Demi
JF-Expert Member
- Nov 22, 2016
- 37,240
- 79,057
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Polisi wasio na weledi ndio wanakimbilia kutumia silaha, Polisi majambazi ndio wanaua watu na kuwabatiza ujambazi, Polisi wa mambosasa mwenye fremu za maduka 100 mabwepande ndio deal likibuma wanakuondosha usijewataja.Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu na kukamata silaha moja bastola aina ya REVOLVER.
Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa inasema kuwa Mnamo tarehe 11/05/2021 majira ya saa tatu usiku huko Mbagala jirani na ukumbi wa Dar Live majambazi wapatao watatu wakiwa kwenye Pikipiki namba MC 640 CGT aina ya TVS wakijiandaa kufanya ujambazi kwenye maduka na vibanda vya miamala ya fedha, lakini kabla hawajatimiza azma yao ya kufanya uhalifu.
Taarifa hiyo imesema Kikosi kazi cha kupambana na ujambazi cha Kanda Maalum Dar es Salaam kilipata taarifa na kujipanga vizuri, ambapo ilipofika majira saa nne usiku majambazi hao wakiwa kwenye pikipiki walipewa amri ya kusimama lakini walikaidi amri hiyo na kuanza kuwarushia askari risasi, ndipo askari wakajibu mashambulizi na kufanikiwa kuwapiga risasi sehemu mbalimbali za miili yao na kufariki dunia papo hapo.
"Kikosi hicho kilifanya ukaguzi kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kupata silaha moja Bastola aina REVELVOR ikiwa na risasi tatu ndani ya magazine na walipopekuliwa kwenye miili yao walikutwa na risasi tano za bunduki ambayo haifahamiki ni ya aina gani." Imeeleza
JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DSM KUIMARISHA USALAMA SIKUKUU YA EID EL-FITRI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu ya Eid el-fitri inayotarajiwa kuadhimishwa tarehe 13/05/2021 au 14/05/2021 pindi itakapothibitishwa na Mh. Mufti wa Tanzania.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawaasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kusherehekea sikukuu ya Eid El-fitri kwa amani na utulivu na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa sheria.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha Wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.
Pia wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea pekenyao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.
Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo.
Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limepiga marufuku Disko toto katika kumbi zote za starehe za hapa Jijini Dar es Salaam.
Vilevile Madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.
Hata hivyo Jeshi la polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawaomba Wananchi kuendelee kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa namba zifuatazo 0653616277, 0755980633 na 0769360416.
Ulikuwepo ukaona anatupa risasi?? Polisi mwenye weledi hawezi kurushiwa risasi kwa sababu hafanyi confrontation ya mhalifu.Unamkamata mtu anakutupia risasi?
Mambosasa katishiwa kuondolewa Dsm ataua sana hata kuloga ataloga ili mradi aonekane anafanyakazi! Ukweli mambosasa amekaa sana kanda maalumu atoke aletwe kamanda mwingine haraka sana.Mmmhhh mara mmeanza kuua?
Msije mkawa mnatengeneza stori
Kwa nini kila siku huwa mnaua tu hamuwezi kuwakamata na kuwapeleka mahakamani?
Nyie haya
Kutulinda mpaka mshitukizwe mpange tukio weledi mmh mmh upo kweri au show?
Hili jeshi kwa kweri
Wake polisi wa patrol mafuta hiwa wanapata wapi,polisi wa defender??Unajitia dole na kujilamba.!!
Ikiwa sudden event,polisi sometimes huwa hawana mafuta au gari mbovu maana hao jamaa maisha yao ni magumu na hata vitendea kazi kwao ni changamoto hasa mafuta kwao imekuwa mtihani usiofanyika sijui ile bajeti inayopitishwa pale bungeni huwa inaishia wapi!jamaa wamekuwa wakiendesha kazi zao kwa kuomba sapoti kwetu sisi 'wadau wa polisi'.
