Polisi Tanzania acheni kukurupuka na kufanya kazi kwa mihemuko (sensationalization). Mangula kuwa na sumu mwilini sio lazima mtu alitaka kumuua

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Ni pale tu Polisi wanapotoa matamko kama kusema Mangula amekutwa na sumu mwilini na hivyo kuna mtu alitaka kumuua watamtafuta kwa udi na uvumba, ndipo unagundua tuna jeshi la polisi lisilo professional, linakurupuka na kufanya kila njia kutaka kujikomba kwa CCM na uongozi uliopo madarakani.

Sikatai kwamba Mangula anaweza kuwa amekutwa na sumu mwilini, lakini suala la Polisi kusema chanzo cha hiyo sumu ni mtu kutaka kumuua Mangula wamelipata wapi? Kwa nini Polisi wanatoa matamko makubwa kama haya bila kuwa wamefanya uchunguzi wa kutosha, wakijua kwamba matamko kama hayo yanaweza kuleta machafuko nchini, iwe migongano baina ya CCM na vyama vya upinzani au ndani ya CCM?

Je, ni kwamba Polisi wamekosa hata chembe ya professionalism kujua kwamba ni mapema mno kutamka kwamba sumu katika mwili wa Mangula chanzo chake ni mtu fulani kutaka kumuua? Na kulikuwa na umuhimu gani wa kutoa hilo tangazo? Inawezekana hata Mangula alikula mihogo mibichi kwa kuamini inaongeza nguvu fulani mwilini, na ikatokea mihogo aliyokula ilikuwa na sumu ya cyanide kwa kiwango kikubwa, au haikumenywa sawasawa. Sasa utasema aliyemuuzia hiyo mihogo mibichi alitaka kumuua? Mangula ametoka kwenye kesi za kina Membe, Kinana na Makamba halafu unakurupuka kutoa matamko kama haya, ni busara kweli?

Chukulia mfano mwingine, ile ajali ya egg chops za Royal Bakery ambayo ilisababisha vifo vya watu kadhaa hapa Dar es Salaam. Ni wazi vifo hivyo vilitokana na sumu katika egg chops na sumu hiyo ingekutwa mwilini mwa waliokula egg chops. Sasa kwa namna hii, hawa Polisi wangekimbilia kusema hao watu kuna mtu aliwawekea hiyo sumu ingekuwaje? Si aibu tupu?

Tunatoa wito Polisi kuacha kufanya kazi kama waganga wa kienyeji bali wawe professional. Kutoa habari za namna hii wakati upelelezi haujafanywa kikamili ni kulidhalilisha jeshi la Polisi na Tanzania kwa ujumla. Pamoja na kuwa watu wanaweza kuwa na sumu mwilini kwa kuwekewa na watu wasio na nia njema, kuna sababu nyingi nyingine zinaweza kusababisha sumu mwilini, kama kula mihogo mibichi au almonds, au mbegu za apples na matunda mengine zenye kiwango kikubwa cha sumu ya cyanide. Hata karanga zisizokaangwa unaweza kula zikawa na aflatoxin ambayo ni sumu katika mwili wa mwanadamu.
 
Siri ya Polisi kutokuwa professional ni hii hapa!
tapatalk_jpeg_1582962299761.jpeg
 
Hao watu wana-exaggerate sana mambo hiyo labda ilikuwa ni "Food Poisoning" ambayo ni kitu cha kawaida kuweza kutokea kwa mtu yeyote yule.

Sasa watu kwa kutafutana ubaya wanatafuta mchawi na labda sasa kuna wanaolengwa kwa ajili ya ulipizwaji visasi.
 
Hao watu wana-exaggerate sana mambo hiyo labda ilikuwa ni "Food Poisoning" ambayo ni kitu cha kawaida kuweza kutokea kwa mtu yeyote yule.

Sasa watu kwa kutafutana ubaya wanatafuta mchawi na labda sasa kuna wanaolengwa kwa ajili ya ulipizwaji visasi.
Nimeshangaa sana Mkuu. Hivi hawa Polisi hapo ndio mwisho wa busara zao? Kwanza kulikuwa na haja gani ya kutangaza hata kama ingekuwa ni kweli kawekewa sumu - si ndio wnaharibu upelelezi? Kwa nini wasipeleleze kimya kimya? Hawajui kwamba kama ni kweli kuna mtu say alimlipa mtu amwekee sumu Mangula, kwa tangazo hili huyo mtu aliyelipwa atauwawa ili kuhakikisha siri haitoki? Wamesomea wapi hawa mambo ya upelelezi, Bagamoyo Mlingotini?
 
