New Force 2015
Member
- Oct 25, 2013
- 63
- 262
Ndugu salum athuman na mwenzie ambaye ametoroka mnamo mwezi wa kwanza mwaka 2014 alikamatwa na jeshi la police kwa kosa la kukutwa na madawa ya kulevya kinyume cha sheria. Kosa hilo lilimpelekea salum athuman kushitakiwa ktk mahakama ya wilaya ya kinondoni, jalada ktk shitaka hilo linasomeka republic versus salum athuman, criminal case no. 24/2014 likiwa chini ya hakimu bedda. Rm kwa muujibu wa shitaka hilo madawa hayo ya kulevya yalisemekana kuwa na dhamani ya tsh. 4,000,000/= kama vile inavyoisomeka kwenye hati yake ya mashitaka hapo mahakamani.
Mara baada ya shitaka kusomwa mahakamani mwezi huo wa kwanza 2014, mshitakiwa alikana kosa hilo na ndipo alipopelekwa gerezani huko segerea. Baada ya wiiki mbili baadaye mshitakiwa huyo alipewa mdhamana na watu wawili wote wakiwa ni watumishi wa mahakama, kwa majina ni oliver (mhudumu) na ….KARANI Mahaka ya mwanzo hapohapo eneo la mahakama ya wilaya kinondoni. Hata hivyo mheshimiwa hakimu bedda. Rm ambaye ndiye alipewa kusikiliza shitaka hilo tangu awali alijiondoa mara baada ya kuona maelewano na public prosecutor afande d/cpl magoma kutofautiana ktk misimamo yao ktkt uendeshaji wa shitaka hilo.
Kesi hiyo ilihamishiwa kwa mheshimiwa hakimu mwingira. Rm. Baada ya shitaka kuahilishwa mara kwa mara kwa madai kwamba upande wa serikali hawajakamilisha ushahidi. Mnamo tarehe……..UPANDE Wa serikali afande d/cpl magoma mwendesha mashitaka wa serikali d/cpl magoma aliiomba mahakama kubadilisha usomekaji wa shitaka hilo kwa maana ya kiwango cha thamani ya madawa hayo kutoka 4,000,000/= mpaka 40,000,000/= . Katika ombi hilo mheshimiwa hakimu mwingira. Rm aliuambia upande wa washitaka kwamba mahakama haiwezi kupokea ombi ambalo halina uthibitisho kwa maana ya uthaminishaji wa hayo madawa. Hivyo basi mheshimiwa hakimu mwingira aliuambia upande wa mashitaka kuwa walete udhibitisho wa uthaminishji wa madawa hayo kutoka mamlaka husika.
Mnamo tarehe 19th 11, 2014 mara baada ya shitaka kuitwa tena mahakamani, d/cpl magoma alikumbushia mahakama juu ya ombi upande wa serikali la kubadilisha kiwango cha thamani ya madawa hayo kutoka 4,000,000/= mpaka 40,000,000/= na kuomba mahakama ibatilishe masharti ya dhamana akitoa marejeo ya kifungu cha 148 (5) (a) (iii) cha sheria ya mwenendo wa mashitaka ya makosa ya jinai, sheria sura namba 20 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Mheshimiwa hakimu mwingira aliukumbusha upande wa watoa mashitaka kutekeleza amri ya mahakama kwanza ya kuleta barua kutoka kwa mthaminishaji wa madawa hayo. Baada ya hakimu kueleza hayo, mdhamini mmoja wa huyo mshitakiwa alijitokeza mahakamani na kuiomba mahakama kujitoa ktk udhamini alioutoa kwa mdhaminiwa.
Mheshimiwa hakimu alimuliza mdhamini kama alikwisha mjulisha mdahminiwa kwanza, mdhamini alijibu hapana, akaulizwa mdhaminiwa kama aliambiwa na mhamini wake kuwa anajitoa akajibu hapana siukuambiwa mheshimiwa hakimu. Baada ya kuliangalia hilo kuindani, mheshimiwa hakimu mwingira. R.m alisema mahakama haitakuwa imetenda haki kukubali ombi la kujitoa kwa mdhamini gafla kiasi hiki bila kwanza kumjulisha mdhaminiwa. Hivyo basi, mahakama ulitupilia mbali ombi hilo na kumwamuru mdhaminiwa kwamba mahakama inampa wiki mbili atamfute mdhamini mwingine ili huyu anayetaka kujitoa ajitoe. Baada ya kauli hiyo ya mahakama, d/cpl magoma alimwambia mheshimiwa hakimu kama ifuatavyo "hakimu umekosea huwezi kumlazimisha mdhamini anyetaka kujitoa aendelee kuwa mdhamini, hakuna sheria kama hiyo mahakama imekosea.
