Polisi wa Tanzania ni kero kwa wasafirishaji wa kimataifa.

commonmwananchi

JF-Expert Member
Mar 12, 2011
3,377
1,952
kutokana na Ripoti ya mwenyekiti wa kamati ya bunge ya miundombinu Mh Peter serukamba,bungeni sasa hivi.
Ni kwamba bandari ya Dar es salaam,imekumbwa na wimbi la kukimbiwa na wateja kwa wingi kutokana na sababu kadhaa.mojawapo ikiwa ni usumbufu wanaoupata wateja kwa kusimamishwa mara kwa mara barabarani na polisi wa Tanzania wanapokuwa safarini kusafirisha mizigo yao kutoka bandari ya Dar es salaam kuelekea katika nchi zao.

Ametoa mfano wa takwimu kwamba Lori moja likisafiri toka Dar es salaam hadi Rusumo mpakani mwa Rwanda,linasimamishwa na polisi njiani mara 45, na wakati huo huo akasema Lori linalosafirisha mzigo toka bandari ya Mombasa hadi Kigali kupitia Uganda linasimamishwa mara 5 tu.

My take: Namuomba IGP mwema atumie taarifa hii kufanya marekebisho makubwa katika jeshi lake ili kuokoa uchumi wa nchi yetu, ikiwa ni pamoja na kamata kamata ndani ya nchi yetu zisizozingatia haki ambazo zinasababisha nguvu kazi ya wananchi wengi kukaa mahabusu bila sababu za msingi na kuligharimu taifa chakula ulinzi na matibabu ikiwa ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi pamoja na kuwasababishia matatizo familia zao.ambazo mara zingine huwa ni wategemezi kwa ndugu hao.
 
Ingekuwa ni vizuri na bora ikiwa kusimamishwa kwenyewe kungekuwa ni ktk ukaguzi wa kawaida usiotanguliza namna gani ufanyike usumbufu utakaosababisha rushwa.kwa sababu kwanza wanalalamikiwa kuwa siyo waelewa kitu ambacho siyo dhana hii ya kuonekana Siyo waelewa inasababishwa na wao kukwepa kuuliza maswala ya msingi ambayo pengine wanahisi majibu yake yatakuwa wazi hivyo wanatafuta maswala mengine ambayo wanafahamu hayana tija kwa mizigo ya transit wala hayahitaji hivyo wanaangalia zaidi wapi wapate rushwa.

Dawa ya hili ni wenyewe kupewa elimu ya uzalendo na kufundishwa sana namna ya kuwaencourage watu kama hao wasafirishaji ambao tunawahitaji kwa ajili ya uchumi kuanzia bandarini hadi huko njiani wanakopita wanakula wanalala na mambo kama hayo,
 
Mmhhh!! Nakwambia sisi watanzania ka vile tumelogwa huko barabarani ni tatizo pamoja na kwamba wageni tulio nao ni wachache kuanzia barabarani hadi viwanja vya ndege wanaosababisha ama kuongeza ukubwa wa tatizo ni hao watendaji tuliowaweka kuanzia barabarani hadi mipakani ama viwanja vya ndege jaribu kwenda border ama airprt utakwama ikiwa huna cheti cha chanjo na umekosa rushwa ya kuwapa ambacho kwa upande wa pili wa nchi unakotoka ama kwenda hilo siyo tatizo sasa cha kushangaza je huko Kenya ama upande wa pili wa mpaka wao hawaaogopi maradhi???

Jaribu kuvuka border ya namanga ama kia airport bila niliyoyataja ndipo utahakiki nilisemalo. Huu ni usumbufu kwa mgeni aliyetoka ngambo na kuingia ktk nchi kupitia kama siyo border uwanja wa ndege kwa kufanya connection kutoka upande wa pili wa nchi.

Nchi imeoza kwa visheria ambavyo havisaidii nchi vimewekwa kwa ajili ya kulelea rushwa tuu....
 
