Mocumentary
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 768
- 1,959
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amesema majeshi yote yameungana na tayari yamesambazwa kwenye mikoa mbali mbali
ikiwemo Arusha ili kusimamia uchaguzi mkuu utakaofanyika Jumatano ijayo Oktoba 28.
Sirro ametaja majeshi hayo kuwa ni Polisi wenyewe, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na Mgambo ambao tayari wapo Mkoani Arusha kwa
ajili ya zoezi la kuhakikisha utulivu unakuwepo siku ya kupiga kura.
Akizungumza akiwa mkoani Arusha, Sirro amesema anatambua kuwa kuna vikund ambavyo vimepangwa kwa ajili ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi na kuvuruga amani, hata hivyo watavikamata kabla ya siku usiku.
"Kuna vikundi vinataka kuharibu amani katika uchaguzi jijini Arusha vitakamatwa kabla ya siku ya uchaguzi ili kuondoa malengo yao ya kuharibu amani, "amesisitiza na kuongeza" Arusha imekuwa na historia ya vurugu tumeleta polisi wa kutosha kudhibiti wachache wanaotaka kufanya vurugu," amesema.
IGP amesema askari wanatakiwa kuhakikisha uchaguzi wa mwaka huu unakuwa wa amani na kudhibiti changamoto zozote ambazo zitajitokeza za kiusalama. Hata hivyo aliwataka wananchi watoe ushirikiano wanapohisi uvunjifu wa amani ili hatua haraka zichukuliwe.
Chanzo: Habari leo
ikiwemo Arusha ili kusimamia uchaguzi mkuu utakaofanyika Jumatano ijayo Oktoba 28.
Sirro ametaja majeshi hayo kuwa ni Polisi wenyewe, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na Mgambo ambao tayari wapo Mkoani Arusha kwa
ajili ya zoezi la kuhakikisha utulivu unakuwepo siku ya kupiga kura.
Akizungumza akiwa mkoani Arusha, Sirro amesema anatambua kuwa kuna vikund ambavyo vimepangwa kwa ajili ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi na kuvuruga amani, hata hivyo watavikamata kabla ya siku usiku.
"Kuna vikundi vinataka kuharibu amani katika uchaguzi jijini Arusha vitakamatwa kabla ya siku ya uchaguzi ili kuondoa malengo yao ya kuharibu amani, "amesisitiza na kuongeza" Arusha imekuwa na historia ya vurugu tumeleta polisi wa kutosha kudhibiti wachache wanaotaka kufanya vurugu," amesema.
IGP amesema askari wanatakiwa kuhakikisha uchaguzi wa mwaka huu unakuwa wa amani na kudhibiti changamoto zozote ambazo zitajitokeza za kiusalama. Hata hivyo aliwataka wananchi watoe ushirikiano wanapohisi uvunjifu wa amani ili hatua haraka zichukuliwe.
Chanzo: Habari leo