Hakimu akarudia akasema mahakama haitakuwa imetenda haki kukubali kumuondolea udhamini mdhaminiwa gafla kiasi hiki bila kumpa nafasi ya kujiandaa kutafuta mdhamini. Hivyo mdhamiwa udhamini wake unendelea mpaka baada ya wiki mbili atakapomleta mdhamini mwingine. D/cpl magoma akasema huyo hatoki hapa ndani. Mara d/cpl magoma akamwamuru askari aliyekuwepo pale ndani kumkama mshitakiwa aliyekuwa na udhamini wa mahakama na kupelekwa police lock up tangu tarehe hiyo ya 19th 11, 2014 mpaka leo. Inasemakana mpaka sasa police wanampango wa kumpa kesi ya armed robbery mshitakiwa huyo maana ndugu walipokwenda kumuona huko oysterbay walikataliwa kumuona na kusema kwamba huyu anakosa la armed robbery tunataka akatuoneshe siraha ilipo. Baada ya mahakama kuahirisha shitaka, mdhamini aliyekuwa anaiomba mahakama ajitoe alipoulizwa alisema ameamua kufanya vile kwa kuwa ameambbiwa na d/cpl magoma asipojitoa watamfukuza kazi ama atauwawa.
Anasema aliambiwa na d/cpl magoima kuwa kesi hii ameishikilia kamanda nzowa, ni kesi mbaya jitoe, utapata wapi wewe milioni 40,000,000/= kulipa ikiwa mshitakiwa atatoroka? Maswali ya msingi kuhoji hapa ni kwamba. 1. Je ikiwa mahakama umeamua kuwa mdhaminiwa anaendelea kuwa chini ya udhamini, ni kosa lipi ambalo police wanaendelea kumshikilia mshitakiwa? 2. Je ni nani mwenye mamlaka ya kumpa udhamini mtuhumiwa kati ya police na mahakama ikiwa shitaka limefika mahakamani? 3. Je police wanapata wapi mamlaka ya kupinga maamuzi ya mahakama? 4.
Thamani ya dawa inapandaje toka 4,000,000, hadi 40,000,000?
Mara baada ya shitaka kusomwa mahakamani mwezi huo wa kwanza 2014, mshitakiwa alikana kosa hilo na ndipo alipopelekwa gerezani huko segerea. Baada ya wiiki mbili baadaye mshitakiwa huyo alipewa mdhamana na watu wawili wote wakiwa ni watumishi wa mahakama, kwa majina ni oliver (mhudumu) na ….KARANI Mahaka ya mwanzo hapohapo eneo la mahakama ya wilaya kinondoni. Hata hivyo mheshimiwa hakimu bedda. Rm ambaye ndiye alipewa kusikiliza shitaka hilo tangu awali alijiondoa mara baada ya kuona maelewano na public prosecutor afande d/cpl magoma kutofautiana ktk misimamo yao ktkt uendeshaji wa shitaka hilo.
Kesi hiyo ilihamishiwa kwa mheshimiwa hakimu mwingira. Rm. Baada ya shitaka kuahilishwa mara kwa mara kwa madai kwamba upande wa serikali hawajakamilisha ushahidi. Mnamo tarehe……..UPANDE Wa serikali afande d/cpl magoma mwendesha mashitaka wa serikali d/cpl magoma aliiomba mahakama kubadilisha usomekaji wa shitaka hilo kwa maana ya kiwango cha thamani ya madawa hayo kutoka 4,000,000/= mpaka 40,000,000/= . Katika ombi hilo mheshimiwa hakimu mwingira. Rm aliuambia upande wa washitaka kwamba mahakama haiwezi kupokea ombi ambalo halina uthibitisho kwa maana ya uthaminishaji wa hayo madawa. Hivyo basi mheshimiwa hakimu mwingira aliuambia upande wa mashitaka kuwa walete udhibitisho wa uthaminishji wa madawa hayo kutoka mamlaka husika.
