Polisi jamii, mbinu hii inazuia uhalifu au inachochea?

ntagunga

JF-Expert Member
Aug 13, 2011
654
256
Tangu 2006, Jeshi la Polisi Tanzania lilizindua mfumo mpya wa kiutendaji ambapo ilizindua POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI.

Maana halisi ya dhana hii ni kwamba kuna uwezekano wa kuwa na jamii ambayo haina uhalifu. .Kufikia hili ndipo jamii nzima inatakiwa iwe mdau wa kuhahakisha kuwa uhalifu unapingwa/
jamii nzima kushiriki katika ulinzi.

Kufanikisha mkakati huu, Jeshi la polisi linamtaka kila mwana jamii ashiriki katika ulinzi kama sheria inayounda serikali za mitaa inavyotaka. Kuna namna nyingi za kushiriki katika hili, nitazitaja mbili tu:-
1. Ni kuzuia vyanzo vya uhalifu katika jamii.
Katika kufanikisha hili, Jeshi la polisi linahimiza kila mwana jamii kuwajibika na kutoa huduma anayotakiwa kuitoa kwa uaminifu. kwa kufanya hivyo huduma bora kwa jamii zitapatikana na hivyo inakuwa ni chanzo cha kuwa na jamii/wanajamii wanaojitosheleza na hivyo kuziba mianya ya watu katika kuwa wahalifu.

Mjia hii inaaminika kuwa inaweza kuzuia uhalifu kwa kiwango kikubwa kwa kuwa, inaaminika kuwa wahalifu wengi, hawafanyi uhalifu kwa utashi wao binafsi, bali hulazimishwa na mifumo dhalimu kwa kuwa inakuwa haitoi huduma bora, inatelekeza watu wake na hivyo huamua kujitafutia maisha mazuri na hivyo kupelekea watu kuwa wahalifu.


2. Jeshi linaitaka jamii kuanzisha vikundi vya ulinzi katika mitaa, kuwa na daftari maalulu la ubalozi kufahamu nani kaingia nani katoka, kutoa taarifa za kuwepo kwa mipango ya kuvuruga amani na utulivu, na kuwa na maamuzi yenye baraka toka kwa wanajamii/uongozi wa jamii husika.

Katika hili, uhalifu mwingi hutokea kwa kuwa baadhi ya viongozi wanmejifanya miungu watu na kudiriki kuamua maamuzi yanayoathiri watu wengi peke yao. Kwa kuwa maamuzi hayo si sehemu ya jamii, wanajamii watayakataa na hivyo kupelekea uvunjifu wa amani. Hivyo jeshi linawataka viongozi kushirikisha jamii/viongozi wenzao.

Je dhana hii ikisimamiwa inatusaidia au ndo itazidisha taabu katika jamii ya ktanzania?

maoni yako nayahitaji ewe mdau wa jamii forum
 
Tangu 2006, Jeshi la Polisi Tanzania lilizindua mfumo mpya wa kiutendaji ambapo ilizindua POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI.

Maana halisi ya dhana hii ni kwamba kuna uwezekano wa kuwa na jamii ambayo haina uhalifu. .Kufikia hili ndipo jamii nzima inatakiwa iwe mdau wa kuhahakisha kuwa uhalifu unapingwa/
jamii nzima kushiriki katika ulinzi.

Kufanikisha mkakati huu, Jeshi la polisi linamtaka kila mwana jamii ashiriki katika ulinzi kama sheria inayounda serikali za mitaa inavyotaka. Kuna namna nyingi za kushiriki katika hili, nitazitaja mbili tu:-
1. Ni kuzuia vyanzo vya uhalifu katika jamii.
Katika kufanikisha hili, Jeshi la polisi linahimiza kila mwana jamii kuwajibika na kutoa huduma anayotakiwa kuitoa kwa uaminifu. kwa kufanya hivyo huduma bora kwa jamii zitapatikana na hivyo inakuwa ni chanzo cha kuwa na jamii/wanajamii wanaojitosheleza na hivyo kuziba mianya ya watu katika kuwa wahalifu.

