Polisi wa Tanzania wanasa Malawi wakifuatilia wahalifu

They are very lucky the Geneva convention accord and treaty came to their rescue otherwise they would have been lynched to death because by trespassing other sovereign state border is to breach international land border and that offense is attempted murder and if convicted straight away an execution sentence by firing squad.

They are lucky!
Kwa lugha iliyotumika hapa .....sijui hata Ile C ya ngeli niliipataje wallah...🙌
 
Ila elimu angalau ya diploma na degree ni muhimu sana kwa Polis wetu, ijapokuwa kuna ulakini katika elimu yetu ya juu!

Nilijaribu kufanya utafiti kidogo, na kubaini kuna utofauti mkubwa sana wa kimawazo kati ya Polisi au mwanajeshi mwenye bachelor degree na huyo form four failure!
Serikali ya kipuuzi sana hii, inamwaga maelfu ya ajira kwa failures, badala ya kuwapa wasomi wasio na ajira.

Afu badae hiyohiyo serikali inakuja kujisifu imemwaga ajira kwa wasomi.

Upumbavu wa kiwango cha SGR, mazafucker.
 
Natoa wito kwa Wazazi kutozaa polisi ambao wanatuletea Majanga kama haya unavukaje mpaka kwenda nchi jirani bila vibali tena na silaha... Kesi yao hao askari ni ugaidi na kutaka kuteka Serikali ya Malawi... Walitaka kwenda ku occupier
 
Heading ilitakiwa kuwa Nduli wa Tanzania atuma majeshi kuivamia kijeshi nchi jirani ya Malawi.. Wanajeshi wote wakamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi na raia tu... Je jeshi lao itakuwaje?
 
Sijasema lolote juu kujua au kutokujua Kiingereza.Nina Cho jua Polisi wa Tanzania ni zero kabisa Kwenye lugha tukiachana hayo waambie siku moja wavuke mpaka wa Sirari wafike Migori waone au wavuke mpaka wa Namanga waone.
Acha upumbavu mbona polisi wengi wa kenya wanavuka kuja sirari na wengine wanabana pale mpakani wanangoja mtanzania akatize wamkamate hana barakoa atoe rushwa na hawataki waone wallet imetuna pumbavu
 
Siku zote tunasema IGP Sirro na genge lake lote wanaojiita Polisi uwezo wao wa kufanya kazi professionally na kwa kutumia akili ni mdogo sana, lakini watu wanabisha. Haya ndio matokeo. Hebu angalia maelezo ya hili tukio hapa chini, na ieleweke ni kina nani walifanya upumbavu wa namna hii. Angalia hata kuandika tu ni tatizo, hakuna hata vituo.

TAARIFA YA TUKIO LA ASKARI POLISI WETU 7 KUINGIA NCHINI MALAWI.