Mnamo tarehe 19th 11, 2014 mara baada ya shitaka kuitwa tena mahakamani, d/cpl magoma alikumbushia mahakama juu ya ombi upande wa serikali la kubadilisha kiwango cha thamani ya madawa hayo kutoka 4,000,000/= mpaka 40,000,000/= na kuomba mahakama ibatilishe masharti ya dhamana akitoa marejeo ya kifungu cha 148 (5) (a) (iii) cha sheria ya mwenendo wa mashitaka ya makosa ya jinai, sheria sura namba 20 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Mheshimiwa hakimu mwingira aliukumbusha upande wa watoa mashitaka kutekeleza amri ya mahakama kwanza ya kuleta barua kutoka kwa mthaminishaji wa madawa hayo. Baada ya hakimu kueleza hayo, mdhamini mmoja wa huyo mshitakiwa alijitokeza mahakamani na kuiomba mahakama kujitoa ktk udhamini alioutoa kwa mdhaminiwa.
Mheshimiwa hakimu alimuliza mdhamini kama alikwisha mjulisha mdahminiwa kwanza, mdhamini alijibu hapana, akaulizwa mdhaminiwa kama aliambiwa na mhamini wake kuwa anajitoa akajibu hapana siukuambiwa mheshimiwa hakimu. Baada ya kuliangalia hilo kuindani, mheshimiwa hakimu mwingira. R.m alisema mahakama haitakuwa imetenda haki kukubali ombi la kujitoa kwa mdhamini gafla kiasi hiki bila kwanza kumjulisha mdhaminiwa. Hivyo basi, mahakama ulitupilia mbali ombi hilo na kumwamuru mdhaminiwa kwamba mahakama inampa wiki mbili atamfute mdhamini mwingine ili huyu anayetaka kujitoa ajitoe. Baada ya kauli hiyo ya mahakama, d/cpl magoma alimwambia mheshimiwa hakimu kama ifuatavyo "hakimu umekosea huwezi kumlazimisha mdhamini anyetaka kujitoa aendelee kuwa mdhamini, hakuna sheria kama hiyo mahakama imekosea.
Hakimu akarudia akasema mahakama haitakuwa imetenda haki kukubali kumuondolea udhamini mdhaminiwa gafla kiasi hiki bila kumpa nafasi ya kujiandaa kutafuta mdhamini. Hivyo mdhamiwa udhamini wake unendelea mpaka baada ya wiki mbili atakapomleta mdhamini mwingine. D/cpl magoma akasema huyo hatoki hapa ndani. Mara d/cpl magoma akamwamuru askari aliyekuwepo pale ndani kumkama mshitakiwa aliyekuwa na udhamini wa mahakama na kupelekwa police lock up tangu tarehe hiyo ya 19th 11, 2014 mpaka leo. Inasemakana mpaka sasa police wanampango wa kumpa kesi ya armed robbery mshitakiwa huyo maana ndugu walipokwenda kumuona huko oysterbay walikataliwa kumuona na kusema kwamba huyu anakosa la armed robbery tunataka akatuoneshe siraha ilipo. Baada ya mahakama kuahirisha shitaka, mdhamini aliyekuwa anaiomba mahakama ajitoe alipoulizwa alisema ameamua kufanya vile kwa kuwa ameambbiwa na d/cpl magoma asipojitoa watamfukuza kazi ama atauwawa.
Anasema aliambiwa na d/cpl magoima kuwa kesi hii ameishikilia kamanda nzowa, ni kesi mbaya jitoe, utapata wapi wewe milioni 40,000,000/= kulipa ikiwa mshitakiwa atatoroka? Maswali ya msingi kuhoji hapa ni kwamba. 1. Je ikiwa mahakama umeamua kuwa mdhaminiwa anaendelea kuwa chini ya udhamini, ni kosa lipi ambalo police wanaendelea kumshikilia mshitakiwa? 2. Je ni nani mwenye mamlaka ya kumpa udhamini mtuhumiwa kati ya police na mahakama ikiwa shitaka limefika mahakamani? 3. Je police wanapata wapi mamlaka ya kupinga maamuzi ya mahakama? 4.
Thamani ya dawa inapandaje toka 4,000,000, hadi 40,000,000?