Elections 2010 Polisi kupewa posho ya shs 5000/= Igunga, watasimamia haki?

Dullo

JF-Expert Member
Oct 24, 2009
251
64
Nimesoma katika gazeti la Mtanzania la leo linasema kuwa Polisi walioko Igunga wanalipwa posho ya shs. 5,000/= kwa siku na imethibitishwa na mkuu wao Isaya Mgulu eti naye amesema anapata hiyo hiyo, hii inawezekana kweli mtu kulipwa 5000/= halafu akasimamia haki katika uchaguzi?

Hii naona imekaa vibaya na inachochea rushwa kwa polisi siku ya uchaguzi na kuondoa usawa, jamani hivi kweli mtu akalale nje kwa pesa hiyo halafu asijihusishe na uharifu?

Nawasilisha kwa wanaJF!!
 
Kilo moja ya nyama, duh,nao wamekubali!Watanzania mavuvuzela kweli.Kwa mtindo huu kwa kweli, wana haki ya kusindikiza malori ya sukari kwenda Kenya.
Nimesoma katika gazeti la Mtanzania la leo linasema kuwa Polisi walioko Igunga wanalipwa posho ya shs. 5,000/= kwa siku na imethibitishwa na mkuu wao Isaya Mgulu eti naye amesema anapata hiyo hiyo, hii inawezekana kweli mtu kulipwa 5000/= halafu akasimamia haki katika uchaguzi?

Hii naona imekaa vibaya na inachochea rushwa kwa polisi siku ya uchaguzi na kuondoa usawa, jamani hivi kweli mtu akalale nje kwa pesa hiyo halafu asijihusishe na uharifu?

Nawasilisha kwa wanaJF!!
 
Duh!!! hiyo kali yaani hata posho ya mwanafunzi wa elimu ya juu anawazidi,kweli hii country inafurahisha sana!!! kwa nini tusifanye reform kama wenzetu pale Kenya ambapo nafasi ya IGP na wasaidizi wake wanne wana apply hizo nafasi,sio kupeana kama njugu!!!
 
nyie hawa watu si wa kutetea maana hawana maana, kwanza ndio wa kwanza kuwageuka watetea haki wkitumiwa na haohao wanaowalalamikia, acha wakione cha moto ili akili iwakae sawa
 
Back
Top Bottom