Ingekuwa ni vizuri na bora ikiwa kusimamishwa kwenyewe kungekuwa ni ktk ukaguzi wa kawaida usiotanguliza namna gani ufanyike usumbufu utakaosababisha rushwa.kwa sababu kwanza wanalalamikiwa kuwa siyo waelewa kitu ambacho siyo dhana hii ya kuonekana Siyo waelewa inasababishwa na wao kukwepa kuuliza maswala ya msingi ambayo pengine wanahisi majibu yake yatakuwa wazi hivyo wanatafuta maswala mengine ambayo wanafahamu hayana tija kwa mizigo ya transit wala hayahitaji hivyo wanaangalia zaidi wapi wapate rushwa.dawa ya hili ni wenyewe kupewa elimu ya uzalendo na kufundishwa sana namna ya kuwaencourage watu kama hao wasafirishaji ambao tunawahitaji kwa ajili ya uchumi kuanzia bandarini hadi huko njiani wanakopita wanakula wanalala na mambo kama hayo,
Sasa hapo umesema kweli,nafikiri Mh Serukamba aliruka kipengele cha kusema "wanasimamishwa na polisi wa Tanzania wakizushiwa makosa mbalimbali na kulazimishwa kutoa rushwa" Halafu inashangaza jinsi jeshi hili linavyowapanga askari wake barabarani.unakuta ni umbali mfupi sana kutoka kizuizi kimoja hadi kingine.suala hapa ni kama vile hawaamianiani au?
 
Mmhhh!! Nakwambia sisi watanzania ka vile tumelogwa huko barabarani ni tatizo pamoja na kwamba wageni tulio nao ni wachache kuanzia barabarani hadi viwanja vya ndege wanaosababisha ama kuongeza ukubwa wa tatizo ni hao watendaji tuliowaweka kuanzia barabarani hadi mipakani ama viwanja vya ndege jaribu kwenda border ama airprt utakwama ikiwa huna cheti cha chanjo na umekosa rushwa ya kuwapa ambacho kwa upande wa pili wa nchi unakotoka ama kwenda hilo siyo tatizo sasa cha kushangaza je huko Kenya ama upande wa pili wa mpaka wao hawaaogopi maradhi??? Jaribu kuvuka border ya namanga ama kia airport bila niliyoyataja ndipo utahakiki nilisemalo. Huu ni usumbufu kwa mgeni aliyetoka ngambo na kuingia ktk nchi kupitia kama siyo border uwanja wa ndege kwa kufanya connection kutoka upande wa pili wa nchi.nchi imeoza kwa visheria ambavyo havisaidii nchi vimewekwa kwa ajili ya kulelea rushwa tuu....
Pia umesahau kero nyingine kwenye hizo border zetu,nayo ni ile ya mtu unafika pale border unajaziwa kila kitu na customs wa kwetu halafu unagonga paspoti yako na kuvusha gari upande wa pili na tatizo linaanza la wale wanaojiita maajenti.

Wanataka uwape wao Documents na wanaanza mizunguko toka ofisi moja hadi nyingine mara wanakurudia sijui ooh! bado hujalipia overtime mara ooh gari yako ni zaidi yz CC4500 na ni commercial registered hivyo sijui lete hela hii,au kama hutaki risiti sema tuongee nao nk....
 
Sasa hapo umesema kweli,nafikiri Mh Serukamba aliruka kipengele cha kusema "wanasimamishwa na polisi wa Tanzania wakizushiwa makosa mbalimbali na kulazimishwa kutoa rushwa" Halafu inashangaza jinsi jeshi hili linavyowapanga askari wake barabarani.unakuta ni umbali mfupi sana kutoka kizuizi kimoja hadi kingine.suala hapa ni kama vile hawaamianiani au?

Swala la kutokuaminiana hapa halipo hao wote wamepangwa kwa wingi ili makusanyo yawe makubwa maana hawa waamepangwa na wametumwa pesa siyo kwamba wamekurupuka ama wamekosa kazi za kufanya.mgao unatembea kutoka ofisi za wakubwa zao.lingekuwa swala hapa ni usalama mbona mpango ungekuwa rahisi tu vingewekwa vituo vya ukaguzi vichache na vinavyoeleweka na kazi ingeendelea bila lawama kutoka kwa wasafiri na wasafirishaji
 
Back
Top Bottom