Bubu Msemaovyo
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 3,832
- 2,790
Hakika kama huamini utaamini hili ninalosema, kabla ya kuanzisha mfumo wa vyama vingi ulitolewa mwito kwa vyombo vya usalama kujihusisha na siasa. Kadri siku zilivyosonga mbele mwitikio wa wananchi kwa vyama vya upinzani umekuwa ukiongezeka hivyo kupunguza idadi ya wanachama wa CCM toka katika makabrasha yake kwa sababu nyingi moja wapo wengi wao kuona chama cha CCM kukosa mwelekeo, kupoteza dira nk.
Mauaji yaliyoshamiri hivi karibuni dhidi ya wananchi wanaoviunga vyama vya upinzani yameongezeka sana, hii inaashiria kuwa askari polisi bado wana itikadi ya chama cha CCM japo kadi hawana. Kadi za chama hiki kwa polisi hawa ziko mioyoni mwao. Wanazo kwa njia mbili aidha kwa matakwa yao yasiyo na maslahi au kwa kulazimishwa na viongozi waandamizi wa CCM.
Tunawataka Polisi waachane na tabia ya kuegemea upande mmoja wa chama wawapo kazini kwani kama tunavyoona kuna athari kubwa sana kwa maisha ya raia. Aidha tunawataka wanasiasa wa CCM waache kuwatumia polisi kulazimisha wananchi kukiunga mkono chama cha CCM.
Mauaji yaliyoshamiri hivi karibuni dhidi ya wananchi wanaoviunga vyama vya upinzani yameongezeka sana, hii inaashiria kuwa askari polisi bado wana itikadi ya chama cha CCM japo kadi hawana. Kadi za chama hiki kwa polisi hawa ziko mioyoni mwao. Wanazo kwa njia mbili aidha kwa matakwa yao yasiyo na maslahi au kwa kulazimishwa na viongozi waandamizi wa CCM.
Tunawataka Polisi waachane na tabia ya kuegemea upande mmoja wa chama wawapo kazini kwani kama tunavyoona kuna athari kubwa sana kwa maisha ya raia. Aidha tunawataka wanasiasa wa CCM waache kuwatumia polisi kulazimisha wananchi kukiunga mkono chama cha CCM.