Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa kuingilia uchaguzi kwa amri toka juu ndio kinaharibu, sio Katiba

Sina tatizo na suala la kuwa na Katiba mpya, lakini tatizo langu ni kuona watu wakidhani Katiba mpya ndio suluhisho la matatizo ya kisiasa nchini. Huko ni kupotoka. Nchi kama Marekani wana katiba ya kidemokrasia sana, lakini leo wanalia Trump na kundi lake kufanya mambo kihuni tu na kwa mabavu. Na hata wanatumia katiba hiyohiyo ya USA kuvuruga demokrasia ya Marekani.

Kwa hiyo tusidhani kwamba tatizo la kukosekana haki na usawa kwa vyama vya upinzani nchini liko kwenye katiba, hapana. Tatizo ni matumizi mabaya ya madaraka na ubabe tu wa wale wanaokuwa katika uongozi. Tatizo ni kiburi na ulevi tu wa madaraka.

Suala la kujiuliza ni kama uwepo wa Katiba mpya utazuia ubabe na ulevi huo wa madaraka. Labda. Lakini tusisahau kwamba viongozi wetu wametumia ubabe hata katika kukiuka mambo ambayo yako wazi kwenye katiba. Mtu ambaye ni mbabe wa kukiuka katiba iliyopo kwa kuwatumia Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa katika kuingilia uchaguzi na kuufanya usiwe huru na haki, hawezi kuacha kufanya hivyo kwa sababu kuna Katiba mpya. Na hawaingilii uchaguzi kwa kuwa Katiba iliyopo inawapa mamlaka ya kuingilia uchaguzi.

Kwa hiyo watu wasijikite kwenye suala la katiba mpya peke yake kama wanataka mabadiliko hapa nchini. Kuna njia nyingi za kumchuna mbuzi ili aliwe kitoweo.
Huo ndio ubovu wenyewe wa katiba.
Ingelikuwa katiba iko sawasawa hayo maagizo toka juu na wapokea maagizo kila mmoja angejua na kutimiza wajibu wake.
 
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
Hapo ndipo hamjaelewa! Jacha ni zao la katiba inayopigwa! Alipatikanaje kuwa mkurugenzi wa uchaguzi.. mmoja wa washidani ndie anamteua msimamizi!!!.....
 
Hata kwa katiba hiihii zikitolewa kinga za viongozi waliopo madarakani na wasitaafu itatufaa tu.
Kama tunasubiri katiba mpya baada ya 2025 basi ipelekwe hoja ya dharula kufuta hiyo sheria.
 
Uko sawa Mkuu! Kama bado Rais yuko juu ya Katiba hata tungepata Katiba kutoka wapi! Kama Rais hawezi kushitakiwa kwa kutumia madaraka vibaya au kukanyaga Katiba bado safari ni ndefu.
 
Sina tatizo na suala la kuwa na Katiba mpya, lakini tatizo langu ni kuona watu wakidhani Katiba mpya ndio suluhisho la matatizo ya kisiasa nchini. Huko ni kupotoka. Nchi kama Marekani wana katiba ya kidemokrasia sana, lakini leo wanalia Trump na kundi lake kufanya mambo kihuni tu na kwa mabavu. Na hata wanatumia katiba hiyohiyo ya USA kuvuruga demokrasia ya Marekani.

Kwa hiyo tusidhani kwamba tatizo la kukosekana haki na usawa kwa vyama vya upinzani nchini liko kwenye katiba, hapana. Tatizo ni matumizi mabaya ya madaraka na ubabe tu wa wale wanaokuwa katika uongozi. Tatizo ni kiburi na ulevi tu wa madaraka.

Suala la kujiuliza ni kama uwepo wa Katiba mpya utazuia ubabe na ulevi huo wa madaraka. Labda. Lakini tusisahau kwamba viongozi wetu wametumia ubabe hata katika kukiuka mambo ambayo yako wazi kwenye katiba. Mtu ambaye ni mbabe wa kukiuka katiba iliyopo kwa kuwatumia Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa katika kuingilia uchaguzi na kuufanya usiwe huru na haki, hawezi kuacha kufanya hivyo kwa sababu kuna Katiba mpya. Na hawaingilii uchaguzi kwa kuwa Katiba iliyopo inawapa mamlaka ya kuingilia uchaguzi.

Kwa hiyo watu wasijikite kwenye suala la katiba mpya peke yake kama wanataka mabadiliko hapa nchini. Kuna njia nyingi za kumchuna mbuzi ili aliwe kitoweo.
Umesema vema. Lakini kumbuka Katiba mpya inaandamana na Tume Huru ya Uchaguzi, ambayo haiwajibiki kwa Rais wala hao viongozi wa Serikali katika ngazi nyingine. Kenya, Malawi na Zambia iliwezekana mpaka Incumbent President anasema Tume imemwonea
 
Huo ndio ubovu wenyewe wa katiba.
Ingelikuwa katiba iko sawasawa hayo maagizo toka juu na wapokea maagizo kila mmoja angejua na kutimiza wajibu wake.
Mkuu, sio kila jambo la kijinga na ovyo linalotendeka nchini suluhisho lake litapatikana katika katiba. South Africa wana katiba ambayo ni moja wapo ya most democratic constitutions in the world, lakini bado wana mambo ya kijinga sana katika uongozi kwa sababu tu ANC ni chama kikongwe
 
Umesema vema. Lakini kumbuka Katiba mpya inaandamana na Tume Huru ya Uchaguzi, ambayo haiwajibiki kwa Rais wala hao viongozi wa Serikali katika ngazi nyingine. Kenya, Malawi na Zambia iliwezekana mpaka Incumbent President anasema Tume imemwonea
Tukipata tume huru na katiba mpya, na CCM au Chadema au TLP ni wale wale, unafikiri itatupa uhakika wa mjinga mwingine kutuharibia nchi? Ndio maana nikauliza, katiba ya USA ina tatizo gani? Lakini mbona ilileta kiongozi aliezua taharuku kali sana huko? Katiba ya South Africa ina tatizo gani? Lakini mbona bado inatoa viongozi wabovu na poor social services huku kundi kubwa la wananchi likiwa kwenye umasikini mkubwa miaka zaidi ya 20 toka wapate katiba iliyosemwa ni one of the best in the world?
 
Back
Top Bottom