wanajf naomba tujadili uhalali wa jesh la polisi kutumia risasi za moto kwa lengo la kumwokoa M/kiti wa kijiji kigamboni baada ya kutekwa na wanakijiji wake baada kutokea vurugu kati yao na police baada ya kuondolewa kwa nguvu ktk eneo lao la kuchimba kokoto. .Je ni halali kwa polisi kufanya hvyo? Je hakuna mbinu mbadala mpaka kutumia risasi za moto? Je kutumia risasi za moto haiamshi hasira zaidi kwa wananchi? Hatujaonyeshwa kama wananchi walikuwa na silaha za hatari je inatoa tafsiri gani kwa jeshi letu-? Kwa wanaojua sheria tupeni ufafanuzi kwa hili jambo.SOURCE ITV