Mjia hii inaaminika kuwa inaweza kuzuia uhalifu kwa kiwango kikubwa kwa kuwa, inaaminika kuwa wahalifu wengi, hawafanyi uhalifu kwa utashi wao binafsi, bali hulazimishwa na mifumo dhalimu kwa kuwa inakuwa haitoi huduma bora, inatelekeza watu wake na hivyo huamua kujitafutia maisha mazuri na hivyo kupelekea watu kuwa wahalifu.


2. Jeshi linaitaka jamii kuanzisha vikundi vya ulinzi katika mitaa, kuwa na daftari maalulu la ubalozi kufahamu nani kaingia nani katoka, kutoa taarifa za kuwepo kwa mipango ya kuvuruga amani na utulivu, na kuwa na maamuzi yenye baraka toka kwa wanajamii/uongozi wa jamii husika.

Katika hili, uhalifu mwingi hutokea kwa kuwa baadhi ya viongozi wanmejifanya miungu watu na kudiriki kuamua maamuzi yanayoathiri watu wengi peke yao. Kwa kuwa maamuzi hayo si sehemu ya jamii, wanajamii watayakataa na hivyo kupelekea uvunjifu wa amani. Hivyo jeshi linawataka viongozi kushirikisha jamii/viongozi wenzao.

Je dhana hii ikisimamiwa inatusaidia au ndo itazidisha taabu katika jamii ya ktanzania?

maoni yako nayahitaji ewe mdau wa jamii forum

maoni yako ni mhimu sana kwa ustawi wa jeshi lakini pia unaweza kusaidia kulifanya jeshi liwajibike ipasavyo
 
tunataka maisha bora kwa kila mtanzania. Polisi=umbea. Sie wengine sio wambea. Nalog off

mkuu, maisha bora kwa kila mtanzania, si ndo kauli mbiu ya JK? Tumeyapata? Tatizo la mpango mkakati wa polisi jamii ya Mwema, unaingiliwa sana na wakuu, hivyo kila siku mtu unashindwa utekeleze kipi uache kipi. Kwa mfano, kuna sehemu uchaguzi umeharibiwa. Uchunguzi huru ukifanywa, tutabaini kuwa viongozi wa eneo hilo waliridhia ucaguzi kuharibiwa kwa manufaa yao. Hap nazungumzia kamati za ulinzi na usalama za maeneo husika.

Nadhani polisi jamii ingekusanya habari za kiintelijensia, na kuwatia nguvuni wote wanaopanga kuhujumu chaguzi hizo lakini wapi, kamati zenyewe ndizo zinabariki michoro ya wizi wa kura.
 
tufanyeje ili wote wanaojiita watumishi wa umma wawe watumishi wa uma kwelikeli?
 
mkuu, maisha bora kwa kila mtanzania, si ndo kauli mbiu ya JK? Tumeyapata? Tatizo la mpango mkakati wa polisi jamii ya Mwema, unaingiliwa sana na wakuu, hivyo kila siku mtu unashindwa utekeleze kipi uache kipi. Kwa mfano, kuna sehemu uchaguzi umeharibiwa. Uchunguzi huru ukifanywa, tutabaini kuwa viongozi wa eneo hilo waliridhia ucaguzi kuharibiwa kwa manufaa yao. Hap nazungumzia kamati za ulinzi na usalama za maeneo husika.

Nadhani polisi jamii ingekusanya habari za kiintelijensia, na kuwatia nguvuni wote wanaopanga kuhujumu chaguzi hizo lakini wapi, kamati zenyewe ndizo zinabariki michoro ya wizi wa kura.
Kama hata Mwema anaingiliwa basi hakuna sababu ya kupoteza muda wetu kwenye jambo kama hili. Nalog off
 
