Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu na kukamata silaha moja bastola aina ya REVOLVER.

Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa inasema kuwa Mnamo tarehe 11/05/2021 majira ya saa tatu usiku huko Mbagala jirani na ukumbi wa Dar Live majambazi wapatao watatu wakiwa kwenye Pikipiki namba MC 640 CGT aina ya TVS wakijiandaa kufanya ujambazi kwenye maduka na vibanda vya miamala ya fedha, lakini kabla hawajatimiza azma yao ya kufanya uhalifu.

Taarifa hiyo imesema Kikosi kazi cha kupambana na ujambazi cha Kanda Maalum Dar es Salaam kilipata taarifa na kujipanga vizuri, ambapo ilipofika majira saa nne usiku majambazi hao wakiwa kwenye pikipiki walipewa amri ya kusimama lakini walikaidi amri hiyo na kuanza kuwarushia askari risasi, ndipo askari wakajibu mashambulizi na kufanikiwa kuwapiga risasi sehemu mbalimbali za miili yao na kufariki dunia papo hapo.

"Kikosi hicho kilifanya ukaguzi kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kupata silaha moja Bastola aina REVELVOR ikiwa na risasi tatu ndani ya magazine na walipopekuliwa kwenye miili yao walikutwa na risasi tano za bunduki ambayo haifahamiki ni ya aina gani." Imeeleza

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DSM KUIMARISHA USALAMA SIKUKUU YA EID EL-FITRI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu ya Eid el-fitri inayotarajiwa kuadhimishwa tarehe 13/05/2021 au 14/05/2021 pindi itakapothibitishwa na Mh. Mufti wa Tanzania.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawaasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kusherehekea sikukuu ya Eid El-fitri kwa amani na utulivu na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa sheria.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha Wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.

Pia wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea pekenyao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.

Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo.

Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limepiga marufuku Disko toto katika kumbi zote za starehe za hapa Jijini Dar es Salaam.

Vilevile Madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.

Hata hivyo Jeshi la polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawaomba Wananchi kuendelee kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa namba zifuatazo 0653616277, 0755980633 na 0769360416.
Polisi wasio na weledi ndio wanakimbilia kutumia silaha, Polisi majambazi ndio wanaua watu na kuwabatiza ujambazi, Polisi wa mambosasa mwenye fremu za maduka 100 mabwepande ndio deal likibuma wanakuondosha usijewataja.

Kumbuka mnaowaua wana wategemezi wao ambao wataathirika maisha bila hatia, kumbuka laana mnayoitengeneza mpaka kizazi chenu cha tatu itawatafuna hata mkiwa kaburini.

Mh. Samiah badilisha uongozi wa polisi makao makuu, mpe mtu ambaye ni kweli analipenda jeshi na amefanya utafiti mpaka amepata PhD ya kazi za Polisi zinavyotakiwa kuendeshwa atarudisha heshima ya taasisi hii ambayo wananchi wanaichekea mdomoni moyoni wanalia, wanaiogopa hawaipendi, wanahofu nayo na wala hawaiheshimu.

Wapo polisi wamewekeza kwenye uhalifu wanafanya uhalifu ndio kitega uchumi wanashiriki moja kwa moja ujambazi nakisha rais ukiwalaumu hawafanyi kazi wanatafuta wa kuwatoa kafara wakuridhishe. Inauma sana.
 
Mmmhhh mara mmeanza kuua?
Msije mkawa mnatengeneza stori
Kwa nini kila siku huwa mnaua tu hamuwezi kuwakamata na kuwapeleka mahakamani?
Nyie haya
Kutulinda mpaka mshitukizwe mpange tukio weledi mmh mmh upo kweri au show?
Hili jeshi kwa kweri
Mambosasa katishiwa kuondolewa Dsm ataua sana hata kuloga ataloga ili mradi aonekane anafanyakazi! Ukweli mambosasa amekaa sana kanda maalumu atoke aletwe kamanda mwingine haraka sana.
 
Unajitia dole na kujilamba.!!
Ikiwa sudden event,polisi sometimes huwa hawana mafuta au gari mbovu maana hao jamaa maisha yao ni magumu na hata vitendea kazi kwao ni changamoto hasa mafuta kwao imekuwa mtihani usiofanyika sijui ile bajeti inayopitishwa pale bungeni huwa inaishia wapi!jamaa wamekuwa wakiendesha kazi zao kwa kuomba sapoti kwetu sisi 'wadau wa polisi'.

