Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,348
- 217,390
Polisi wa Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya wametandikwa na Raia wa Malawi baada ya kuingia nchi hiyo ya kigeni kwa lengo la kuwasaka wafanya magendo .
Bado Haijafahamika walikopata utaratibu huo wa kuingia nchi ya watu kutafuta wahalifu huku Nchi ya Malawi ikiwa na Polisi wake , hata hivyo tunaishukuru serikali ya Malawi kwa kuwanusuru na vifo baada ya kuingilia kati kuwaokoa.
====
Mnamo tarehe 15/09/2021 majira kati ya saa 16:30 - 17:30hrs huko maneo ya kitongoji cha Mtima, kijiji cha Ikumbilo, kata ya Chitete, tarafa ya Bulambya, wilaya ya Ileje na mkoa wa Songwe askari G.3695 d/sgt Ramadhani, H.694 pc Edward, h.8096 pc Safari, wp.12285 pc Anastazia, h.9727 pc Joseph, h.9781 pc Hussein na h.8764 pc Jumanne wakiwa na gari pt.3676 toyota l/cruiser mali ya jeshi la polisi Tanzania wakitokea Vwawa kupeleka watuhumiwa wa kesi ya mauaji pi.3/2020, walipofika maeneo ya Mtima na kuona pikipiki inayosadikiwa kuwa imebeba magendo kutoka nchi jirani ya Malawi, waliisimamisha lakini pikipiki hiyo iliamua kukimbia kuelekea nchi jirani ya Malawi, askari.
Waliamua kuifukuzia na kuvuka mpaka wa Tanzania na kuingia nchini Malawi na ndipo wananchi wa Malawi waliizingira gari hilo ikiwa na askari nco g3695 dsgt Ramadhan, h.8096 pc Safari, h9727 pc Joseph, h.694 d/c Edward, h.9781 pc Hussein, wp.12285 pc anastazia na h.8764 pc jumanne wakiwa na silaha mbili aina ya ak 47 na kuanza kuwashambulia kwa mawe na baadaye kupata msaada wa kuokolewa na askari polisi wa Malawi(+) katika vulugu hizo askari mmoja h8764 pc pc Jumanne ambaye ni dereva alijeruhiwa kwa kukatwa na panga kichwani hali yake sio mbaya anaendelea vizuri pia gari inasemekana limeharibiwa kwa kupigwa kwa mawe na silaha ak 47 zote mbili zipo salama na zimehifadhiwa kituo cha polisi Chitipa Malawi.
Askari no. G.3695 d/sgt Ramadhani ambaye alikuwa kiongozi wao, h.8096 pc Safari na h.9727 pc Joseph walifanikiwa kutoroka katika vulugu hizo na kurudi kituoni salama na wapo mahabusu kwa hatua za kinidhamu. Mawasiliano kati ya uongozi wa wilaya na mkoa Tanzania na Malawi yanaendelea kwa ajili ya kuwarejesha nchi askari hao pamoja na gari na silaha.
Pia soma: Songwe: Askari waliovuka mpaka kuingia Malawi kinyume cha sheria wafukuzwa kazi
Bado Haijafahamika walikopata utaratibu huo wa kuingia nchi ya watu kutafuta wahalifu huku Nchi ya Malawi ikiwa na Polisi wake , hata hivyo tunaishukuru serikali ya Malawi kwa kuwanusuru na vifo baada ya kuingilia kati kuwaokoa.
====
Mnamo tarehe 15/09/2021 majira kati ya saa 16:30 - 17:30hrs huko maneo ya kitongoji cha Mtima, kijiji cha Ikumbilo, kata ya Chitete, tarafa ya Bulambya, wilaya ya Ileje na mkoa wa Songwe askari G.3695 d/sgt Ramadhani, H.694 pc Edward, h.8096 pc Safari, wp.12285 pc Anastazia, h.9727 pc Joseph, h.9781 pc Hussein na h.8764 pc Jumanne wakiwa na gari pt.3676 toyota l/cruiser mali ya jeshi la polisi Tanzania wakitokea Vwawa kupeleka watuhumiwa wa kesi ya mauaji pi.3/2020, walipofika maeneo ya Mtima na kuona pikipiki inayosadikiwa kuwa imebeba magendo kutoka nchi jirani ya Malawi, waliisimamisha lakini pikipiki hiyo iliamua kukimbia kuelekea nchi jirani ya Malawi, askari.
Waliamua kuifukuzia na kuvuka mpaka wa Tanzania na kuingia nchini Malawi na ndipo wananchi wa Malawi waliizingira gari hilo ikiwa na askari nco g3695 dsgt Ramadhan, h.8096 pc Safari, h9727 pc Joseph, h.694 d/c Edward, h.9781 pc Hussein, wp.12285 pc anastazia na h.8764 pc jumanne wakiwa na silaha mbili aina ya ak 47 na kuanza kuwashambulia kwa mawe na baadaye kupata msaada wa kuokolewa na askari polisi wa Malawi(+) katika vulugu hizo askari mmoja h8764 pc pc Jumanne ambaye ni dereva alijeruhiwa kwa kukatwa na panga kichwani hali yake sio mbaya anaendelea vizuri pia gari inasemekana limeharibiwa kwa kupigwa kwa mawe na silaha ak 47 zote mbili zipo salama na zimehifadhiwa kituo cha polisi Chitipa Malawi.
Askari no. G.3695 d/sgt Ramadhani ambaye alikuwa kiongozi wao, h.8096 pc Safari na h.9727 pc Joseph walifanikiwa kutoroka katika vulugu hizo na kurudi kituoni salama na wapo mahabusu kwa hatua za kinidhamu. Mawasiliano kati ya uongozi wa wilaya na mkoa Tanzania na Malawi yanaendelea kwa ajili ya kuwarejesha nchi askari hao pamoja na gari na silaha.
Pia soma: Songwe: Askari waliovuka mpaka kuingia Malawi kinyume cha sheria wafukuzwa kazi