Nimepata taarifa za kusikitisha kutoka mkoa wa Geita. Taarifa zinadai kwamba, juzi kati ya saa moja jioni, askari polisi wapatao 8 wakiwa na silaha nzito za kivita-SMG- 'walimteka' kisha kumkamata, wakampiga na kumuumiza vibaya kwa kumpasua mishipa midogo ya damu katika jicho la kushoto, Mwandishi wa habari Salumu Maige, anayeandikia gazeti la Mwananchi na Redio Free Afrika huko Geita. Polisi walikuwa na gari Namba PT 1998-OCD Geita. Mwenye taarifa zaidi atujuze!.