Ila tukio kama hili 'liloripotiwa' ni planned event hivyo iliwachua rahisi polisi kujiandaa kivyote(gari+mfuta &nguvu kazi).
Watoto watajifunza ujambazi ni mbaya na unaweza kuuwawa kwa ajili ya ujambaziMsiwe mnatutangazia asee, watoto wetu watajifunza nini. Waueni kimya kimya.
Utafiiiiiii.....waBAWACHA soma hiyo
Ni Mambosasa. Baada ya kuona kula yake inatikiswa. Ni hatari kwani wanaweza kuua na wasi na hatia ili kuonysha wako makiniPongezi kwa jeshi, yule askari machachari wa kupambana na majambazi kisharudi?
Waongeze masnichi mtaani.
Everyday is Saturday...............................
Weka hadithi ya kwako ambayo hawakutupa risasi tuijadili.Ulikuwepo ukaona anatupa risasi?? Polisi mwenye weledi hawezi kurushiwa risasi kwa sababu hafanyi confrontation ya mhalifu.
Tutaamini vipi kwamba hao majambazi hawakuwa wameshaiba tayari pesa nyingi, na hao polosi wakaamua kuwafanyia ujambazi hao majambazi kisha wakapoteza ushahidickwa kuwamaliza? Tutaamini vipi?! Maana Zombe alituondolea imani kabisa kwa jeshi la polisi, hiyo imani haitakaa iridi tena!!!Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu na kukamata silaha moja bastola aina ya REVOLVER.
Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa inasema kuwa Mnamo tarehe 11/05/2021 majira ya saa tatu usiku huko Mbagala jirani na ukumbi wa Dar Live majambazi wapatao watatu wakiwa kwenye Pikipiki namba MC 640 CGT aina ya TVS wakijiandaa kufanya ujambazi kwenye maduka na vibanda vya miamala ya fedha, lakini kabla hawajatimiza azma yao ya kufanya uhalifu.
Taarifa hiyo imesema Kikosi kazi cha kupambana na ujambazi cha Kanda Maalum Dar es Salaam kilipata taarifa na kujipanga vizuri, ambapo ilipofika majira saa nne usiku majambazi hao wakiwa kwenye pikipiki walipewa amri ya kusimama lakini walikaidi amri hiyo na kuanza kuwarushia askari risasi, ndipo askari wakajibu mashambulizi na kufanikiwa kuwapiga risasi sehemu mbalimbali za miili yao na kufariki dunia papo hapo.
"Kikosi hicho kilifanya ukaguzi kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kupata silaha moja Bastola aina REVELVOR ikiwa na risasi tatu ndani ya magazine na walipopekuliwa kwenye miili yao walikutwa na risasi tano za bunduki ambayo haifahamiki ni ya aina gani." Imeeleza
JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DSM KUIMARISHA USALAMA SIKUKUU YA EID EL-FITRI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu ya Eid el-fitri inayotarajiwa kuadhimishwa tarehe 13/05/2021 au 14/05/2021 pindi itakapothibitishwa na Mh. Mufti wa Tanzania.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawaasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kusherehekea sikukuu ya Eid El-fitri kwa amani na utulivu na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa sheria.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha Wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.
Pia wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea pekenyao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.
Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo.
Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limepiga marufuku Disko toto katika kumbi zote za starehe za hapa Jijini Dar es Salaam.
Vilevile Madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.
Hata hivyo Jeshi la polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawaomba Wananchi kuendelee kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa namba zifuatazo 0653616277, 0755980633 na 0769360416.
Huyu Mambosasa anahaha sana kujisafishaVyema.
Ila isijekuwa ni Mambosasa anataka kujihalalishia nafasi yake kwa kuwachapa risasi raia.
Wambura sio?Pongezi kwa jeshi, yule askari machachari wa kupambana na majambazi kisharudi?
Waongeze masnichi mtaani.
Everyday is Saturday...............................