Synthesizer,
Ninyi wenye elimu ya hapa na pale mnasumbuaga sana jamii. Hujui kama madaktari wamegundua aina ya sumu ama la! Hujui madaktari wamegundua iliwekwa kwenye alichokula,hujui alihojiwa kote alipokula sikuhiyo nk. nk. Unaongea mambo ya miogo mibichi kwa matajiri wanaokula Serena hotel?? Angeeleza kala hayo makitu si ripoti ya daktari ingeweka bayana au wewe ni zaidi ya madaktari,wapelelezi,mapolisi waliomhoji huku wewe wala humjui!?

Usidhani nimtu kakurupuka kutangaza lazima imejadiliwa kwakina na kuonekana nivema ielezwe isifichwefichwe!!
Jamaa tuliza mtori nyama zikochini usifanye papara
 
Pengine Mangula roho ilimuuma kulazimishwa kumukuza Bernad Membe uwanachama wa CCM, akaamua kuchukua sheria mkononi kunywa sumu (Suicide).

Kaona wenzake waliokipigania CCM wameisha "BATIZWA KWA MOTO". Akaona a "SIGN OUT" mapema kabla na yeye hajabatizwa.
 
Ninyi wenye elimu ya hapa na pale mnasumbuaga sana jamii. Hujui kama madaktari wamegundua aina ya sumu ama la! Hujui madaktari wamegundua iliwekwa kwenye alichokula,hujui alihojiwa kote alipokula sikuhiyo nk. nk. Unaongea mambo ya miogo mibichi kwa matajiri wanaokula Serena hotel?? Angeeleza kala hayo makitu si ripoti ya daktari ingeweka bayana au wewe ni zaidi ya madaktari,wapelelezi,mapolisi waliomhoji huku wewe wala humjui!?
Usidhani nimtu kakurupuka kutangaza lazima imejadiliwa kwakina na kuonekana nivema ielezwe isifichwefichwe!!
Jamaa tuliza mtori nyama zikochini usifanye papara
Wewe umeiona ripoti ya madaktari? Maana unasema hujui, kwa hiyo wewe unajua?

Na hujaelewa mada. Kwani akila chakula chenye sumu Serena maana yake kuna mtu alitaka kumuua? Umepewa mfano wa egg chop lakini kwa kuwa una akili zito ya kijani umechagua kutoelewa.

Na amekutwa na sumu mwilini, sio chakula cha Serana chenye sumu tumboni!

Licha ya hivyo, kuna busara ya kutolipigia vuvuzela hili suala. Inasaidia nini kupiga vuvuzela badala ya kupeleleza kimya kimya?

Na umeambiwa labda alijiwekea sumu je? Sidhani kama Polisi wamefanya uchunguzi juu ya hilo ndio waka rule out!
 
Kila mtu; narudia tena kila mtu at any given time akipimwa kikamilifu ni lazima akutwe na viwango vya sumu tofauti tofauti mwilini...!!

Wao wangetwambia ni sumu gani? Nani amethibitisha?

Hiyo sumu inapatikana wapi? Inamwingiaje mtu mwilini (kwa kula, kuvuta au kwa kudungwa, nk)
Matumizi yake ni yepi?
Madhara yake yakoje?
Ni ya muda mrefu au mfupi?
Na je mhanga anaendeleaje?

NB: Wasitufanye siye wajinga sana?!!
 
Synthesizer,
Sumu KUVU ni sumu inayopatikana kwenye chakula cha nafaka, sijui kama maabara ya polisi na madakitari wao wanaijua hiyo. Wizara ya afya itueleze wananchi kama taarifa ya kulishwa sumu imetoka kwao.
 
