Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,360
MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA KUKUTANA DODOMA KUJIPANGA NA UCHAGUZI MKUU UJAO
Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi hapa nchini,
kesho Jumatatu Desemba, 14, watakutana mjini Dodoma kupanga mikakati mipya itakayofanikisha uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na madiwani utakaofanyika baadaye mwakani.
Mkuu wa Sera na Utafiti wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msadizi Mwandamizi Paul Ntobi, amesema leo mjini hapa kuwa mafunzo hayo yatafunguliwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Lewis Makame.
Amesema kuwa mafunzo hayo pia yatawashirikisha Wakuu wa Vikosi vya Kutuliza Ghasia wa mikoa, Wakuu wa Upelelezi na Wakuu wa Operesheni maalum kutoka kila mkoa hapa nchini.
Kamanda Ntobi amesema mafunzo kama hayo pia yaliwahi kutolewa kwa Wakuu wa Polisi wa walaya na wa Upelelezi wakati wa maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.
Amesema Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Saidi Mwema na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini Kamishna Robert Manumba, watahudhuria kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo yatakayofanyika mjini Dodoma.
Tayari washiriki wote wa mafunzo hayo kutoka bara na Visiwani wameshawasili mjini Dodoma kwa ajili ya mafunzo hayo.
Vyama 18 vya Siasa vyenye usajili wa kudumu hapa nchini, vinatarajiwa kushiriki katika kinyang'anyiro hicho huku baadhi ya vyama hivyo vikiwa na wagombea wa viti vya urais na vingine vikiwa na Wagombea wa Viti vya Ubunge na Udiwani pekee.
kesho Jumatatu Desemba, 14, watakutana mjini Dodoma kupanga mikakati mipya itakayofanikisha uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na madiwani utakaofanyika baadaye mwakani.
Mkuu wa Sera na Utafiti wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msadizi Mwandamizi Paul Ntobi, amesema leo mjini hapa kuwa mafunzo hayo yatafunguliwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Lewis Makame.
Amesema kuwa mafunzo hayo pia yatawashirikisha Wakuu wa Vikosi vya Kutuliza Ghasia wa mikoa, Wakuu wa Upelelezi na Wakuu wa Operesheni maalum kutoka kila mkoa hapa nchini.
Kamanda Ntobi amesema mafunzo kama hayo pia yaliwahi kutolewa kwa Wakuu wa Polisi wa walaya na wa Upelelezi wakati wa maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.
Amesema Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Saidi Mwema na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini Kamishna Robert Manumba, watahudhuria kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo yatakayofanyika mjini Dodoma.
Tayari washiriki wote wa mafunzo hayo kutoka bara na Visiwani wameshawasili mjini Dodoma kwa ajili ya mafunzo hayo.
Vyama 18 vya Siasa vyenye usajili wa kudumu hapa nchini, vinatarajiwa kushiriki katika kinyang'anyiro hicho huku baadhi ya vyama hivyo vikiwa na wagombea wa viti vya urais na vingine vikiwa na Wagombea wa Viti vya Ubunge na Udiwani pekee.
source: michuzi.blog
Wadau hii inashangaza kidogo, polisi wanakutana kupanga mikakati ya kufaniskisha uchaguzi mkuu, kusimamia usalama wakati wa uchaguzi mkuu ni sehemu ya kawaida kabisa ya kazi za kipolisi je wanahitaji kupanga mikakati, hii mbona inatia shaka.
Pili mafunzo yanafunguliwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ambaye ni sehehmu muhimu katika kuandaa, kusimamia na mwishoni kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu, kwa nini wasimwite Prof Lipumba au sema Mbowe ili afungue huo mkutano, Mwenyekiti wa tume ana nini cha ziada cha kuwaambia.
Kwa nini Mwenyekiti asikae na wananchi wapiga kura kuwapa elimu ya Uraia ambayo wananchi wanaikosa na badala yake yuko busy na mapolisi.
Refa na kibendera waliochaguliwa na timu moja wakijifungia pamoja kwenye chumba wakitoka humo na kuchezasha mechi baina ya timu iliyowachagua refa na kibendera hao dhidi ya timu pinzani, kutakuwa na usalama kweli???
Naomba tulijadili hili.
Pili mafunzo yanafunguliwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ambaye ni sehehmu muhimu katika kuandaa, kusimamia na mwishoni kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu, kwa nini wasimwite Prof Lipumba au sema Mbowe ili afungue huo mkutano, Mwenyekiti wa tume ana nini cha ziada cha kuwaambia.
Kwa nini Mwenyekiti asikae na wananchi wapiga kura kuwapa elimu ya Uraia ambayo wananchi wanaikosa na badala yake yuko busy na mapolisi.
Refa na kibendera waliochaguliwa na timu moja wakijifungia pamoja kwenye chumba wakitoka humo na kuchezasha mechi baina ya timu iliyowachagua refa na kibendera hao dhidi ya timu pinzani, kutakuwa na usalama kweli???
Naomba tulijadili hili.