kamili
JF-Expert Member
- Feb 10, 2011
- 1,213
- 849
Ni kawaida unapokuwa Mbeya kusikia mtu au watu wamepigwa nondo kichwani na majambazi na kuporwa mali. Na wakati mwingine matukio hayo hutokea hata jirani na police.
Mwaka jana tukio moja liliwakumba police wawili wakiwa wamevaa kiraia na kupelekea moja kufariki kwa kupigwa nondo na hao majambazi.
Matukio hayo yameanza muda mrefu sana, zaidi ya miaka 10 sasa. Wiki ya jana watu wasiopungua watano walilazwa hospitali ya rufaa Mbeya kwa kupigwa vichwani na nondo.
Juzi tumeona kule Songea watu wasiokuwa na silaha wameuwawa na police, lakini pia police wamelaumiwa mara nyingi kwa kuua watu wasiokuwa na hatia katika matukio kadhaa.
Swali langu ni kuwa kwa nini police haitumii maguvu yake kudhibiti vitendo vya kihalifu kama hivi vya ujambazi wa nondo na badala yake huelekeza maguvu hayo kwa watu wasio na hatia wala silaha?
Na tena wasiwasi wangu mkubwa ipo siku wakazi wa Mbeya wataandama kuwasilisha kilio chao hicho na bila ya shaka kama ilivyo kawaida police watawauwa waandamanaji kikatili.
Naomba mjadala kwa wana JF nini kifanyike kuepusha hali hiyo.
Mwaka jana tukio moja liliwakumba police wawili wakiwa wamevaa kiraia na kupelekea moja kufariki kwa kupigwa nondo na hao majambazi.
Matukio hayo yameanza muda mrefu sana, zaidi ya miaka 10 sasa. Wiki ya jana watu wasiopungua watano walilazwa hospitali ya rufaa Mbeya kwa kupigwa vichwani na nondo.
Juzi tumeona kule Songea watu wasiokuwa na silaha wameuwawa na police, lakini pia police wamelaumiwa mara nyingi kwa kuua watu wasiokuwa na hatia katika matukio kadhaa.
Swali langu ni kuwa kwa nini police haitumii maguvu yake kudhibiti vitendo vya kihalifu kama hivi vya ujambazi wa nondo na badala yake huelekeza maguvu hayo kwa watu wasio na hatia wala silaha?
Na tena wasiwasi wangu mkubwa ipo siku wakazi wa Mbeya wataandama kuwasilisha kilio chao hicho na bila ya shaka kama ilivyo kawaida police watawauwa waandamanaji kikatili.
Naomba mjadala kwa wana JF nini kifanyike kuepusha hali hiyo.