Nilikuwa nafuatilia usaili wa polisi wapya nchini Kenya katika tv siku kama tatu zimepita . Kigezo chao kikubwa ni kwamba anayeomba nafasi ya kujiunga na upolisi ni lazima awe na DIPLOMA yeyote ile alafu vigezo vingine ndio vifuatie
Yaani askari wa kenya pamoja na ukorofi wao lakini elimu ipo tofauti kabisa na huku kwetu tz
Elimu Kenya ni kipau mbele, nilikua na fundi mkata mbao porini. Huyu jamaa ni mkenya ana Advance diploma in Carpentry and Mason. Alikua anauchambua uchumi wa Africa na mwenendo wa ongezeko la watu. Dah nilijiona mtupu mbele yake wakati yeye wakati huo alikua kibarua wangu wa siku, typical wage worker.
Is that so??!
Sidhani kama ni kweli usaili ulikuwa unachukuwa waliomaliza Form IV na wenye kuanzia C- na kuendelea
Waliokuwa na D- na kushuka chini hawakusailiwa ila hiyo ya kuwa na Diploma sikuisikia mimi
Nadhani anazungumzia vetting ya kamishna wa polisi na makamu wake. Viegezo nadhani zaidi ya diploma.