Nakunywa soda ni sumu
Natumia sukari ni sumu
Natumia chumvi nyingi ni sumu
Sifanyi mazoez ya mwili mara kwa mara narundika sumu
Natumia mafuta ya viwandani ni sumu
Sinywi maji ya kutosha natengeneza sumu mwilini
Nakula kisha hapo hapo naingia kulala ni sumu
Ikiwezekana hata mke wa mtu natemmbea nae NI SUMU
Mangula ana sumu aina gani



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nakunywa soda ni sumu
Natumia sukari ni sumu
Natumia chumvi nyingi ni sumu
Sifanyi mazoez ya mwili mara kwa mara narundika sumu
Natumia mafuta ya viwandani ni sumu
Sinywi maji ya kutosha natengeneza sumu mwilini
Nakula kisha hapo hapo naingia kulala ni sumu
Ikiwezekana hata mke wa mtu natemmbea nae NI SUMU
Mangula ana sumu aina gani

Kwa uchungu ulio nao mkuu angalia wasije wakawa na shaka na wewe kuhusika. Maana uko kama unatoa utetezi wa kumpatia dhamana mshukiwa.

Sent from my iPhone using JamiiForums
 
brazaj akil ndogo tu inahitajika kuelewa comment yangu kuwa binadamu hata tufanyeje sumu tunazo katika miili yetu so wataalamu waachwe watoe ripot ya kueleweka


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
brazaj akil ndogo tu inahitajika kuelewa comment yangu kuwa binadamu hata tufanyeje sumu tunazo katika miili yetu so wataalamu waachwe watoe ripot ya kueleweka


Sent from my iPhone using JamiiForums

Unasomeka vyema mkuu. Ni wazi kuwa polisi hawa hawakuyasikia hata ya Kangi aliamua kulala nao mbele. Watayasikia ya muadhini?
 
Tatizo kubwa kwa sasa hapa Tanzania, Ni kila mtu kudhan anajua kila kitu. Mtoa mada unajaribu kutumia common sense kuzungumzia kitu professional. Umeongea maneno mengi ya laymen. Walau ungekuwa na knowledge japo kiduchu ya Forensic Pathology, nina uhakika usingeandika ulichokiandika. Polisi Tanzania wana mapungufu mengi kama taasisi inayoongozwa na wanadamu, wanakosea mengine kwa maksudi,tuwakosoe/ tuwapinge pale inapobidi. Lakin kabla ya kufanya hivyo, nasi tujielimishe kwa hivyo tunavyowakosoa ili katika kukosoa, tusionekane sisi ndio wajinga zaidi.
 
K
Synthesizer,
Ninyi wenye elimu ya hapa na pale mnasumbuaga sana jamii. Hujui kama madaktari wamegundua aina ya sumu ama la! Hujui madaktari wamegundua iliwekwa kwenye alichokula,hujui alihojiwa kote alipokula sikuhiyo nk. nk. Unaongea mambo ya miogo mibichi kwa matajiri wanaokula Serena hotel?? Angeeleza kala hayo makitu si ripoti ya daktari ingeweka bayana au wewe ni zaidi ya madaktari,wapelelezi,mapolisi waliomhoji huku wewe wala humjui!?

Usidhani nimtu kakurupuka kutangaza lazima imejadiliwa kwakina na kuonekana nivema ielezwe isifichwefichwe!!
Jamaa tuliza mtori nyama zikochini usifanye papara
Kwani Mangula ana nafasi gani kwenye serikali ya JMT?
 
Tatizo kubwa kwa sasa hapa Tanzania, Ni kila mtu kudhan anajua kila kitu. Mtoa mada unajaribu kutumia common sense kuzungumzia kitu professional. Umeongea maneno mengi ya laymen. Walau ungekuwa na knowledge japo kiduchu ya Forensic Pathology, nina uhakika usingeandika ulichokiandika. Polisi Tanzania wana mapungufu mengi kama taasisi inayoongozwa na wanadamu, wanakosea mengine kwa maksudi,tuwakosoe/ tuwapinge pale inapobidi. Lakin kabla ya kufanya hivyo, nasi tujielimishe kwa hivyo tunavyowakosoa ili katika kukosoa, tusionekane sisi ndio wajinga zaidi.
Mkuu sijui umri wako. Lakini nakwambia hata wewe unakiasi Fulani cha sumu mwilini ,sumu hizi ni matokeo ya chronic gradual acumulation jinsi umri unavyoenda..tinazipata hewani, kwenye maji, chakula, vipodozi, dawa mbalimbali tunazotumia na wakati mwingine impact inaweza kuonekana pale ikawa beyond the tolerable level of the body to handle it. Pia mtu anawepata acute poisoning kwa kupewa dose kubwa na wahalifu.
 
Back
Top Bottom