Polisi Na Makahaba

Mfamaji

JF-Expert Member
Nov 6, 2007
6,631
1,926
Polisi Jijini wazidi kuwasomba makahaba

2008-07-21 19:15:44
Na Moshi Lusonzo, Polisi Kati


Wanawake 21 na wanaume watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Ilala kwa tuhuma za kufumwa usiku wakidaiwa kufanya biashara ya ukahaba.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogire amesema wanawake hao na wanaume hao walikamatwa jana mishale ya saa 2:00 usiku katika baa za Kimboka, Asemwe na Sehewa silizopo Ilala.

Akasema wanawake hao walikamatwa wakiwa katika maeneo hayo wakituhumiwa kufanya biashara ya uchangudoa wakati wanaume hao wanatuhumiwa kuwa wateja.

Amesema watu hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Hivi hawa manjagu wa Kibongo wanaelewa kuwa ukahaba ni deal kwa wenzetu waliokwisha ona mbele? Wanalipa kodi na the game is authorised.
Hapa bongo badala ya kuhangaika na ujambazi wanahangaika na kina dada poa. Wanatumia magari, pikipiki ,mishahara etc kupamabana na wanaouza na kununua ngono. Can,t they set priorities?
 
Polisi Jijini wazidi kuwasomba makahaba

Hivi hawa manjagu wa Kibongo wanaelewa kuwa ukahaba ni deal kwa wenzetu waliokwisha ona mbele? Wanalipa kodi na the game is authorised.
Hapa bongo badala ya kuhangaika na ujambazi wanahangaika na kina dada poa. Wanatumia magari, pikipiki ,mishahara etc kupamabana na wanaouza na kununua ngono. Can,t they set priorities?


Heshima mbele mkuu, nafikiri katika hili huwatendei haki askari kwani biashara hii ni haramu kwa nchi kama Tanzania na ni haramu katika maadili yetu ya kitanzania.Kodi ya uchangudoa si tu ni chafu mbele za mungu lakini pia ni chafu mbele ya mtu yoyote mwenye mapenzi mema. Hili si wazo jema unalokuja nalo na ninafikiri hatutakiwi tufike mahala ambapo biashara ya ukahaba itahalalishwa ni kama kupigia debe kuhalalishwa uuzaji wa gongo mkuu!
 
[/I]

Heshima mbele mkuu, nafikiri katika hili huwatendei haki askari kwani biashara hii ni haramu kwa nchi kama Tanzania na ni haramu katika maadili yetu ya kitanzania.Kodi ya uchangudoa si tu ni chafu mbele za mungu lakini pia ni chafu mbele ya mtu yoyote mwenye mapenzi mema. Hili si wazo jema unalokuja nalo na ninafikiri hatutakiwi tufike mahala ambapo biashara ya ukahaba itahalalishwa ni kama kupigia debe kuhalalishwa uuzaji wa gongo mkuu!

Sawa mkuu. Sio lazima ihalalishwe. Lakini ni jambo linalotusumbua zaidi kuliko yote hadi wavalie njuga?. Tuna matatizo kibao zaidi ya uchangudoa.
 
Back
Top Bottom