Polisi: Kifo cha Mwanafunzi wa Skuli ya Laurent, hakihusiani na kipigo

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Jeshi la Polisi mkoa wa Kusini Pemba limekanusha kuhusu tukio la kifo cha mwanafuzni wa skuli ya Laurent International kuwa halihusiani na kupigwa na mwalimu.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kusini Pemba Mh, Sheikhan Mohd Sheikhan amesema kifo cha Saleh Abdallah Massoud aliyekuwa mwanafunzi wa skuli hiyo iliyopo Ole Kianga Mkoa wa Kusini Pemba hakikutokana na kupigwa na mwalimu kama inavyodaiwa na walio wengi bali kimechangiwa na kuumwa na Figo, Ini pamoja na uvimbe katika shingo yake.

Akizungumza na wandishi wa habari jana huko ofisini kwake Madungu Chakechake Pemba amesema mnamo tarehe 30/05/2017 majira ya saa 5: 00 asubuhi walipokea taarifa ya kifo cha mwanafunzi huyo na ndipo walipochukua hatua za haraka kufika skulini hapo kuwahoji walimu pamoja na wanafunzi wa skuli hiyo na katika taarifa za awali uchunguzi ulibaini kwamba mwanafunzi huyo alipata adhabu baada ya kuharibu midoli ya kufundishia wanafunzi wa chekechea skulini hapo.

Shekhan amesema, mtoto huyo kabla ya hapo awali alipata kuanguka chooni na kuumia sehemu ya bega la mkono wa kulia na alianza kupatiwa matibabu ya awalii na daktari wa skuli hata hivyo hali haikua nzuri na kulazimika kupelekwa hospitali ya Chakechake na Mwanamashungi kwa matibabu zaidi.

Amefahamisha kuwa 25.05.2017 baba wa mtoto huyo alifika skulini hapo kwa ajili ya kumchukua na kwenda nae nyumbani kwa lengo la kumpeleka hospitali ya Wete kwa matibabu zaidi aliruhusiwa kurudi nae nyumbani na ilipofika 29/05/2017 alirejeshwa tena hospitali ya Wete na kulazwa na hatimae majira ya saa 8:00 alifariki dunia.

Amesema kutokana na uchunguzi wa daktari aliyemtibu katika hospitali ya Wete aligundua kuvimba kwa shavu la kulia , uvimbe usio na maumivu mbeleni mwa shingo, uvimbe kwenye mguu wa kulia, umanjano wa macho na hakua na jeraha lolote wala sehemu yeyote iliyotoka damu wala mkwaruzo au alama zisizo za kawaida.

Pia vipimo vingine vilionesha kuwa alikuwa na upungufu wa damu, kuumwa na Figo pamoja na Ini na sio kujeruhiwa na kupelekea hali yake kuwa mbaya na hatimae kufariki dunia.

Aidha amesema kwa sasa wanawashikilia watu saba na uchunguzi ukikamilika watapandishwa mahakamani kwa kujibu shtaka la uzalilishaji pomoja na uzembe na sio shtaka la mauaji.

Pemba News Midea
 
siku zote chung usiwe sababu ya kifo cha mtu..itakupotezea muda na uelekeo wa maisha..
 
Back
Top Bottom