Ila tukio kama hili 'liloripotiwa' ni planned event hivyo iliwachua rahisi polisi kujiandaa kivyote(gari+mfuta &nguvu kazi).
Wake polisi wa patrol mafuta hiwa wanapata wapi,polisi wa defender??


Wakiingia sheli wanajichotea tu mafuta acha kutetea ujinga
 
Pongezi kwa jeshi, yule askari machachari wa kupambana na majambazi kisharudi?
Waongeze masnichi mtaani.

Everyday is Saturday............................... :cool:
Ni Mambosasa. Baada ya kuona kula yake inatikiswa. Ni hatari kwani wanaweza kuua na wasi na hatia ili kuonysha wako makini
 
Nakumbuka ile issue ya akina Zombie,ilianza kuripotiwa kama hii "eti polisi wamekuwa majambazi" Kila mtu akaamini,mwisho wa siku ukweli ukawekwa wazi,kumbe waliouwawa walikuwa ni wafanyabiashara ya madini tena Wana ndugu,very sad story.
 
Ulikuwepo ukaona anatupa risasi?? Polisi mwenye weledi hawezi kurushiwa risasi kwa sababu hafanyi confrontation ya mhalifu.
Weka hadithi ya kwako ambayo hawakutupa risasi tuijadili.
Hii iliyopo inasema walitupa risasi.
Kipimo cha weledi wakati wa vita si somo jepesi.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu na kukamata silaha moja bastola aina ya REVOLVER.

Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa inasema kuwa Mnamo tarehe 11/05/2021 majira ya saa tatu usiku huko Mbagala jirani na ukumbi wa Dar Live majambazi wapatao watatu wakiwa kwenye Pikipiki namba MC 640 CGT aina ya TVS wakijiandaa kufanya ujambazi kwenye maduka na vibanda vya miamala ya fedha, lakini kabla hawajatimiza azma yao ya kufanya uhalifu.

Taarifa hiyo imesema Kikosi kazi cha kupambana na ujambazi cha Kanda Maalum Dar es Salaam kilipata taarifa na kujipanga vizuri, ambapo ilipofika majira saa nne usiku majambazi hao wakiwa kwenye pikipiki walipewa amri ya kusimama lakini walikaidi amri hiyo na kuanza kuwarushia askari risasi, ndipo askari wakajibu mashambulizi na kufanikiwa kuwapiga risasi sehemu mbalimbali za miili yao na kufariki dunia papo hapo.

"Kikosi hicho kilifanya ukaguzi kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kupata silaha moja Bastola aina REVELVOR ikiwa na risasi tatu ndani ya magazine na walipopekuliwa kwenye miili yao walikutwa na risasi tano za bunduki ambayo haifahamiki ni ya aina gani." Imeeleza

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DSM KUIMARISHA USALAMA SIKUKUU YA EID EL-FITRI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu ya Eid el-fitri inayotarajiwa kuadhimishwa tarehe 13/05/2021 au 14/05/2021 pindi itakapothibitishwa na Mh. Mufti wa Tanzania.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawaasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kusherehekea sikukuu ya Eid El-fitri kwa amani na utulivu na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa sheria.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha Wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.

Pia wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea pekenyao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.

Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo.

Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limepiga marufuku Disko toto katika kumbi zote za starehe za hapa Jijini Dar es Salaam.

Vilevile Madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.

Hata hivyo Jeshi la polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawaomba Wananchi kuendelee kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa namba zifuatazo 0653616277, 0755980633 na 0769360416.
Tutaamini vipi kwamba hao majambazi hawakuwa wameshaiba tayari pesa nyingi, na hao polosi wakaamua kuwafanyia ujambazi hao majambazi kisha wakapoteza ushahidickwa kuwamaliza? Tutaamini vipi?! Maana Zombe alituondolea imani kabisa kwa jeshi la polisi, hiyo imani haitakaa iridi tena!!!
 
Safi sana.

Dawa ya moto ni moto.

safi sana na pongezi kwa Jeshi letu la polisi kwa kazi nzuri

kamwe msiwaache majambazi wavunje heshima ya Jeshi letu la polisi, hilo haliwezekani, tuwaahidi kutoa ushirikiano kuwafichua majambazi wote na wezi katika mitaa yetu.
 
Tulitoa tahadhari kwa majambazi baada ya kauli ya Mh SSH ,watakula vyuma sana wasipoacha ujambazi ,dawa ya jambazi hakuna kujadiliana nae ni kumlisha chuma tu na mtandao wao wote.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom