Wanajukwaa Salaam!
Naomba niwaeleze snario iliyopo Polisi Wilaya ya Masasi Mkoa wa MTWARA.
Iko Hivi, tarehe 27 oct 2021 kulitokea tukio la kukamatana masuala ya ugoni.
Bwana J ndiye Mwenye Mke ambaye baada ya kumuona mkewe amebadilika kitabia na mienendo yake mibaya aliamua kumfuatilia kwa ukaribu. Hivyo katika kufuatilia aliweka mitego yake na ndipo siku 40 za mwizi zilitimia.
Baada ya mtego kukamilika aliwachukua ndugu zake 7 ambapo walifika kwenye guest wakawakuta. Mgoni aliambiwa waende polisi lakini kabla ya kufika hatua ya kwenda polisi mgoni aliomba msamaha na kutaka wayamalize.
Jamaa akaagiza kwa kijana wake amletee fedha pale alipokuwepo. Kweli ililetwa ambapo Mwenye mke alikuwa analazimisha waende polisi lakini mgoni alikataa na kutaka wayamalize.
Mgoni alipoletewa fedha alimtaka Mwenye Mke aweze kupokea fedha kiasi cha Milioni 5! Kweli ndugu wa jamaa Mwenye mke walimsihi wayamalize kwa mtindo huo na kumfichia aibu mkewe kwa kuwa tayari yameshatokea.
Hoja yangu siyo kueleza hayo Bali Ni matukio baada ya Jambo Hilo kumalizika kule guest.
Ndugu zangu Wana jamii! Baada ya tukio, yule aliyeshikwa Alikwenda polisi na kugeuza kesi kwamba amekabwa na kutekwa na Yule Mwenye mke na kwamba wamlazimisha amtume mwanaye kuleta fedha.
Polisi walichofanya wakamkamata Mwenye mke na mkewe na mmoja wa ndugu yake wakawaweka ndani toka tarehe 28/10 Hadi leo tarehe 07 Nov 2021 Ni siku ya 11 wapo selo ya polisi Wilaya na hawajapekwa japo mahakamani.
Kumbe jamaa amewalipa fedha polisi na kuwaambia wahakikishe wanamkomesha Mwenye mke anarudisha fedha. Na Mwenye mke amesema hatarudisha fedha Ila Kama kweli mgoni wake alichowaeleza Ni kweli wakamalize mahakamani.
Suala sasa limebakia hapo na sasa Mgoni hapokei simu na hata akipigiwa simu anakata na anazima simu.
Ndugu wamekwenda Hadi kwa DC na DC alimuagiza OCD awaachie lakini OCD amekaidi. Ukweli kunapoendelea Ni kubaya baina ya familia hii na Jeshi la Polisi na kwa taarifa kunafanyika organization watu wanataka kuandamana Kama walivyofanya wakati wa gesi ya Mtwara na kwa mnaokumbuka ilileta madhara makubwa mno na ikumbukwe chanzo hasa kilikuwa Ni hao polisi kupitia kwa traffic mmoja.
Waziri Simbachawene tambua hili.
Waziri Mwambe Jofrey na (Mb) wa Jimbo la Masasi tambua hili.
Polisi MASASI wanafanya Jambo la hatari Sana.
Naomba niwaeleze snario iliyopo Polisi Wilaya ya Masasi Mkoa wa MTWARA.
Iko Hivi, tarehe 27 oct 2021 kulitokea tukio la kukamatana masuala ya ugoni.
Bwana J ndiye Mwenye Mke ambaye baada ya kumuona mkewe amebadilika kitabia na mienendo yake mibaya aliamua kumfuatilia kwa ukaribu. Hivyo katika kufuatilia aliweka mitego yake na ndipo siku 40 za mwizi zilitimia.
Baada ya mtego kukamilika aliwachukua ndugu zake 7 ambapo walifika kwenye guest wakawakuta. Mgoni aliambiwa waende polisi lakini kabla ya kufika hatua ya kwenda polisi mgoni aliomba msamaha na kutaka wayamalize.
Jamaa akaagiza kwa kijana wake amletee fedha pale alipokuwepo. Kweli ililetwa ambapo Mwenye mke alikuwa analazimisha waende polisi lakini mgoni alikataa na kutaka wayamalize.
Mgoni alipoletewa fedha alimtaka Mwenye Mke aweze kupokea fedha kiasi cha Milioni 5! Kweli ndugu wa jamaa Mwenye mke walimsihi wayamalize kwa mtindo huo na kumfichia aibu mkewe kwa kuwa tayari yameshatokea.
Hoja yangu siyo kueleza hayo Bali Ni matukio baada ya Jambo Hilo kumalizika kule guest.
Ndugu zangu Wana jamii! Baada ya tukio, yule aliyeshikwa Alikwenda polisi na kugeuza kesi kwamba amekabwa na kutekwa na Yule Mwenye mke na kwamba wamlazimisha amtume mwanaye kuleta fedha.
Polisi walichofanya wakamkamata Mwenye mke na mkewe na mmoja wa ndugu yake wakawaweka ndani toka tarehe 28/10 Hadi leo tarehe 07 Nov 2021 Ni siku ya 11 wapo selo ya polisi Wilaya na hawajapekwa japo mahakamani.
Kumbe jamaa amewalipa fedha polisi na kuwaambia wahakikishe wanamkomesha Mwenye mke anarudisha fedha. Na Mwenye mke amesema hatarudisha fedha Ila Kama kweli mgoni wake alichowaeleza Ni kweli wakamalize mahakamani.
Suala sasa limebakia hapo na sasa Mgoni hapokei simu na hata akipigiwa simu anakata na anazima simu.
Ndugu wamekwenda Hadi kwa DC na DC alimuagiza OCD awaachie lakini OCD amekaidi. Ukweli kunapoendelea Ni kubaya baina ya familia hii na Jeshi la Polisi na kwa taarifa kunafanyika organization watu wanataka kuandamana Kama walivyofanya wakati wa gesi ya Mtwara na kwa mnaokumbuka ilileta madhara makubwa mno na ikumbukwe chanzo hasa kilikuwa Ni hao polisi kupitia kwa traffic mmoja.
Waziri Simbachawene tambua hili.
Waziri Mwambe Jofrey na (Mb) wa Jimbo la Masasi tambua hili.
Polisi MASASI wanafanya Jambo la hatari Sana.