MNAMO TAREHE 15/09/2021 MAJIRA KATI YA SAA 16:30 - 17:30HRS HUKO MANEO YA KITONGOJI CHA MTIMA, KIJIJI CHA IKUMBILO, KATA YA CHITETE, TARAFA YA BULAMBYA, WILAYA YA ILEJE NA MKOA WA SONGWE ASKARI G.3695 D/SGT RAMADHANI,H.694 PC EDWARD, H.8096 PC SAFARI, WP.12285 PC ANASTAZIA, H.9727 PC JOSEPH, H.9781 PC HUSSEIN NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA GARI PT.3676 TOYOTA L/CRUISER MALI YA JESHI LA POLISI TANZANIA WAKITOKEA VWAWA KUPELEKA WATUHUMIWA WA KESI YA MAUAJI PI.3/2020, WALIPOFIKA MAENEO YA MTIMA NA KUONA PIKIPIKI INAYOSADIKIWA KUWA IMEBEBA MAGENDO KUTOKA NCHI JIRANI YA MALAWI, WALIISIMAMISHA LAKINI PIKIPIKI HIYO ILIAMUA KUKIMBIA KUELEKEA NCHI JIRANI YA MALAWI, ASKARI. WALIAMUA KUIFUKUZIA NA KUVUKA MPAKA WA TANZANIA NA KUINGIA NCHINI MALAWI NA NDIPO WANANCHI WA MALAWI WALIIZINGIRA GARI HILO IKIWA NA ASKARI NCO G3695 DSGT RAMADHAN, H.8096 PC SAFARI, H9727 PC JOSEPH, H.694 D/C EDWARD, H.9781 PC HUSSEIN, WP.12285 PC ANASTAZIA NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA SILAHA MBILI AINA YA AK 47 NA KUANZA KUWASHAMBULIA.KWA.MAWE NA BAADAYE KUPATA MSAADA WA KUOKOLEWA NA ASKARI POLISI WA MALAWI(+) KATIKA VULUGU HIZO ASKARI MMOJA H8764 PC PC JUMANNE AMBAYE NI DEREVA ALIJERUHIWA KWA KUKATWA NA PANGA KICHWANI HALI YAKE SIO MBAYA ANAENDELEA VIZURI PIA GARI INASEMEKANA LIMEHARIBIWA KWA KUPIGWA KWA MAWE NA SILAHA AK 47 ZOTE MBILI ZIPO SALAMA NA ZIMEHIFADHIWA KITUO CHA POLISI CHITIPA MALAWI. ASKARI NO. G.3695 D/SGT RAMADHANI AMBAYE ALIKUWA KIONGOZI WAO, H.8096 PC SAFARI NA H.9727 PC JOSEPH WALIFANIKIWA KUTOROKA KATIKA VULUGU HIZO NA KURUDI KITUONI SALAMA NA WAPO MAHABUSU KWA HATUA ZA KINIDHAMU. MAWASILIANO KATI YA UONGOZI WA WILAYA NA MKOA TANZANIA NA MALAWI YANAENDELEA KWA AJILI YA KUWAREJESHA NCHI ASKARI HAO PAMOJA NA GARI NA SILAHA.
Vipi hao watuhumiwa wa mauaji wako wapi?
 
Watu wengi wanatype kuuliza 'Hawakuuona mpaka?' wakidhani ni kama kwenye muvi kwamba mpaka utakua na watu wa custom, askari wengine, maafisa uhamiaji n.k.

Yes, sehemu ambayo mtu anataka kupita kihalali itakua hivyo.

Lakini hawa walikua wanafuatilia magendo unadhani wangepitia hapo? Logically it means walipita njia za panya na njia hizo zilivyo kujua kwamba upo sehemu nyingine ni kazi ya ziada. Kwani mnavyosikia kuna waTz wananunua sukari Malawi unafikiri wanapita wapi? Kwenye hilo eneo la ukaguzi?

Na kuna swala jingine hapa. Hii ishu haitakua treated kama askari wameingia Malawi bali itakua ni waTz wameingia Malawi. Na haitasemwa wananchi wa Ipenza wamerushia mawe gari la askari wa Tz no itakua ni waMalawi wamewashambulia waTz.

Kwahiyo mtu yuko bize kusema hao askari ni divisheni zero but actually hata yeye hana tofauti na hao askari na inamaanisha tu hata kiingereza hajui. WaTz tubadilike tusiione habari na kuipokea kwa kuangalia inafeed vipi ego zetu badala yake tuielewe habari na tusisome ili tujibu, tusome kuelewa.

Kama unashangaa hao askari kuingia Malawi huku hawana hata ramani nikikuambia kuna jenerali wa jeshi aliingia nchi nyingine, akiwa na ramani na akasimika bendera ya nchi yake eneo jingine huku akiwa na kikosi bila kujua kama yupo nchi nyingine utasemaje?
Usiwatetee polisi wamefanya uzembe, kwenye gari umebeba watuhumiwa wa mauaji unaenda kuhangaika na pikipiki ili iweje? Yote hiyo ni kutaka rushwa tu, sasa unajua hao watuhumiwa wa mauaji walipo? Je kama wametoroka kutokana na hilo sekeseke
 
wao walivuka mipaka wanategemea nini? au ndo walikuwa wanaringishia na uniform zao, kwamba na wao wanaajira YEHODAYA.
Hongera sana polisi wetu kutuwakilisha vizuri kwa kuipeleka Tanzania kimataifa, kuwathibitishia kuwa utendaji wenu unaovuka mipaka kufikiri kiweredi na kulalamikiwa na watanzania ni wa kweli.
 
30 Reactions
Reply
Back
Top Bottom