Polisi wakihakikisha Usalama wa katibu Mkuu wa CCM Taifa Bashiru Ally akiwa ziarani Mkoani Mtwara

mkulima gwakikolo,
Binafsi nawalaumu sana wapinzani kukuaa kimya, hayo mambo walipaswa kuyaweka wazi ikiwezekana waandike rasmi barua jeshi la polis kutokukubaliana Na jeshi la polis kwenye ubaguzi wa mambo ya kisiasa. Polisi wanapaswa kuwa neutral.
 
Chama kinalindwa Na dola, hii Ni hatari sana.nilitamani polis wafanye haya kwa vyama vyote.Huu sio usawa aliopigania mwalimu nyerere.
Mlishajitengenezea mazingira ya kutowaamini polisi,mtawezaje kufanya nao kazi?
Kuna sehemu mliomba ulinzi mkanyimwa?
 
Hivi ungelikuwa ndo RPC halafu jamaa apatie tatizo jimboni mwako; Ungelisema umepungukiwa na nyenzo gani za kumlinda tu? Kwani hao feefeeyuu ni wako hata useme wamekugharimu hela nyingi?? Nadhani swali la kujiuliza ni; Wamevuta mpunga mkuu kiasi gani? Acha watoto wawenzio wachuchumae wakijinyea kwa shibe za baba zaao
Atapata tatizo gani kwa mfano? Ukitoa mfano mmoja tu wa tatizo linaloweza kumpata ambalo suluhu yake ni hawa wanaohemea juu juu ingependeza.
 
1582518540518.png
 
Hivi hawa ni UVCCM au ni polisi wetu?
Tumekuwa tunaaminishwa polisi wako neutral kwenye siasa
Lakini hili kina nipa mashaka, ndio maana vyama vya upinzani wana lalamika kuhusu kuzuiliwa kufanya makusanyiko ambayo ni haki yao kikatiba.
Kama polisi wameweza kuwa na mapenzi makubwa hivi tena ya wazi kwa Ccm je kuna uwezekano wa kutenda haki hapa?
Tunataka tamko toka Ccm na kutoka jeshi la polisi kuhusu hili jambo
Screenshot_20200224-121621.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katibu Mkuu wa ccmni kiongozi mwandamizi wa Nchi

Yeye anaismamia serkali

Usimfananishe na waropokaji
 
Back
Top Bottom