Kama hata Mwema anaingiliwa basi hakuna sababu ya kupoteza muda wetu kwenye jambo kama hili. Nalog off

tunaweza kujadili ili kuibuka na hoja nzito itakayowafanya watendaji wa serikali wasiingiliwe katika kazi zao. log on washwashw
 
tunaweza kujadili ili kuibuka na hoja nzito itakayowafanya watendaji wa serikali wasiingiliwe katika kazi zao. log on washwashw
Ndugu yangu serikali hii ya ccm kubadilika ni vigumu kama kufanya mapenzi na tembo. Nalog off
 
kabla hawajaleta hoja ya polisi jamii walitakiwa wafanye mabadiliko makubwa yenye tija ndani ya polisi,halafu waijenge upya imani waliyoipoteza toka kwa wananchi then ndio waje na kupandikiza wazo la polisi jamii.

Kwanza waache kuitwa Jeshi la polisi hili neno jeshi linawajengea dhana ya matumizi ya nguvu katika kila jambo/maamuzi dhidi ya wanaotakiwa kuwatumikia yaani wananchi.

Wamekuwa mabwana badala ya kuwa watwana.tukifanya nao polisi jamii watakuwa wakitutuma badala ya kushirikiana nao,watakuwa wakitukosoa badala ya kutufunza,watatufunja nguvu kwa kuchukua rushwa toka kwa watuhumiwa na kutuachuia visasi ktk jamii.
 
kabla hawajaleta hoja ya polisi jamii walitakiwa wafanye mabadiliko makubwa yenye tija ndani ya polisi,halafu waijenge upya imani waliyoipoteza toka kwa wananchi then ndio waje na kupandikiza wazo la polisi jamii.

Kwanza waache kuitwa Jeshi la polisi hili neno jeshi linawajengea dhana ya matumizi ya nguvu katika kila jambo/maamuzi dhidi ya wanaotakiwa kuwatumikia yaani wananchi.

Wamekuwa mabwana badala ya kuwa watwana.tukifanya nao polisi jamii watakuwa wakitutuma badala ya kushirikiana nao,watakuwa wakitukosoa badala ya kutufunza,watatufunja nguvu kwa kuchukua rushwa toka kwa watuhumiwa na kutuachuia visasi ktk jamii.

Nashukuru kwa mchango wako mzuri. Na mabadiliko ndani ya Jeshi bado, kitu hiki ndicho kinachopelekea askari kutokuwa waaminifu katika kazi zao. Mwema amejitahidi kwa kiasi fulani lakini bado hajafikia ile hatua inayotakiwa kuwafanya askari wawe wawajibikaji kwa jamii yao.

Na hilo ulilosema wasiitwe Jeshi la polisi, mbadala wake ni nini?
 
Nashukuru kwa mchango wako mzuri. Na mabadiliko ndani ya Jeshi bado, kitu hiki ndicho kinachopelekea askari kutokuwa waaminifu katika kazi zao. Mwema amejitahidi kwa kiasi fulani lakini bado hajafikia ile hatua inayotakiwa kuwafanya askari wawe wawajibikaji kwa jamii yao.

Na hilo ulilosema wasiitwe Jeshi la polisi, mbadala wake ni nini?


Kaka Ntagunga

kwa nchi zilizoona tatizo matatizo ya dhana hiyo ya utumiaji nguvu na unyanyasaji wa Raia wanawaita Idara ya Polisi (Police Department au police Service)

Mfano wa karibu:
Following the promulgation of the new Constitution of Kenya on 27 August 2010, as laid down in Chapter 17 Part 4 of the said document, the Kenyan police forces shall undergo a series of reforms. Hence called The Kenya Police Service, it shall be headed by an Inspector-General and the division of its functions shall be organized to take into account the devolved structure of government in Kenya.

Nimetohoa kipengele toka website ya kenya police service inasema "The just concluded Constitutional review holds a promise for the establishment of an emancipated Police Service, that will operate in conformity with democratic transformation from the current practice of Regime Policing to Democratic Policing (Community Policing)

Mwema amjitahidi kufanya mabadiliko Pongezi ila anaweka mvinyo mpya kwenye kiriba cha zamani=Mvinyo utachacha tu.
 
Back
Top Bottom