babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,398
- 3,243
Habarini wandugu, Leo asubuhi nimesikiliza maoni ya bwana mmoja kuhusu polisi na wajibu wao hakika amenifurahisha.
Kwanza kabisa ametolea mfano polisi wa mataifa yaliyoendelea jinsi wanavotimiza wajibu wao kwa haki ili kukwepa baadae kugeuziwa kibao.
Mfano polisi anapomkamata mtuhumiwa
(1). Anatakiwa awe na vitambulisho vinavyomtambulisha yeye ni nani.
(2). Wajibu wa kumueleza mtuhumiwa ni kwa nini anakamatwa.
(3). Kumueleza mtuhumiwa ni nini haki zake wakati wa kupelekwa kituoni.
(4). Kutotumia nguvu na vitisho wakati wa kumpeleka mtuhumiwa kama yeye hakupinga kwenda kwa hiari yake.
(5). Akimfikisha kituoni mtuhumiwa huelezwa tena haki zake upya na huulizwa iwapo polisi walitumia nguvu wakati wa kumleta kituoni.
Kwa kweli kama polisi wetu wangetumia njia hizo hapo juu hakika wangekua marafiki na raia.
Kinyume chake tunashuhudia kila cku polisi wakitumia nguvu na vitisho pale wanapomkamata mtuhumiwa na tena wengine bila hata kujitambulisha huku wakijua wamevalia kiraia.
Sasa fika kituoni utaambiwa kwa lugha kali vua viatu toa mkanda na vitisho vingine vingi.
Mtuhumiwa yampasa kujua haki zake pale kituoni kama muda wa kukaa pale kabla ya kufikishwa mahakamani uwepo wa wakili wake wakati wa kutoa maelezo kama ana wakili na mengine yanayostahili pale kama haki yake.
Pia polisi ama wanajua au hawajui ni kipi kifanyike na kwa wakati gani ili kuepusha vurugu na kutoaminiwa na wananchi kama ilivo sasa.
Tunataka polisi mjue wajibu wenu ili mjenge imani mpya kwa wananchi.
Kwa kweli ni maoni mema kwa jeshi la polisi kujivua gamba.
Kwanza kabisa ametolea mfano polisi wa mataifa yaliyoendelea jinsi wanavotimiza wajibu wao kwa haki ili kukwepa baadae kugeuziwa kibao.
Mfano polisi anapomkamata mtuhumiwa
(1). Anatakiwa awe na vitambulisho vinavyomtambulisha yeye ni nani.
(2). Wajibu wa kumueleza mtuhumiwa ni kwa nini anakamatwa.
(3). Kumueleza mtuhumiwa ni nini haki zake wakati wa kupelekwa kituoni.
(4). Kutotumia nguvu na vitisho wakati wa kumpeleka mtuhumiwa kama yeye hakupinga kwenda kwa hiari yake.
(5). Akimfikisha kituoni mtuhumiwa huelezwa tena haki zake upya na huulizwa iwapo polisi walitumia nguvu wakati wa kumleta kituoni.
Kwa kweli kama polisi wetu wangetumia njia hizo hapo juu hakika wangekua marafiki na raia.
Kinyume chake tunashuhudia kila cku polisi wakitumia nguvu na vitisho pale wanapomkamata mtuhumiwa na tena wengine bila hata kujitambulisha huku wakijua wamevalia kiraia.
Sasa fika kituoni utaambiwa kwa lugha kali vua viatu toa mkanda na vitisho vingine vingi.
Mtuhumiwa yampasa kujua haki zake pale kituoni kama muda wa kukaa pale kabla ya kufikishwa mahakamani uwepo wa wakili wake wakati wa kutoa maelezo kama ana wakili na mengine yanayostahili pale kama haki yake.
Pia polisi ama wanajua au hawajui ni kipi kifanyike na kwa wakati gani ili kuepusha vurugu na kutoaminiwa na wananchi kama ilivo sasa.
Tunataka polisi mjue wajibu wenu ili mjenge imani mpya kwa wananchi.
Kwa kweli ni maoni mema kwa jeshi la polisi kujivua gamba.