Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Wanawake watatu waliojitambulisha kuwa ni Helen Mgaya (22), Robi Wambura (20) na Sophia Marwa (43) wote wakazi wa Kijiji cha Kebweye wilayani Tarime, Mkoa wa Mara, waliwaambia waandishi wa habari kuwa, Mei 4, mwaka huu walivamiwa na askari kadhaa wa Polisi na kudhalilishwa na askari hao.
Akielezea tukio hilo kwa upande wake, Mgaya alisema " ilikuwa ni tarehe nne mwezi uliopita (Mei), usiku, saa nane, walifika watu waliojitambulisha kuwa ni askari nyumbani kwangu na kunilazimisha nifungue mlango, nikagoma maana ni usiku sana nilijua ni majambazi, walilazimisha na kuvunja mlango kisha wakaingia na kuniuliza mume wangu yuko wapi, nikawaonesha,' alieleza Mgaya.
Alisema walimchukua mumewe na kumlazimisha avue nguo zote kisha wakamtoa nje na kumlaza kifudifudi kisha wakamchukua na shemeji yake (mdogo wa mumewe) na kufanya vivyo hivyo kisha wakamlazimisha …. ambapo alitii baada ya kutishiwa bastola na kupigwa.
Naye Wambura alisema siku hiyo hiyo walifika nyumbani kwake na kumfanyia kitendo hicho hicho na walipomaliza walikwenda kwa Marwa ambaye ni mkwe wa ukoo wa Mgaya na Wambura na alidai kuwa alipolazimishwa naye kuwanyonya watoto wake wa kiume, aligoma na kuwataka watu hao wamuue kuliko kufanya hivyo kwa watoto wake.
Source: Gazeti la Habari Leo
Akielezea tukio hilo kwa upande wake, Mgaya alisema " ilikuwa ni tarehe nne mwezi uliopita (Mei), usiku, saa nane, walifika watu waliojitambulisha kuwa ni askari nyumbani kwangu na kunilazimisha nifungue mlango, nikagoma maana ni usiku sana nilijua ni majambazi, walilazimisha na kuvunja mlango kisha wakaingia na kuniuliza mume wangu yuko wapi, nikawaonesha,' alieleza Mgaya.
Alisema walimchukua mumewe na kumlazimisha avue nguo zote kisha wakamtoa nje na kumlaza kifudifudi kisha wakamchukua na shemeji yake (mdogo wa mumewe) na kufanya vivyo hivyo kisha wakamlazimisha …. ambapo alitii baada ya kutishiwa bastola na kupigwa.
Naye Wambura alisema siku hiyo hiyo walifika nyumbani kwake na kumfanyia kitendo hicho hicho na walipomaliza walikwenda kwa Marwa ambaye ni mkwe wa ukoo wa Mgaya na Wambura na alidai kuwa alipolazimishwa naye kuwanyonya watoto wake wa kiume, aligoma na kuwataka watu hao wamuue kuliko kufanya hivyo kwa watoto wake.
Source: Gazeti la Habari Leo