom mtaleta kero tupu!! Mathalan Lissu alipokamatwa alitetewa na mawakili 17.. sasa jiulize wale vijana waliokamatwa Dom itakuwaje!!! Ushauru: Tufanye kazi vijana tuache kutumuwa na wanasiasa kwa maslahi yao!!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom